Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Hilo swali gumu sana na huwezi kulijibu mpaka utakufa.
Mkuu Saguda47 ndio maana watu wana conclude kwamba Mungu hayupo kwa dhana hiyohiyo.

Kwamba kama Mungu ndiye aliumba ulimwengu, bila shaka yeye Mungu ni complex kuliko ulimwengu aliouumba.

Sasa kama ulimwengu ambao kwa muktadha huo, ni less complex kulinganisha na aliyeuumba, sasa kwanini iwe lazima uwe umeumbwa!?

Basi kama kitu simple kama ulimwengu (kwa muktadha huo) ni lazima kiumbwe yaani hakiwezi kutokea chenyewe, vipi kwa kitu complex!? Basi na chenyewe lazima kimeubwa na object ambayo ni even complex than it.

Basi kumbe, kama Mungu(ambaye ni so complex) hakuumbwa basi kunauwezekano hata universe(ambayo ni simple) haikuumbwa.
 
nimekuelewa vizuri mkuu, Mungu complex power ambayo mwisho na mwanzo wake ni mgumu sana kujulikana.
Mkuu Saguda47 ndio maana watu wana conclude kwamba Mungu hayupo kwa dhana hiyohiyo.

Kwamba kama Mungu ndiye aliumba ulimwengu, bila shaka yeye Mungu ni complex kuliko ulimwengu aliouumba.

Sasa kama ulimwengu ambao kwa muktadha huo, ni less complex kulinganisha na aliyeuumba, sasa kwanini iwe lazima uwe umeumbwa!?

Basi kama kitu simple kama ulimwengu (kwa muktadha huo) ni lazima kiumbwe yaani hakiwezi kutokea chenyewe, vipi kwa kitu complex!? Basi na chenyewe lazima kimeubwa na object ambayo ni even complex than it.

Basi kumbe, kama Mungu(ambaye ni so complex) hakuumbwa basi kunauwezekano hata universe(ambayo ni simple) haikuumbwa.
 
Ukiamini Mungu yupo ! Jibu ni rahisi , ni yeye aliyeweka mwanga na giza hivyo dhambi ipo ndani ya giza .
 
Ukiamini Mungu yupo ! Jibu ni rahisi , ni yeye aliyeweka mwanga na giza hivyo dhambi ipo ndani ya giza .
Unajua mkuu, kadiri ya maoni ya wengi gasa wanazuoni ni kuwa, Yawezekana Mungu kweli yupo, lakini si wa sifa hizi zinazoubiriwa na Abrahamic Religions (ukristu, uislamu na uyahudi), kwa sababu kuna mengi sana yanayo contradict kumuhusu.

Lakini hata hivyo imani juu ya uwepo wa mungu linabaki ni suala binafsi ya maamuzi ya mtu husika.
 
Kama unaamini hakuna Mungu huna la kujibu ila kama unaamini yupo basi aliumba kila kitu na dhambi ipo ndani ya " kila kitu " hivyo Mungu aliumba dhambi" utauliza kwa nini! Ukifa utaonana nae na utamuuliza kwa nini uturushie mrejesho huku duniani
Uyo mungu alitokea wapi?
 
Na hapo kwenye hoja hii uliyotoa unaweza kujiuliza swali hili:

Kama Mungu aliumba universe, Je yeye aliumbwa na nani!?
Kwani nani amesema Mungu kaumbwa hadi tumtafute aliyemuumba?
 
Unajua mkuu, kadiri ya maoni ya wengi gasa wanazuoni ni kuwa, Yawezekana Mungu kweli yupo, lakini si wa sifa hizi zinazoubiriwa na Abrahamic Religions (ukristu, uislamu na uyahudi), kwa sababu kuna mengi sana yanayo contradict kumuhusu.

Lakini hata hivyo imani juu ya uwepo wa mungu linabaki ni suala binafsi ya maamuzi ya mtu husika.
Yapi yenye kucontradict?
 
Mkuu, kwa hiyo unakubali kwamba inawezekana kitu kisiwe kimeumbwa lakini kikawepo? Yaani kikawepo bila kuumbwa!?
Kitu kama kimeumbwa basi lazima kuna muuumbaji ambaye ndiye aliyeumba hicho kitu,sasa wanaosema kuwa huu ulimwengu umeumbwa husema kuwa aliyeumba ni Mungu kwamba ndio muumbaji.

