Je, mifumo ya Vyama vya Upinzani ina uwezo wa kutosha?

Gift mzalendo

JF-Expert Member
Dec 13, 2019
1,006
1,171
Heshima kwenu wanajukwaa,

Kwanza nitangulize shukrani kwa vyama vya upinzani ambavyo vimeendelea kuonyesha ushindani kwa chama tawala.

Ndugu wanajukwaa moja ya Jambo ambalo naamini, ni kwamba watanzania au kawaida binadamu wanapenda sana mabadiliko kwa Kila eneo. Katika hulka hii ya binadamu hubadilisha kwa lengo la kupata kitu Bora zaidi ya kile alichonacho na huku ndiko tunapata neno maendeleo.

Kabla ya kubadili huhitaji yafutayo
1.Kuamini kuwa atapata kitu Bora zaidi ya kile alichonacho
2.Kile kitu kitampa Unafuu wa maisha yake kwa kiwango gani zaidi
3.Uimara wa kitu kipya
4.Kudumu kwa muda gani

Moja ya maswali ambayo naamini watu wengi wanajiuliza
Je, tukiwapa upinzani nchi wataweza kuhandle nchi na mifumo yake yote?
Je, mifumo ya vyama upinzani ina uwezo wa kusimamia mifumo mingine ya nchi?
Je, ina uimara kiasi gani ya kusimamia nchi na mifumo yake bila mifumo yake yenyewe kubomoka (collapse)?
Je, imeandaa watu wake kwa kiasi gani ambao watakuwa mbadala was viongozi waliopo na kuleta mabadiliko?

Nikiri tu Mimi Ni muumini wa mifumo imara na muumini wa vyama vingi vinavyoshindana kwa sera na hoja. Ni miongoni mwa watu wanaotamani kuona tunakuwa na vyama mbadala ambavyo vinabadilishana madaraka Kila inapobidi, ili kuleta ushindani wa kimaendeleo. Leo kinaongoza chama A kikiboronga kinaongoza B nk.

Maoni yangu
Moja vyama vya viimarishe mifumo yao Kwanza, nafikiri tunaona vyama vikishindwa kubeba hata baadhi ya wanachama wao wanaohamia wenye umaaeufu.

Pili viimarishe demokrasia yao ya ndani.

Tatu viweke mpango wa kuimarisha uchumi wake, kwa kuwa na vyanzo halali vya mapato, Hili nasisitiza hi Ni moja ya sababu kuu ya kufa kwa vyama vya upinzani na hata kuharibu misimamo ya viongozi wake na kuonekana kituko.

Nne vyama viwe na mfumo wake wa kuandaa viongozi na watendaji wake.

Tano wekeni kando ubinafsi mtuundie umoja wa vyama madhubuti au chama kimoja Cha upinzani

Imarisheni na kupanua mifumo yenu tuamanisheni wananchi mtakuwa mbadala wa chama kilichopo.

Wananchi wawape ridhaa kuongoza
Hayo ni maoni yangu machache
 
Vyama vya upinzani havina shida na hayo yote, havina shida hata ya kushika Dola wala Jeshi wala Mahakama wala Hazina wala BOT. Hivyo vyote vibakie kumilikiwa na CCM.

Vyama vya upinzani vina shida moja tu ambayo ni wananchi wapatiwe "KATIBA MPYA". Hilo tu, halafu tukutane 2025 kwenye sanduku la kura.

Nasema uongo ndugu zangu?
 
Vyama vya upinzani havina shida na hayo yote, havina shida hata ya kushika Dola wala Jeshi wala Mahakama wala Hazina wala BOT.

Vyama vya upinzani vina shida moja tu ambayo ni wananchi wapatiwe "KATIBA MPYA". Hilo tu, halafu tukutane 2025 kwenye sanduku la kura.
Ikiwa hivyo vinapoteza uhalali wake wa kuwa vyama vya siasa, kila taasisi ina kusudi lake ambalo inalisimamia, likipoteza Hilo kusudi inapoteza uhalali wake, uungwaji mkono unapungua hatimae hufa, Moja ya Kusudi kuu la chama Cha kisiasa Ni kushika dola ili kiweze kutekeleza ahadi na sera zake Bora kwa wananchi.

Kikihama hapo lazima kijikute kwenye wakati mgumu.

Katiba inaweza kuwa lengo mojawapo lakini sio kusudi.
 
Ikiwa hivyo vinapoteza uhalali wake wa kuwa vyama vya siasa, kila taasisi ina kusudi lake ambalo inalisimamia, likipoteza Hilo kusudi inapoteza uhalali wake, uungwaji mkono unapungua hatimae hufa, Moja ya Kusudi kuu la chama Cha kisiasa Ni kushika dola ili kiweze kutekeleza ahadi na sera zake Bora kwa wananchi.

Kikihama hapo lazima kijikute kwenye wakati mgumu.

