Adverse Effect
JF-Expert Member
- Oct 8, 2017
- 3,518
- 8,967
Tunapokutana na matatizo au changamoto mbalimbali tunapata fursa ya kuchagua mambo mawili. Mosi ni kukabiliana na changamoto na kujaribu kuzitatua ili zisiwepo na jambo la pili ni kujaribu kuzoea changamoto na kuendelea kuishi nazo hata kama zinakutesa.
Miaka mitano iliyopita bi mkubwa wetu mama mzazi alipata hitilafu katika mwili wake ambapo iligundulika tatizo kwenye pingili za uti wa mgongo na kupelekea sehemu za miguu kufa ganzi na kukosa nguvu kabisa.
Tulitumia bima ya afya katika mchakato wote wa matibabu yake na ninakiri bima ilisaidia sana hadi kufika hospitali ya rufaa ila hatua ya mwisho Kuna matibabu ambayo bi mkubwa alitakiwa afanyiwe ambayo ni upasuaji na ilionekana bima tunayotumia haiwezi kugharamia.
Wataalamu walituambia bi mkubwa akatibiwe India au Kuna hospitali binafsi ya daktari bingwa fulani ambaye yeye n kwa wakati huo angeweza akamsaidia mgonjwa wetu ila gharama ilikuwa kubwa sana na bima haitatumika ni pesa mbele.
Kabla sijamalizia kuelezea kilichotokea kwa mgonjwa wetu naomba nieleze kwanini nimeandika Uzi huu.
Katika kipindi cha takribani miongo miwili kumetokea matukio yanayohusisha ukiukwaji wa haki za binadamu katika Taifa letu tunalolipenda Tanzania.
Matukio hayo ya ukiukwaji wa haki za binadamu yamepekekea kuporwa kwa haki ya msingi ikiwepo haki ya kuishi au uhai.
Tumeshuhudia wananchi wakitekwa, wakiteswa, kubakwa, kulawitiwa na mwisho kuuwawa. Mbaya zaidi udhalimu na uhalifu huo unahusishwa moja kwa moja au kwa namna nyingine na vyombo vya dola, makundi au magenge yenye mkono wa viongozi wa serikali wasio waadilifu. Lazima tuseme ukweli sio viongozi wote wa serikali wanahusika na kufurahia mambo maovu yanayotokea katika Taifa letu
Viongozi au watendaji wa serikali ambao wanahusika kutekeleza udhalimu, dhuluma, ubatili na hata mauaji sio kwamba hatuwajui na kuwafahamu. Wanaofanya na kutekeleza maagizo kutoka juu hawaishi katika sayari ya mars au katika milima ambayo hatuwezi kuwafikia na kuwaona
Lengo na dhamira kufahamu na kutambua hao watendaji wanapoishi wao na familia zao sio kwa ajili ya kuwafanyia ubaya au kuwalipizia kisasi bali ni kuwakumbusha pale inapolazimu na kubidi kuwa Kuna maisha ya kazi na maisha ya kitaa/mtaa na mwisho kuwaeleza ukweli kuwa kazi na majukumu yana mwisho ila mtaa na wanaishi mtaani watakuwepo milele na milele.
Wote wanaopenda haki raia na wasio raia( walio katika vyombo vya dola) mnapaswa kuliangalia na kutizama jambo la haki za binadamu katika muktadha wa kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa.
Ninaamini wapo watendaji wema wa serikali kama mahakimu, maaskari, mapolisi, magereza ambao wanapenda na kuthamini haki isipokuwa wamekuwa wakipokea maelekezo wanayoita yametoka juu.
Tulipofikia sasa itakapobidi italazimika kutumia teknolojia kuweka alama isiyofutika na kuweka wazi makazi, mitaa, location au kuonyesha faragha ikiwepo mke au watoto. Sidhani kama tunapaswa kufika huko? Ila ikibidi hakutakuwa na jinsi.
Kwa kumalizia kuhusu mgonjwa wetu ni kwamba ilitulazimu kwenda kwa daktari bingwa katika hospitali yake binafsi ila matibabu yalishindikana sababu ya gharama kubwa ambazo hatukuweza kulipia kipindi hicho.
Mwisho tulipata wazo la kufahamu nyumbani kwake anapoishi na familia yake na hapa ndipo tulipo para suluhisho na amini usiamini bi mkubwa wetu alitibiwa kwa punguzo la gharama ya karibu asilimia thelathini na tuliweza kumudu na mpaka sasa na leo hii tunashukuru bi mkubwa ni mzima wa afya ana miaka sabini na moja anaendelea vizuri ukiacha changamoto za hapa na pale za utu uzima.