Sasa wewe ukauliza na Mungu kaumbwa na nani? Ndio nikakuuliza kwani nani aliyesema Mungu kaumbwa hadi tumtafute aliyemuumba?

Sasa hilo kwamba vitu vinaweza kutokea tu bila kuumbwa au lazima viumbwe ni suala jengine,kama wewe unaona kitu kinaweza kutokea tu chenyewe bila kuumbwa hivyo unapingana na wanaodai kuwa ulimwebgu umeumbwa basi sawa.
 
Kitu kama kimeumbwa basi lazima kuna muuumbaji ambaye ndiye aliyeumba hicho kitu,sasa wanaosema kuwa huu ulimwengu umeumbwa husema kuwa aliyeumba ni Mungu kwamba ndio muumbaji.

Sasa wewe ukauliza na Mungu kaumbwa na nani? Ndio nikakuuliza kwani nani aliyesema Mungu kaumbwa hadi tumtafute aliyemuumba?

Sasa hilo kwamba vitu vinaweza kutokea tu bila kuumbwa au lazima viumbwe ni suala jengine,kama wewe unaona kitu kinaweza kutokea tu chenyewe bila kuumbwa hivyo unapingana na wanaodai kuwa ulimwebgu umeumbwa basi sawa.
Kwenye hiyo para ya mwisho mkuu.

Kama mtu unaamini kuwa Mungu amekuwepo bila kuumbwa, its obvious kumbe kuna vitu vipo bila kuumbwa!?

Au wewe unajuaje hapo!? Je, Mungu yupo bila kuumbwa!?
 
Yale uliyosema kuwa ni ya Mungu, i.e.au kwa nini Mungu alimuumba shetani wakati anajua yatakayokuja, au kama mbinguni ni kutakatifu na shetani alikuwa mbinguni patakatifu; kuwa alishawishiwa na nani kuasi na maswali mengine mengi mazuri; maoni yangu:
Kuna kasoro/Shida kubwa ya kimaumbile tuliyonayo binadamu kwenye ulimwengu huu. Kasoro yenyewe ni ya kiufahamu. Yaani uwezo wetu wa ufahamu binadamu hutegemea kufundishwa. Kama fundusho fulani limekaa katika mlengo fulani, mlengo huo ndo hummuumba mtu huyo.

Kwenye maswali yako, inawezekana hoja zote/ maswali yote uliyonayo kutoka kwenye mistari ya kwenye maandiko yakawa hayana ukweli wowote! Kwamba tunayoyafahamu au tunayoyaamini hutokana na tunavyofundishwa. Bahati mafundisho hayo yamewekwa kuwa na uhalali, yamepewa hadhi ya ukweli wa kiMungu. Lkn ukweli huo mtakatifu, ukweli wake mtakatifu nao ni wa kufundishwa.

Kwa hiyo kikubwa cha kuwaza ni kuwa haya tunayoyaamini inastahiki kuwa na msing/ukweli wa kuaminiwa kiasi hicho!?

Mafundisho ya uwepo wa Mungu na mbingu, shetani na jehanamu hufundishwa sana na imani zenye asili ya mashariki ya Kati yaani Ukristo na Uislamu. Kwenye maswali yako, ungeongeza kwa nini dini hizi tu ndo hutambua na huamini uwepo wa Mungu na shetani. Bahati mbaya(nzuri kwa wafuasi) dini hizi ndo zimeenezwa sana duniani, kwa hiyo watu wengi tunafanya hivyo, misingi ya ukweli wa kiimani tumefundishwa hivyo.

Kwa udhaifu ule wa kiufahamu wa binadamu, wa kuwa vile au kuamini kulingana na mafundisho; hatukwepi mtego/changamoto yake. Lkn ukitoka nje ya muktadha/mazingira yetu, utaona kuna jamii ambazo haziamini katika uwepo wa nguvu mbili yaani Mungu na shetani. Mfano ni jamii ya kichina na India. Kutoa judgement kwa jamii hizo kwa kuzingatia uwepo wa Mungu na shetani, atakushangaa kwa sababu kwenye ufahamu wake, hakuna taarifa hiyo.