Katiba inaweza kuwa lengo mojawapo lakini sio kusudi.
Wanataka kwanza kumpunguza nguvu chama tawala kwa kutumia hiyo katiba mpya,hilo likiwezekana wanaamini itawezekana kwao kushinda uchaguzi na kumtoa ccm.
 
Ikiwa hivyo vinapoteza uhalali wake wa kuwa vyama vya siasa, kila taasisi ina kusudi lake ambalo inalisimamia, likipoteza Hilo kusudi inapoteza uhalali wake, uungwaji mkono unapungua hatimae hufa, Moja ya Kusudi kuu la chama Cha kisiasa Ni kushika dola ili kiweze kutekeleza ahadi na sera zake Bora kwa wananchi.

Kikihama hapo lazima kijikute kwenye wakati mgumu.

Katiba inaweza kuwa lengo mojawapo lakini sio kusudi.
Bila tume huru ya uchaguzi ni kazi bure
 
Tatu viweke mpango wa kuimarisha uchumi wake, kwa kuwa na vyanzo halali vya mapato, Hili nasisitiza hi Ni moja ya sababu kuu ya kufa kwa vyama vya upinzani na hata kuharibu misimamo ya viongozi wake na kuonekana kituko
Hili la muhimu sana niliona chama cha ODM kina zaidi ya Billion 200 na hata hakipo serikalini!! kwa staili hiyo ni ngumu kushawishika kukimbia chama.

Changamoto hapa Tz hata vyanzo vya pesa za upinzani vinakua frustrated..... Waliokua wanawachangia walifilisiwa, biashara za pembeni kufund chama zilipigwa kodi nzito.... Nakumbuka hta pesa kutoka vyama marafiki kuja kwa upinzani zilizuiwa kwa sheria za utakatishaji pesa!! So inakua ngumu tofauti na kenya ambapo kuna mabilionea wanao changia pesa upinzani miaka yote na hawasumbuliwi.

Tano wekeni kando ubinafsi mtuundie umoja wa vyama madhubuti au chama kimoja Cha upinzani
Labda alliance ila chama kimoja ni ngumu mfano CHADEMA ni mrengo wa kati-kulia ilihali ACT ni mrengo wa kushoto. Hapo bado mmoja ni Socialist mwingine ni mnazi wa Market economy sasa hapo mnaungana vipi??
 
Moja ya Kusudi kuu la chama Cha kisiasa Ni kushika dola ili kiweze kutekeleza ahadi na sera zake Bora kwa wananchi.

Kikihama hapo lazima kijikute kwenye wakati mgumu.
Hapa unakwama kuna vyama duniani mfano kimoja kule Uingereza chenyewe kili deal na Brexit tu kma agenda kuu na kikapata wabunge wakutosha wala hawakuwa wana target kupata serikali but kujaza wabunge kuharakisha Brexit.

Kuna chama cha siasa kinaitwa AFP hapa bongo ni cha wakulima..... Wao Agenda kuu ni kuforward hoja za wakulima ziweze kufika kwenye vyombo vya maamuzi. Huwezi shida urais huna hata diwani!! So malengo yanakuwa ni kuoata sauti kwenye vyombo vya uwakilishi ukisha jiazititi ndio unawaza dola.... So huwezi sema chama lazma kifocus kushika dola!!

Pia huko sauzi kuna chama kikuu cha upinzani kinaitwa DA wao agenda yao ni kukamata miji mikubwa na kuongeza kura za watu weusi.... Wala hawana mpango wa kukamata dola kwa sasa!! Ina fact walikamata majimbo zaidi ya 100 wakaona ni ushindi wa kimbunga! So kila chama kina malengo yake ya kuanzishwa.
 
Heshima kwenu wanajukwaa,

Kwanza nitangulize shukrani kwa vyama vya upinzani ambavyo vimeendelea kuonyesha ushindani kwa chama tawala.

Ndugu wanajukwaa moja ya Jambo ambalo naamini, ni kwamba watanzania au kawaida binadamu wanapenda sana mabadiliko kwa Kila eneo. Katika hulka hii ya binadamu hubadilisha kwa lengo la kupata kitu Bora zaidi ya kile alichonacho na huku ndiko tunapata neno maendeleo.

Kabla ya kubadili huhitaji yafutayo
1.Kuamini kuwa atapata kitu Bora zaidi ya kile alichonacho
2.Kile kitu kitampa Unafuu wa maisha yake kwa kiwango gani zaidi
3.Uimara wa kitu kipya
4.Kudumu kwa muda gani

Moja ya maswali ambayo naamini watu wengi wanajiuliza
Je, tukiwapa upinzani nchi wataweza kuhandle nchi na mifumo yake yote?
Je, mifumo ya vyama upinzani ina uwezo wa kusimamia mifumo mingine ya nchi?
Je, ina uimara kiasi gani ya kusimamia nchi na mifumo yake bila mifumo yake yenyewe kubomoka (collapse)?
Je, imeandaa watu wake kwa kiasi gani ambao watakuwa mbadala was viongozi waliopo na kuleta mabadiliko?

