Je, ni sawa mwanaume kumfulia nguo mwanamke?

Je, ni sawa mwanaume kumfulia nguo mwanamke?

Mkuu achana na haya mambo. Nyumba zina mambo mengi. Ina maana wewe huwezi mfulia mkeo nguo?
Yawezekana anaumwa
Au yawezekana huyo mwanaume yupo kazini yaani DOBI
Conclusion it depends on the situation. ( Mimi huwa nikiwa naumwa au kipibdi mjamzito au nimejifungua huwa ananifulia)

Hapo lazima patakuwa uswazi kwa jinsi ufuaji unafanyikia hadharani.
 
Huo ni wajibu wako. Utaona nnavyokujali pindi unadharura ya msingi, kinyume napo kwanini usifue mwenyewe?

Ndio nimekwambia kusaidiana jamani.Kuna siku mtu unaamka mwili hautaki kufanya kazi yoyote na nguo zimejaa kwanini usinisaidie jamani Mashaxizo!??
 
Last edited by a moderator:
Kama unaweza kumnunulia simu
Ka. A Unaweza kumnunulia gari
Kama unaweza kumnyonya papuchi

Kama unaweza.......

Kwanini ushindwe kumfulia ?
 
Kama kuvua kutanifanya niwe "jinsia ya kike" basi nishakuwa tayari. Nafanya, tena kwa ridhaa yangu kwa sababu majukumu ya ndani ni kusaidiana.
Mmetoka wote job, mke apike, aoshe vyombo, afue, apige deki...wewe umekaa sebuleni unaangalia tv. Hii dhana ya kuwa mwanaume ni kumuachia mke kazi za ndani sioni mantiki yake hata kidogo.!
 
Honey Faith everlenk Ikiwa mnaamini hizo ni promo muamini pia wanaume wote wanaosha nguo za ke wao. Hap akina Eli79, Kikulacho chako na wengineo ni wazuri kitheory na kimkakati! (mvaage miwani sku moja moja)

eve kwenye uchumvi uchumvi usikufananishe na kufua. Simple qn: Nisipozama mimi atazama nani?
 
Last edited by a moderator:
Mimi nafua nguo za mke wangu na hata Wanangu sijasikia kuitwa Marioo wala poyoyo
 
Jamani kwani kuna tatizo gani ..wakati mwingine natamani hata kuzivaaaa 😂😂😂😂 ngoja nsubirie Matusi hapa
 
Honey Faith everlenk Ikiwa mnaamini hizo ni promo muamini pia wanaume wote wanaosha nguo za ke wao. Hap akina Eli79, Kikulacho chako na wengineo ni wazuri kitheory na kimkakati! (mvaage miwani sku moja moja)

eve kwenye uchumvi uchumvi usikufananishe na kufua. Simple qn: Nisipozama mimi atazama nani?

Mashaxizo best wanasema ukimpenda utamlinda,kulinda huko ni kwa kila hali,kwangu mimi sitapenda tendo hilo la kufua lifanyike kwa lazima ila lifanyike kwa moyo wa upendo tena kutoka uvunguni mwa moyo kabisa,jamani upendo wa kweli hutufundisha kuwa waungwana,nakwambia ukweli ukiona mwenziyo yuko bize sana nawe umekaa tu jua there is something wrong upendo wa ukweli hautakubali ukae tu unamwangalia kuna kitu hata kama siyo kufua utatamani kufanya ili mwenziyo amalize kwa wakati ili muwe na muda wa kupumzika wote kwa pamoja.

Najua kitu kingine ni malezi,tumetoka familia mbalimbali wengine kwao toka akiwa kwa wazazi wake yule mwanaume alizoea kufanya kazi kama hizo,hivyo kwake haoni shida na huendelea kufanya kazi hizo hata akioa,na kuna makabila mengine mwanaume akifanya kazi hizo ni matusi makubwa,vivyohivyo kwa wanawake kuna makabila kama kulisha na kukamua ng'ombe ni kazi zao wakati kwa wengine ni kazi za wanaume,ila yote juu ya yote upendo wa kweli hutufundisha kuwa waungwana.

