Je, Rais Samia Suluhu ndo Deng Xiaoping wa Tanzania?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Amani iwe nanyi wadau

Leo ninakuja na Swali hili, Je, Rais Samia Suluhu Hassan ndo Deng Xiaoping wa Tanzania?

Kwa wale msiojua Deng Xiaoping ni Rais wa China aliyechukua usukani wa Uongozi wa China baada ya kifo cha Rais wa Kwanza wa China Mao Zedong. Mao Zedong alijulikana kwa wachina kama Rais mwenye msimamo mkali usioyumba ambaye hakupatana na Marekani na nchi za Magharibi. Aliiongoza China Kwa mkono wa Chuma ila katika kipindi chake China ilikuwa nchi yenye uchumi mbovu sana kutokana na Sera zake za kukataa uwekezaji kutoka nje na kugombana na nchi za magharibi.

Kwa wachina wengi pamoja na kumuheshimu sana Mao ila wanamchukulia Deng Xiaoping Kama Baba wa Mapinduzi ya Kiuchumi ya China. Hii ni Kwa sababu Deng Xiaoping ndo mtu aliyekuja kutengeneza China yenye siasa za kikomunist Ila yenye uchumi imara wa kibepari ulioongozwa na msemo wake “It doesn’t matter if a cat is white or black , as long as it catches a mice, it’s a good cat”

Kwa wasioelewa kimombo Deng Xiaoping alikuwa anamaanisha haijalishi paka ni mweupe au mweusi Ila ingawa anakamata panya basi huyo ni paka mzuri

Sera hii ya Deng Xiaoping ndo ilisababisha China kuanza kukaribisha uwekezaji mkubwa kutoka Magharibi ulioingiza fedha na mitaji mikubwa nchini China na hatimaye Leo hii China ni Taifa la pili kwa kuwa na uchumi mkubwa na maendeleo duniani na inasemekana ndani ya muda mchache atachukua nafasi ya kwanza na kuizidi Marekani.

Jana nimetoka kuongea na rafiki yangu ambaye ni mkurugenzi wa moja ya mabenki hapa nchini na ameniambia kweli sasa biashara imeanza kupaa. Wiki iliyo pita nilikuwa Mwanza na Arusha na kote wafanyabiashara wa ma hoteli wanasema biashara imeanza kuja juu sana saivi

Leo Hii ninapoandika huu uzi Kuna Rafiki yangu mwingine ameniambia Kuna wawekezaji wamekuja na wana mtaji wa pesa ndefu wameanza taratibu za kufanya uwekezaji wao hapa Tanzania.

Swali langu kwenu nyie wadau leo ni Je Rais Samia Suluhu Hassan ndo Deng Xiaoping wa Tanzania???

Uzi huu nitaufufua 2030 Inshallah tukiwepo Rais Samia akiwa anamaliza Urais wake( hapa naamini Chama chake kitampitisha kugombea tena 2025-2030

Muwe na jioni njema wanabodi!!
 
Ni ngumu kumtabiri huyu mama, ila so far so good.

Naona dalili ya nchi kufunguka sana kwa mda kidogo. She is bold ktk mambo anayoyaamini. Let us give her time to implement her views
 
Ni ngumu kumtabiri huyu mama, ila so far so good.

Naona dalili ya nchi kufunguka sana kwa mda kidogo. She is bold ktk mambo anayoyaamini. Let us give her time to implement her views
Kwa haya maoni ninazidi kuamini kuwa itakuwa ndo yeye mwenyewe!

Kweli tuzidi kumpa muda
 
Ni mapema mno kumpa hadhi ya Deng xiao Ping mama Samia. Biashara unayosema inapaa ni ya kufikirika kwani mitaani hela bado sana. Akiwa na utashi wa kisiasa Samia atatufikisha pazuri ila Level ya Deng, sidhani.

Deng ni mwanasiasa bora kwa kukuza uchumi wa nchi kutoka umaskini hadi utajiri ndani ya muda wa kizazi kimona. Deng ameweza kuthibitizha kuwa demokrasia sio muhimu sana kuewza kupiga hatua ya maendeleo.

Huyo ndio Deng the great, he has no equal in modern era leadership of a society.mwaka wa kwanza wa uongozini aliita wanasayansi na kuwauliza kuwa mnahitaji pesa kiasi gani tuweze kuwaibia teknolojia wamarekani ili tuwafikie ndani ya miaka 30 kiteknolojia . Walimwambia tunahitaji dola 15 bilioni.

Deng aliwapa 30 bilioni na kuwaambia anzeni Kazi. Leo wachina wako hapo..Ndio slogan yake kuwa it down,t matter whether a cat is black or white,provided it catches a mouse ilivyoshika mshiko,maana alidhamiria alete maendeleo bila demokrasia , ndio maana mwaka 1989 vijana walioxI demokrasia walipondwa na vifaru kea amri yake pale Tianan men square.

Ushupavu wa Deng Samia hawezi na pia jamii anayoongeza haujafikia kiwango cha wachina enzi hizo.
 
Ni mapema mno kumpa hadhi ya Deng xiao Ping mama Samia. Biashara unayosema inapaa ni ya kufikirika kwani mitaani hela bado sana. Akiwa na utashi wa kisiasa Samia atatufikisha pazuri ila Level ya Deng, sidhani. Deng ni mwanasiasa bora kwa kukuza uchumi wa nchi kutoka umaskini hadi utajiri ndani ya muda wa kizazi kimona. Deng ameweza kuthibitizha kuwa demokrasia sio muhimu sana kuewza kupiga hatua ya maendeleo. Huyo ndio Deng the great, he has no equal in modern era leadership of a society.mwaka wa kwanza wa uongozini aliita wanasayansi na kuwauliza kuwa mnahitaji pesa kiasi gani tuweze kuwaibia teknolojia wamarekani ili tuwafikie ndani ya miaka 30 kiteknolojia . Walimwambia tunahitaji dola 15 bilioni. . Deng aliwapa 30 bilioni na kuwaambia anzeni Kazi. Leo wachina wako hapo..Ndio slogan yake kuwa it down,t matter whether a cat is black or white,provided it catches a mouse ilivyoshika mshiko,maana alidhamiria alete maendeleo bila demokrasia , ndio maana mwaka 1989 vijana walioxI demokrasia walipondwa na vifaru kea amri yake pale Tianan men square. Ushupavu wa Deng Samia hawezi na pia jamii anayoongeza haujafikia kiwango cha wachina enzi hizo.
Well said
 
Well said
Umesema vyema kuhusu Deng ku crack down Democracy. Ila huoni Samia ameendeleza katazo la mikutano ya hadhara ya kisiasa? Kuna tofauti gani hapo???

Juzi tu nimeona vikao vikirushwa tbc vya wadau wakianza kutoa maoni juu ya kubadili mtaala wa Elimu Tanzania. Je huoni Samia anatembea humo humo???

Umesikia mipango yake na alivyoanza kufanya juu ya uwekezaji ili kukuza ajira na kuleta maendeleo? Huoni nae anatembea mule mule kwa Deng The Great??
 
Back
Top Bottom