Kwa hiyo, maswali yako ni ya kiufahamu kutokana na mafundisho yetu. Jamii nyingi za kiafrika, America ya kusini, hata America ya kaskazini n.k., imani hii tuliipata kwa mafundisho, tena mafundisho ya nguvu na kikatili ya kikoloni.

Jamii ambazo hawakupambana na zahma hiyo ya mafundisho, hawana imani hiyo pia. Jiulize kwa nini! Ongezea pia, kwa nini waliokaa na wakoloni wa kilutheri ni walutheri, wa kianglicana nao ni waangilikana, wakatoliki nao hivyo hivyo. Na waliokaliwa na Uislamu nao ni waislamu, vile vile na tofauti za kimaarifa kutokana na maarifa anayofundishwa.

Kwa hiyo maswali yako yanaweza kuonekana na mantiki kulingana katika muktadha wa imani yako. Ukweli wake wa kiimani utatokana/ unategemea na mafundisho ya mtu .

Katika mafundisho mengine yakawa hayapo. Kwa kumalizia, maswali yako hayawezi kupata majibu ya kibinadamu wala kwa binadamu. Mwenye uwezo wa kuyajibu sawa sawa bila kuleta mkanganyiko ni Mungu mwenyewe ambaye siyo yule tunayemtafsiri kulingana na mafundisho/imani zetu(think) .
 
Kwenye hiyo para ya mwisho mkuu.

Kama mtu unaamini kuwa Mungu amekuwepo bila kuumbwa, its obvious kumbe kuna vitu vipo bila kuumbwa!?

Au wewe unajuaje hapo!? Je, Mungu yupo bila kuumbwa!?
Ndiyo maana nilisema kwamba kitu chochote ambacho tukisema kimeumbwa basi lazima kuwe kuna muumbaji wa hicho kitu,na tulichokuwa tukijadili ni swali lako ulilouliza aliyemuumba Mungu? nikakwambia kuwa hakuna anayesema Mungu kaumbwa hivyo hatuwezi kumtafuta muumbaji wa kitu ambacho hakijaumbwa.

Na kuhusu Mungu ni kwamba yeye ndiye pekee muumbaji hakuna mwengine,kwa hivyo vyote vile ambavyo tutasema vimeumbwa basi muumbaji ni Mungu tu na si vinginevyo.

Kwahiyo si tu kwamba Mungu hajaumbwa bali yeye ndio pekee muumbaji.
 
Ndiyo maana nilisema kwamba kitu chochote ambacho tukisema kimeumbwa basi lazima kuwe kuna muumbaji wa hicho kitu,na tulichokuwa tukijadili ni swali lako ulilouliza aliyemuumba Mungu? nikakwambia kuwa hakuna anayesema Mungu kaumbwa hivyo hatuwezi kumtafuta muumbaji wa kitu ambacho hakijaumbwa.

Na kuhusu Mungu ni kwamba yeye ndiye pekee muumbaji hakuna mwengine,kwa hivyo vyote vile ambavyo tutasema vimeumbwa basi muumbaji ni Mungu tu na si vinginevyo.

Kwahiyo si tu kwamba Mungu hajaumbwa bali yeye ndio pekee muumbaji.
Mkuu, nakubaliana na wewe kwamba kwa unavyoamini ni kuwa Mungu hajaumbwa, na wala hata mimi, kwa sasa sitaki kujua kama Mungu ameumbwa au la!

Ninachotaka kujua kutoka kwako ni kupitia jibu utakalolitoa la swali hili:

Je, unakubali kwamba kuna vitu vinaweza tokea vyenyewe bila kuumbwa!?
 
Mkuu, nakubaliana na wewe kwamba kwa unavyoamini ni kuwa Mungu hajaumbwa, na wala hata mimi, kwa sasa sitaki kujua kama Mungu ameumbwa au la!

Ninachotaka kujua kutoka kwako ni kupitia jibu utakalolitoa la swali hili:

Je, unakubali kwamba kuna vitu vinaweza tokea vyenyewe bila kuumbwa!?
Kama vitu gani mkuu?
 
Back
Top Bottom