Onyo kwa wanawake wenzangu najua baadhi wengine mna bahati na mwanaume anafanya kazi hizo kwa upendo kabisa basi mlivyo wajinga kutwa kwenda kujitapa kwa mashoga mume wangu nimemuweka mkononi ananifulia,ananipikia n.k au mwingine hajitapi kwa mashoga ila siku mwanaume asipofanya ananuna kama nini au ndo kiburi kinaanza viamri vya hapa na pale haviishi,kumbukeni mwanamke mpumbavu ................. ukipendwa pendeka.....ukibebwa bebeka.........
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri kuna kitu kimoja kinawekwa kando. Mwanamke ni kiumbe anahitaji matunzo na uangalizi wa karibu hususani kutoka kwa mumewe.
Ndani ya ndoa nzuri hakuna mfumo dume wala mfumo jike. Uchawi mkubwa ndani ya mahusiano/mapenzi ni kuhurumiana.

Hawa dada zetu mnao waona wanapenda sana mtu anaowajali na kuwasikiliza.Kumfulia mwanamke nguo si kosa wala si ajabu wengi tu TUNAFUA.
Ila sasa katika kumfanyia ziada mkeo unatakiwa ujiridhishe na shukrani ya mkeo ilivyo. Maaana mwingine ukimcare ndo anakuona ZOBA huyo hupaswi kumcare kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.

KUMFULIA/KUMPIKIA MKEO HAKUPUNGUZI UANAMME
 
Yani hayo ndiyo mahaba yenyewe sasa,yani mie nikimpata na wakunipikia ntampendaje.embu rudi tena ukamuangalie sasa ivi,maana unaweza mkuta njemba anakuna nazi tena huku anatabasamu.hahahahahahaaa!hayo ndiyo mahaba ninyonge.
 
everlenk

Safi sana na hongera kwa kunyambulisha na kuangalia pande zote mbili.Mapenzi ni kusaidiana, i do agree. Lipi la kusaidiana hapo kuna utata. Ni mbaya sana kwa me kumfulia ke wake bila sababu za msingi, kati ya hasara za kufanya hivyo, nyengine umeshazielezea hapo juu.

On other hand unaweza kumfulia mtu kwa kile kimuhemuhe cha mapenzi (kwa kawaida kinakuja mda mfupi na kutoweka) pia ukiacha tu kumfulia unamskia mwenzio anakwambia umebadilika! We are human, we are flexible, ni ke wangapi wanatambua hilo?

Mapenzi, mapenzi, mapenzi, mbona nahisi ni part ndogo tu kwa life ya mtu, ukitaka kuyakuchukulia kama zile filamu yatakushinda, mimi napenda tena napenda sana, lakini bado kumfulia ke huko mbali sana, kwangu excuse ni moja tu AUMWE.

Ingawa bado sijaoa but najikuta nikikataa baadhi ya mambo ya hao nanii wangu, eg: m1 alipenda nimbebee kikoba chake wakati tunatembea, mwengine anapenda kupigiwa simu, usipopiga siku moja tu gubu lake usiombe, nk. nk. may be mapenzi siyajui. But kwangu ni lazima kuwe na mipaka kwa baadhi ya mambo, kumfulia wife bila dharura haijakaa vyema hiyo.

Thanks.
 
Last edited by a moderator:
Mashaxizo

Hahahaha!Wewe utakuwa ni mura nini?(joking) sasahivi ongea tu baba yangu ukipenda na ukaingia kwenye real life utajikuta tu kuna visheria vinavunjika vyenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Tafua kama atakua anaumwa ilakama haumwi siwezi labda awe menilisha lukomolo ili niwe zuzu
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom