Je, Profesa Assad aongezewe ulinzi?

Je, Profesa Assad aongezewe ulinzi?

View attachment 1061459

Huyu mtu kiukweli anayajua madudu mengi mno ya nchi hii , na kwa jinsi ya maelezo ya kamati ya maadili ya bunge , kuna chuki kubwa sana iliyochanganyika na wivu wa kimasikini uliojaa ushamba mkubwa sana ndani yake dhidi ya Assad.

Nashauri kwenye kipindi hiki cha mpito Profesa huyu aongezewe ulinzi .

Wenye akili wamenielewa .
Hata mimi naona aongezewe ulinzi.
Hasa ukizingatia cdm hawana pa kushika kwa sasa,wanaweza wakamdhuru halafu wakaanza kuimba nyimbo za kuisingizia serekali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini humfahamu Prof Assad,aliotufundisha UDSM tunamjua vizuri sana ndio maana hata alipoitwa na Kamati ya Maadili bado alisimamia msimamo wake,unadhani alikuwa hajui nini kitafuata? Ogopa sana mtu anaemcha Mungu kwa dhati na akiwa Msomi wa kiwango cha Prof Assad,sidhani kama hata anahitaji hizo teuzi za Ubalozi!
Mkuu pammoja na Uprofesa wake,na kumjua vizuri alipokuwa mwalimu wako,watu wamepenya humo humo kumkatisha,na kumfedhehesha alipoonekana amekuwa too much kwao.
Hii ndio Bongo walikuwepo kama yeye wengi tu lakini walionja joto ya jiwe.
Kama -:
Tutemeke Sanga
Dr Kyaruzi
Titi Mohamed
Kasela Bantu
Oscar Kambona
Choga
Professor Rweyemamu
Mtei
Professor Babu
 
View attachment 1061459

Huyu mtu kiukweli anayajua madudu mengi mno ya nchi hii , na kwa jinsi ya maelezo ya kamati ya maadili ya bunge , kuna chuki kubwa sana iliyochanganyika na wivu wa kimasikini uliojaa ushamba mkubwa sana ndani yake dhidi ya Assad.

Nashauri kwenye kipindi hiki cha mpito Profesa huyu aongezewe ulinzi .

Wenye akili wamenielewa .
Atapewa ulinzi na watu dhaifu????????? Maana ukisema bunge dhaifu maana yake serikali dhaifu na kwa sababu yeye Prof Assad ni sehemu ya serikali basi na yeye ni goigoi, hivyo hana haja ya ulinzi, apambane na hali yake. Na kinachoshangaza ni kwanini anashindwa kuelewa alikosea????
 
tusaidiane uelewa kidogo, suala aliloibua mkaguzi hasa unaosemekana ni upotevu wa matrilioni ya kodi na kutamka kuwa kuna udhaifu bungeni ni janga kubwa sana la kitaifa sababu nadharia ya separation of power na checks and balance ya bongo mimi kama msomi wa Mlimani wa dhana hiyo naamini hiyo ishu imebaki vitabuni tu tangu kuanzishwa kwake kwa maslahi ya watawala na maisha yameendelea sasa huyu bwana mkubwa ameamsha popo! sasa hapa tunapoteza muda tu kujadili, sababu tukikubali izungumzwe ina maana tunahitaji kufumua nchi! hiyo ikimaanisha bunge kwanza liwe laivu kwakuwa ni kituko kukutuma ukaniwakilishe (mpiga kura) halafu eti unafanya siri yale unayoniwakilisha (mbunge) na pia bunge litahitaji kuwa na wabunge angalau wenye digrii na uelewa wa kutosha kiakili (miswada mingine ni mizito inahitaji wasomi tu ) bunge litahitaji wabunge wenye kuwajibika kwa wananchi na sio executive ( wanaosema ndiooooooo!) , bunge litahitajika kuibana serikali kisawasawa ikiwepo kupiga kura za kutokuwa na imani na waheshimiwa ikibidi , bunge likianzisha maazimio ya kukataa kupitisha bajeti za executive wasizozielewa na kuhoji na kupeleka mahakamani taarifa za upotevu wa pesa za umma unaosomeka kwenye ripoti za CAG na pia mahakama itahitaji kuwaburuza mahakamani na kuwatupa jela watendaji wote wa executive wanaofanya matumizi mabaya ya pesa za umma, wanaotumia vibaya madaraka yao na wanaovunja katiba na sheria za nchi na hasa ukwiukwaji wa haki za binadamu bila kuangalia vyeo vyao na mamlaka zao! Habari njema ni kuwa mambo hayo yatawezekana katika kipindi cha miaka 60 toka sasa baada ya genge zima la watu fulani wenye athari za utawala wa kikoloni wote kutimkia kwenye udongo!!
hili aliloibua mkaguzi ni jambo zito mno kwa maslahi ya nchi kwa wasiojua!!
ni vizuri sana Mzee akikaa pembeni sasa kwa maana pongezi kwake yeye mwenye hofu ya Mungu.
Elimu ya wabunge sidhani kama ni tatizo sana kwenye ( japo elimu ni muhimu sana ) , ukiangalia wote waliopanga njama hii wanayo elimu ya kuridhisha tu , tatizo kubwa ni kutumikishwa na kutii hata ujinga .
 
View attachment 1061459

Huyu mtu kiukweli anayajua madudu mengi mno ya nchi hii , na kwa jinsi ya maelezo ya kamati ya maadili ya bunge , kuna chuki kubwa sana iliyochanganyika na wivu wa kimasikini uliojaa ushamba mkubwa sana ndani yake dhidi ya Assad.

Nashauri kwenye kipindi hiki cha mpito Profesa huyu aongezewe ulinzi .

Wenye akili wamenielewa .
Aongezewe ulinzi kwa lipi? au kwa hizo predictions unazotoa?
 
Ni jukumu la wananchi wenyewe kujitolea na kujiorganise kumpa ulinzi masaa 24 KUANZIA SASA HIVI. Ulinzi wa kweli na sahihi kwake ndiyo huo. Unajua wengine wanaweza kuondoa ulinzi wanapojisikia.
 
Hawatamuachia moja kwa moja...

Kuna kazi zingine atapangiwa ili aendelee kubaki ndani ya system...


Cc: mahondaw
 
Hivi kikatiba hawezi kuacha kazi au? Ni wakati wake kutafakari na kuacha kazi hii ili arudi kufundisha wanafunzi wake na kufanya consultancy zake na ile firm yake. To be frank kwa elimu na weledi alio nao huyu Mwalimu aliyetukuka na mpenda haki na mwenye weledi na uadilifu wa kazi basi ni vyema arudi kwa familia yake. Ulinzi wa Allah ukae naye popote.

Pia ni vyema ajihami sana kuanzia ofisini kwake na kwa wote ambao wako karibu naye kwa kipindi hiki. Awe extra carefully.

Ila sasa kwa kipindi hiki ambacho serikali iko makini kwa matumizi ya mapato yake na ikampata mtu mzuri kama ASSAD imekuwaje tena kuwe na mtafaruku huu mkubwa? Ni kitu cha watanzania kuangalia kwa jicho la pili na maombi sana ya kumuomba Mungu aondoe huu ukungu uliop.
 
Hivi kikatiba hawezi kuacha kazi au? Ni wakati wake kutafakari na kuacha kazi hii ili arudi kufundisha wanafunzi wake na kufanya consultancy zake na ile firm yake. To be frank kwa elimu na weledi alio nao huyu Mwalimu aliyetukuka na mpenda haki na mwenye weledi na uadilifu wa kazi basi ni vyema arudi kwa familia yake. Ulinzi wa Allah ukae naye popote.

Pia ni vyema ajihami sana kuanzia ofisini kwake na kwa wote ambao wako karibu naye kwa kipindi hiki. Awe extra carefully.

Ila sasa kwa kipindi hiki ambacho serikali iko makini kwa matumizi ya mapato yake na ikampata mtu mzuri kama ASSAD imekuwaje tena kuwe na mtafaruku huu mkubwa? Ni kitu cha watanzania kuangalia kwa jicho la pili na maombi sana ya kumuomba Mungu aondoe huu ukungu uliop.
Je ni kweli kwamba serikali iko makini kwenye matumizi ya mapato yake ?
 
Je ni kweli kwamba serikali iko makini kwenye matumizi ya mapato yake ?
Angalao kwa Serikali ya Awamu ya Tano nimeona Mh. Rais Mwenyewe akitumia hata inteligensia yake kufuatilia na hata kwa taasiis za serikali kujaribu kupunguza au kuacha kabisa yale matumizi ya hovyo. Mfano safari za nje ambazo hazikuwa hata na tija sana zimeweza kubanwa na mengine kama hayo. Wezi wa pesa za miradi nao wameogopa sana hata kama wanakula ila watakuwa wanakula kwa kuvizia sana. Sasa kumpata mtu kama CAG ambaye yuko makini na kufukua makaburi ya wezi nilitegemea Mh. Rais angemtetea kwa nguvu zote kwa kuwa ni mkono wake wa kumsaidia katika mauala ya pesa.

Ndiyo maana nikasema watanzania tumwombe sana Mungu kila mmoja kwa imani yake ili Mh. Rais aweze kuufahamu mchezo unaoendelea. Nikasema zaidi kuwa angetumia hata timu zaidi ya moja ya usalama wa taifa kuchunguza hili SAKATA kwa kuwa unajae wenye pesa wanaweza kuyumbusha tu ili CAG aondolewe ili waendelee na ule wizi wao. Money is the strongest weapon!!!!
 
Back
Top Bottom