msafiri.razaro
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 1,244
- 744
Kama ulikuwepo vile.Je,unatambua kuwa unatumia utashi ulionao kuuliza haya maswali uliyopost?Inawezekana kupitia haya Maswali una asi au vilevile unafanya vizuri.Lakini yote kwa yote unatumia utashi wako kufikiri na kuchambua Mambo mbalbali.Je,kosa La MUNGU ni kukupa wewe utashi au kosa ni wewe kwenda kinyume na maagizo yake ili baadae useme isingekuwa utashi aliokupa usingeasi?
Utashi una faida na hasara zake.Na MUNGU Hilo alilijua Sana tu.Hasara Ni kwamba,ukiutmia vibaya unakuwa huna thamani mbele ya MUNGU,na Hilo kosa si la MUNGU.Utashi Ni zawadi kubwa kwa wale wanaoutumia kwa kufuata amri za MUNGU.
MUNGU aliona kuwapa Malaika utashi Ni vyema machoni pake kwa maana unawawezesha kutekeleza maagizo yake kwa Uhuru bila ya kuwalazimisha.
Lucifer alitumia huo utashi kubishana na Michael kwenye swala la kumsujudia Adam.Michael alitumia jitihada zake zote kumshauri mwenzake asitumie utashi wake vibaya maana utamgharimu lakini hakutaka.Je kosa hapo Ni kupewa utashi au ni kutumia utashi vibaya?
Utashi ndio unatuwezesha kuamua kufuata au kutokufuata sheria za Mungu.Usipofuata kosa Ni lako Ni si la MUNGU.
Sent using Jamii Forums mobile app