Nikiri tu Mimi Ni muumini wa mifumo imara na muumini wa vyama vingi vinavyoshindana kwa sera na hoja. Ni miongoni mwa watu wanaotamani kuona tunakuwa na vyama mbadala ambavyo vinabadilishana madaraka Kila inapobidi, ili kuleta ushindani wa kimaendeleo. Leo kinaongoza chama A kikiboronga kinaongoza B nk.

Maoni yangu
Moja vyama vya viimarishe mifumo yao Kwanza, nafikiri tunaona vyama vikishindwa kubeba hata baadhi ya wanachama wao wanaohamia wenye umaaeufu.

Pili viimarishe demokrasia yao ya ndani.

Tatu viweke mpango wa kuimarisha uchumi wake, kwa kuwa na vyanzo halali vya mapato, Hili nasisitiza hi Ni moja ya sababu kuu ya kufa kwa vyama vya upinzani na hata kuharibu misimamo ya viongozi wake na kuonekana kituko.

Nne vyama viwe na mfumo wake wa kuandaa viongozi na watendaji wake.

Tano wekeni kando ubinafsi mtuundie umoja wa vyama madhubuti au chama kimoja Cha upinzani

Imarisheni na kupanua mifumo yenu tuamanisheni wananchi mtakuwa mbadala wa chama kilichopo.

Wananchi wawape ridhaa kuongoza
Hayo ni maoni yangu machache

Una mashaka na uwezo wa vyama vya upinzani kwasababu unatumia hisia na vigezo vya kiccm. Kwa taarifa yako nchi hii inaweza kuongozwa na Chama chochote cha siasa. Kama ccm imeweza tena huku ikiwa haifakii nyingi ya ahadi zake, ni chama gani kitashindwa kazi hiyo?
 
Wanataka kwanza kumpunguza nguvu chama tawala kwa kutumia hiyo katiba mpya,hilo likiwezekana wanaamini itawezekana kwao kushinda uchaguzi na kumtoa ccm.
Hilo Ni moja ya lengo majawapo
Zuri
Lakini Bado tunajiuliza katika hali ya mifumo na utengano was vyama vya upinzani , je wanayo nguvu ya kupunguza nguvu ya chama tawala?
Kwanini wanashindwa kuunganisha nguvu ya pamoja kusukuma agenda ya katiba mpya.
 
UPUUZI MTUPU!!!
Ikiwa hivyo vinapoteza uhalali wake wa kuwa vyama vya siasa, kila taasisi ina kusudi lake ambalo inalisimamia, likipoteza Hilo kusudi inapoteza uhalali wake, uungwaji mkono unapungua hatimae hufa, Moja ya Kusudi kuu la chama Cha kisiasa Ni kushika dola ili kiweze kutekeleza ahadi na sera zake Bora kwa wananchi.

Kikihama hapo lazima kijikute kwenye wakati mgumu.

Katiba inaweza kuwa lengo mojawapo lakini sio kusudi.
 
Hapa unakwama kuna vyama duniani mfano kimoja kule Uingereza chenyewe kili deal na Brexit tu kma agenda kuu na kikapata wabunge wakutosha wala hawakuwa wana target kupata serikali but kujaza wabunge kuharakisha Brexit.

Kuna chama cha siasa kinaitwa AFP hapa bongo ni cha wakulima..... Wao Agenda kuu ni kuforward hoja za wakulima ziweze kufika kwenye vyombo vya maamuzi. Huwezi shida urais huna hata diwani!! So malengo yanakuwa ni kuoata sauti kwenye vyombo vya uwakilishi ukisha jiazititi ndio unawaza dola.... So huwezi sema chama lazma kifocus kushika dola!!

Pia huko sauzi kuna chama kikuu cha upinzani kinaitwa DA wao agenda yao ni kukamata miji mikubwa na kuongeza kura za watu weusi.... Wala hawana mpango wa kukamata dola kwa sasa!! Ina fact walikamata majimbo zaidi ya 100 wakaona ni ushindi wa kimbunga! So kila chama kina malengo yake ya kuanzishwa.
Ni kweli Kuna malengo madogo ya muda mfupi ambayo chama kinaweza kujiwekea lakini lengo kuu au kusudi lake Ni kukamata madaraka , maana hiyo ndo njia ya kuweza kutekeleza sera zake ahadi na misimamo, na ndo wanakuwa na nguvu ya kusimamia hoja zao,
Nje ya hapo vitabaki tu kuwa vyama vya matamko visivyo na meno
 
Wanaouliza kwa nini Mbowe amekamatwa sasa na si vinginevyo wanasahau kuwa Mbowe, Lema, Meya wa zamani Ubungo Boniface walikamatwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa na kabla Rais hajaapishwa kwa kuchochea maandamano yasiyo na kikomo kupinga matokeo. Mambosasa alihojiwa na vituo vya ITV na TBC na kutoa madai hayo hayo ya ugaidi.
 
Back
Top Bottom