Miaka mitano iliyopita bi mkubwa wetu mama mzazi alipata hitilafu katika mwili wake ambapo iligundulika tatizo kwenye pingili za uti wa mgongo na kupelekea sehemu za miguu kufa ganzi na kukosa nguvu kabisa.
Tulitumia bima ya afya katika mchakato wote wa matibabu yake na ninakiri bima ilisaidia sana hadi kufika hospitali ya rufaa ila hatua ya mwisho Kuna matibabu ambayo bi mkubwa alitakiwa afanyiwe ambayo ni upasuaji na ilionekana bima tunayotumia haiwezi kugharamia.
Wataalamu walituambia bi mkubwa akatibiwe India au Kuna hospitali binafsi ya daktari bingwa fulani ambaye yeye n kwa wakati huo angeweza akamsaidia mgonjwa wetu ila gharama ilikuwa kubwa sana na bima haitatumika ni pesa mbele.
Kabla sijamalizia kuelezea kilichotokea kwa mgonjwa wetu naomba nieleze kwanini nimeandika Uzi huu.
Katika kipindi cha takribani miongo miwili kumetokea matukio yanayohusisha ukiukwaji wa haki za binadamu katika Taifa letu tunalolipenda Tanzania.
Matukio hayo ya ukiukwaji wa haki za binadamu yamepekekea kuporwa kwa haki ya msingi ikiwepo haki ya kuishi au uhai.
Tumeshuhudia wananchi wakitekwa, wakiteswa, kubakwa, kulawitiwa na mwisho kuuwawa. Mbaya zaidi udhalimu na uhalifu huo unahusishwa moja kwa moja au kwa namna nyingine na vyombo vya dola, makundi au magenge yenye mkono wa viongozi wa serikali wasio waadilifu. Lazima tuseme ukweli sio viongozi wote wa serikali wanahusika na kufurahia mambo maovu yanayotokea katika Taifa letu
Viongozi au watendaji wa serikali ambao wanahusika kutekeleza udhalimu, dhuluma, ubatili na hata mauaji sio kwamba hatuwajui na kuwafahamu. Wanaofanya na kutekeleza maagizo kutoka juu hawaishi katika sayari ya mars au katika milima ambayo hatuwezi kuwafikia na kuwaona
Lengo na dhamira kufahamu na kutambua hao watendaji wanapoishi wao na familia zao sio kwa ajili ya kuwafanyia ubaya au kuwalipizia kisasi bali ni kuwakumbusha pale inapolazimu na kubidi kuwa Kuna maisha ya kazi na maisha ya kitaa/mtaa na mwisho kuwaeleza ukweli kuwa kazi na majukumu yana mwisho ila mtaa na wanaishi mtaani watakuwepo milele na milele.
Wote wanaopenda haki raia na wasio raia( walio katika vyombo vya dola) mnapaswa kuliangalia na kutizama jambo la haki za binadamu katika muktadha wa kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa.
Ninaamini wapo watendaji wema wa serikali kama mahakimu, maaskari, mapolisi, magereza ambao wanapenda na kuthamini haki isipokuwa wamekuwa wakipokea maelekezo wanayoita yametoka juu.
Tulipofikia sasa itakapobidi italazimika kutumia teknolojia kuweka alama isiyofutika na kuweka wazi makazi, mitaa, location au kuonyesha faragha ikiwepo mke au watoto. Sidhani kama tunapaswa kufika huko? Ila ikibidi hakutakuwa na jinsi.
Kwa kumalizia kuhusu mgonjwa wetu ni kwamba ilitulazimu kwenda kwa daktari bingwa katika hospitali yake binafsi ila matibabu yalishindikana sababu ya gharama kubwa ambazo hatukuweza kulipia kipindi hicho.
Mwisho tulipata wazo la kufahamu nyumbani kwake anapoishi na familia yake na hapa ndipo tulipo para suluhisho na amini usiamini bi mkubwa wetu alitibiwa kwa punguzo la gharama ya karibu asilimia thelathini na tuliweza kumudu na mpaka sasa na leo hii tunashukuru bi mkubwa ni mzima wa afya ana miaka sabini na moja anaendelea vizuri ukiacha changamoto za hapa na pale za utu uzima.