Je, ni nani asiye na kijicho!

sana tena nitakuombea ufanikiwe zaidi
BADILI TABIA mimi ni mmoja wa wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa na mkuu wa kaya hivi karibuni nikiwazkilisha wilaya mpya ya Kideleko ................Nipongeze basi..................LOL
 
Last edited by a moderator:
maadam mimi ni binadam kukikosa nikiri tu kwamba ni ngumu ila najizuiaje kisiwe kibaya ndo jambo la muhimu
 
kijicho? lol
ndo kikoje?
what if sitaki kusaidia mtu kwa sababu tu sioni ulazima
hiko ni kijicho?

na wale wanaosaidia watu kwa kutegemea 'malipo'?
hawana kijicho?

na wanaosaidia watu huku mioyoni wana wivu?
 
Ukitaka kujua kuwa wewe ni mwenye kijicho dhidi ya mafanikio au jitihada za wenzio, jiulize maswali machache yafuatayo:

Je unaposikia jirani kanunua gari, kajenga nyumba, kafungua biashara kubwa au mwanae kapata nafasi ya kusoma nje ya nchi na mengine mengi kama hayo maadamu yawe mafanikio, unajisikiaje moyoni?

Au jirani yako anapokuomba ushauri wa kuanzisha biashara, kununua shamba, gari au nyumba, unampa ushauri kwa moyo mweupe au unatoa ushauri usiofaa?

Kwa vyovyote vile, majibu ya maswali hayo hapo juu yanatosha kukujulisha iwapo una kijicho dhidi ya mafanikio ya mwenzio au la.

Hebu tusiwe wanafiki, tujifanyie tathmini ili tujijue tuko upande gani……………

Nani athubutu?
Ha ha haaaaa


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ukiwa nakijicho karne hii si utajikuta unakufa mapema.
Mara jirani wa kushoto kazipiga mahali kavuta Hammer,wa kulia yupo na vogue,
Dogo uliemleta town mara anamiliki bonge la biashara.

Sasa ukiwa na kijicho hapo itakuwaje?
 
Sina wivu na sijuwagi kuumia kwaajili ya mafanikio ya mwengine, Labda kama inafanana na kupenda cha mwingine,

Mtu wa aina ,jinsia, Hali Yoyote akinitaka ushauri nitampa to the Best of my know how ya jambo husika
 
Wivu ni muhimu ili na we ufanikiwe! Hivi jamani hamjawai kuona mtu hana wivu matokeo yake kila siku yuko hapo hapo! Wivu wa maendeleo sio mbaya! Cha msingi na we kazana! Upate! Tatizo linakuja pale mtu ye kashakata tamaa ya kutafuta basi anakaa anatafuta njia za kuwazuia wenzake wasiendelee ili walingane na yeye! We kama huna wivu kaa hivyo hivyo usiharibie wenzako! Ha ha haaaaa!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mtambuzi, uzi wako siyo watu wanakwepa ila mada uliyoiweka imekuwa na changamoto kwenye kuichangia. Kwa upande wangu mimi suala la kuwa na kijicho au kutokuwa na kijicho inategemea na ukaribu wa huyo mtu ambaye anamuonea kijicho/asiyemuonea kijicho mwenzie.

Kwa mfano si rahisi, mtu akigombana na mwenzake, kwa vyovyote vile, hatapenda kuona mwenzake (huyo mgomvi wake) anafanikiwa kwa yale atakayokuwa anayafanya. Hii ni nature ya binadamu na ndiyo maana kuna msemo unasema adui yako muombee njaa, na huwa hawasemi muombee mafanikio!!!

Lakini ktk hali ya kawaida, huwezi kuwa na kijicho kwa yule mtu ambaye una mahusiano naye mazuri. Kwa mfano rafiki zako, ndugu zako, jamaa zako wa karibu nk nk huwezi kuwaonea kijicho wanapofanikiwa na kama ikitokeo hivyo, basi wewe utakuwa na matatizo au una ile kitu inayoitwa ROHO MBAYA! :confused2:

Yaani umesema sahihi kabisa..........
Lakini kuna namna nzuri ya kuondokana na hiyo dhana ya "adui yako muombee njaa"
Ninaandaa makala juu namna ya kuondokana na kijicho chenye kisirani............................!

Naisubiria hiyo Makala kwa hamu sana Mtambuzi, najuwa umebobea kwenye taaluma ya kuandika makala zenye kuijenga na kuishauri jamii. Big up sana mkuu!
 
Mwenye+Jicho+Hafanikiwi+KHANGA.jpg
:sick:
 
Back
Top Bottom