Capt Tamar
JF-Expert Member
- Dec 15, 2011
- 11,655
- 14,492
Habari za shughuli ndugu zangu,
Naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa mwanzoni mwa mwaka huu, baada ya mazishi kuna kikao cha ndugu kilikaa kujadili mustakabali wa familia kama ilivyo desturi sasa kwenye kikao kile, wengi walikuwa ni ndugu wa mke wangu.
Wengi wao hata nilikuwa siwafahamu, kikao kikamteua shemeji yangu ambaye ndiye kaka mkubwa wa mke wangu awe msimamizi wa mirathi, mke wangu alikuwa na mali alizochuma yeye mwenyewe kabla hatujaoana, na mimi nilikuwa na zangu binafsi.
Na kuna kiwanja alikinunua kwa kaka yake huyohuyo wakati tukiwa tunaishi pamoja, higher kiwanja tukajenga nyumba za kupangisha, na tukapata mpangaji mmoja aliyepanga vyumba vyote 8, wakati huo mimi nilikuwa nipo nje ya mkoa kikazi.
Kwa hiyo, hata wakati ujenzi unaendelea, mimi sikuwepo, mtu aliyekuwa akisimamia ujenzi ni huyo kaka wa mke wangu, kwakuwa hakuwa na shughuli yoyote kipindi hicho hivyo nikawa namlipa asaidie kusimamia ujenzi na hata shughuli nyinginezo za ujenzi kwenye nyumba nyingine niliyokuwa naijenga mtaa mwingine ambayo ndiyo tunayoishi hata sasa, sasa tabu imekuja baada ya yeye kukabidhiwa jukumu la kusimamia mirathi.
Kwanza alikosana na yule mpangaji hali iliyomlazimu mpangaji yule kuhama mimi nikiwa sipo, kisha akawapangishia wapangaji wengine bila kunitaarifu.
Baadaye kodi ikaanza kusumbua, mara anitumie mara asitume, nikaamua kumfuata ili anieleze tatizo ni nini, baada ya kufokeana sana akaniambia yeye ndiye msimamizi wa mali zote kwa hiyo sipaswi kumpangia.
Ni takriban miezi mitano sasa hajaleta kodi ya nyumba, wale wapangaji sijui aliwaseti vipi, maana kila nikijaribu kuwafata huwa wananikwepa, nadhani hajafungua mirathi mahakamani kwani kuna vielelezo ambavyo angepaswa kuvipata kutoka kwangu ila hakuwahi kuniomba nimpatie, sasa nafikiri nimpeleke mahakamani, ila huko sina nijualo especialy kwa kesi ya aina hii.
Naamini hapa kuna wajuzi wa mambo kama haya. Hivyo naomba mchango wenu wa mawazo ili niweze kuilinda haki ya familia yangu nikiwa na ujasiri.
Natanguliza shukrani zangu kwenu.
Naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa mwanzoni mwa mwaka huu, baada ya mazishi kuna kikao cha ndugu kilikaa kujadili mustakabali wa familia kama ilivyo desturi sasa kwenye kikao kile, wengi walikuwa ni ndugu wa mke wangu.
Wengi wao hata nilikuwa siwafahamu, kikao kikamteua shemeji yangu ambaye ndiye kaka mkubwa wa mke wangu awe msimamizi wa mirathi, mke wangu alikuwa na mali alizochuma yeye mwenyewe kabla hatujaoana, na mimi nilikuwa na zangu binafsi.
Na kuna kiwanja alikinunua kwa kaka yake huyohuyo wakati tukiwa tunaishi pamoja, higher kiwanja tukajenga nyumba za kupangisha, na tukapata mpangaji mmoja aliyepanga vyumba vyote 8, wakati huo mimi nilikuwa nipo nje ya mkoa kikazi.
Kwa hiyo, hata wakati ujenzi unaendelea, mimi sikuwepo, mtu aliyekuwa akisimamia ujenzi ni huyo kaka wa mke wangu, kwakuwa hakuwa na shughuli yoyote kipindi hicho hivyo nikawa namlipa asaidie kusimamia ujenzi na hata shughuli nyinginezo za ujenzi kwenye nyumba nyingine niliyokuwa naijenga mtaa mwingine ambayo ndiyo tunayoishi hata sasa, sasa tabu imekuja baada ya yeye kukabidhiwa jukumu la kusimamia mirathi.
Kwanza alikosana na yule mpangaji hali iliyomlazimu mpangaji yule kuhama mimi nikiwa sipo, kisha akawapangishia wapangaji wengine bila kunitaarifu.
Baadaye kodi ikaanza kusumbua, mara anitumie mara asitume, nikaamua kumfuata ili anieleze tatizo ni nini, baada ya kufokeana sana akaniambia yeye ndiye msimamizi wa mali zote kwa hiyo sipaswi kumpangia.
Ni takriban miezi mitano sasa hajaleta kodi ya nyumba, wale wapangaji sijui aliwaseti vipi, maana kila nikijaribu kuwafata huwa wananikwepa, nadhani hajafungua mirathi mahakamani kwani kuna vielelezo ambavyo angepaswa kuvipata kutoka kwangu ila hakuwahi kuniomba nimpatie, sasa nafikiri nimpeleke mahakamani, ila huko sina nijualo especialy kwa kesi ya aina hii.
Naamini hapa kuna wajuzi wa mambo kama haya. Hivyo naomba mchango wenu wa mawazo ili niweze kuilinda haki ya familia yangu nikiwa na ujasiri.
Natanguliza shukrani zangu kwenu.