Je, Kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia kuanzia shule za sekondari mpaka vyuo vikuu? Jadili

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901


Kuna watu wanasema kuwa lugha ya kufundishia kwenye mfumo wetu wa Elimu iwe Kiingereza kwa sababu Kiingereza ndo lugha ya dunia na uandishi wa vitabu mbali mbali na ugunduzi wa technologia nyingi ikiwepo kompyuta uko kwenye lugha ya kiingiereza.

Watetezi wa hoja hii wanasema nchi nyingi zlilizoendelea zinatumia kiingereza kwa hivyo sisi tulio nyuma kimaendeleo hatuwezi kuacha kufundisha watoto wetu kwa lugha hiyo ya dunia.

Watetezi wa hoja hii wanasema tusipojifunza kiingereza tutashindwa kuwasiliana na nchi tajiri duniani kama Uingereza, marekani nk ambazo zinatumia kiingereza. Kushindwa kuwasiliana huko kutaathiri mahusiano yetu na nchi Tajiri na mwishowe tutashidwa kufanya biashara na nchi hizo. Kubwa zaidi, hata vijana wetu hawataweza kuajiriwa katika nchi hizo.

Watetezi wengi wa hoja hii ni wanasiasa ambao watoto wao ama wanasoma nje ya nchi ama wako ndani ya nchi lakini kwenye shule za st xyz au accademy ambazo shule zinazotumia kiingereza kama lugha ya kufundishia.

Kwa upande wa pili, Wako wanaosema kiingereza isiwe lugha ya kufundishia kwenye shule na vyuo vyetu. Watetezi wa msimamo huu wengi wao (si wote) ni wataalamu wa vyuo vya juu, wao wanasema kiingereza ifundishwe kama lugha nyingine yo yote kama kifaransa, kichina, kireno, kiarabu nk ili watanzania wawasiliane na watu wengine duniani. Wao wanataka lugha ya kufundishia shuleni na vyuoni iwe kiswahili.

Sababu zao ni kama hizi zifuatazo:

Kwamba wanadai kuwa kisayansi Binadamu yo yote hufikiri kwa kutumia lugha ya kwanza wa wazazi wake, kisha hulazimika kutafsiri lugha hiyo kichwani kama atalazimika kuongea kiingereza na kwamba mchakato huu unarudisha nyuma au unachelewesha ubunifu wa watoto na hivyo tunaishia kuwa na wasomi waliokariri badala ya wasomi wanaoibua vitu vipya.

Matokeo yake wahitimu wa vyuo vikuu hawaji na ugunduzi wo wote mpya na mwisho wa siku wasomi wetu wa kukariri kiingereza wameshindwa kututoa kwenye lindi la umasikini pamoja na rasilimali nyingi tulizo nazo.

Pili, kwa kuwa kiingereza yenyewe ni tabu, wengi wanadhani kuwa wanafunzi wengi wa sekondary wakifika shuleni wanaanza kuhangaika na lugha ya kiingereza matokeo yake uelewa/ufaulu wao kwenye masomo lengwa unaathiriwa.

Watetezi wa hoja hii wanatoa mifano ya nchi kama China, Korea kusini, Malaysia nk ambazo zimeendelea kwa kutumia lugha zao za asili na hawatumii kiingereza hata kwenye mifumo yao ya Elimu. China kwa sasa ndo mkopeshaji wa Marekani.

Kati ya watetezi wa hoja hii wako Dr Martha Qoroo( Dean wa Chuo kikuu cha Dsm) na Jenerali Ulimwengu (mmiliki wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania)

Tume ya jaji Warioba kwenye rasimu yao ya pili walitangaza kiswahili kama lugha rasmi ya Taifa lakini hawakusema pia kwamba Kiingereza kisiwe lugha ya kufundishia -- waliipa kiswahili nguvu lakini kuhusu lugha ya kufundishia walikaa kimya.

kwa maneno rahisi akina Warioba walikwepa mjadala huu na kuamua kukaa katikati, japo katikati yao inaelemea upande wa Kiswahili zaidi hata kama ni kwa kiasi kidogo sana.

Wewe una maoni gani na kwa nini?
 
Mimi na wazalendo wenzangu wenye akili tunataka kiswahili iwe lugha ya kila kitu, kwani China Korea wametoka wapi wapo wapi na lugha zao, wao wameweza sisi tushindwe kwanini.

Hiyo hoja ya wanazuoni ni ukweli mtupu, hatutafika popote kwenye sayansi na fani yoyote kama tunakuja kutumia lugha nyingine tofauti na halisi, elimu ya juu; hata kama itabidi kufumua kila kitu na kuanza upya, akheri hivyo: Nguo ya kuazima haisitiri matako.
 
Tunazihitaji lugha zote mbili Kiswahili kama lugha mama na utambulisho wetu na lugha za kigeni kwa ajili ya mahusiano ya kimataifa
 
Msitudanganye kiswahili sio deal, kiingereza kiliishatupiga bao karne nyingi acheni tutaumia wenyewe. Mfano mdogo tu kupata kazi UN interview iko kiingereza hujui unaachwa.

Mkifanya hivyo wenye uwezo watahamisha watoto wao kusoma nje ya nchi, tunabaki na kiswahili, mi niko wazi Msitudanganye kiswahili hakikufikishi popote tuliishapigwa bao karne nyingi.
 
Ukitaka kuamini kuwa lugha ya kingereza ndio inapaswa kuwa lugha ya kufundishia kuanzia chekechea hadi chuo kikuu na Kiswahili libaki kama somo kwanza jiulize kwanini mtu asome kiswahili miaka zaidi ya tisa

halafu ndani ya miaka minne analazimishwa kujua kingereza vizuri na anaonekana hana sifa ya kwenda chuo au kusoma sekondari kama hajui kingereza hao hao wanasahau wamemfundisha kwa kiswahili zaidi ya miaka saba!

Kusema ukweli lugha ya kiswahili haitusaidii chochote na haina manufaa yeyote kwetu ndio maana secondary na chuo kikuu inatupwa na kutumika kingereza! Nchi yetu imejaa unafiki mwingi hasa kwenye elimu kama kweli kiswahili kingekuwa na muhimu kingefundishwa hadi chuo kikuu!

Lugha ya kiswahili haiwezi kutumika kwenye ushindani kabisa kwenye nyanja zote za uchumi!
 
Msitudanganye kiswahili sio deal, kiingereza kiliishatupiga bao karne nyingi acheni tutaumia wenyewe. Mfano mdogo tu kupata kazi UN interview iko kiingereza hujui unaachwa.

Mkifanya hivyo wenye uwezo watahamisha watoto wao kusoma nje ya nchi, tunabaki na kiswahili, mi niko wazi Msitudanganye kiswahili hakikufikishi popote tuliishapigwa bao karne nyingi.

Husichanganye lugha ya elimu na lugha ya mawasiliano,lugha ya elimu ni mahususi kwa kuweka ujuzi na maarifa vichwani mwa watumiaji.KISWAHILI inapaswa iwe lugha ya kufundishia na lugha nyingine ziwe za mawasiliano.

Mfano mwepesi hakuna binadamu anayeota ndoto kwa lugha ambayo si asili yake. KISWAHILI ni miongoni mwa lugha 5 duniani kwa kuenea,

hakuna maarifa yanayopatikana kwa lugha ya kigeni na Waingeleza waliliona hilo wakafuta KIRATINI katika elimu wakatumia lugha yao ya kiingeleza kipindi hicho ikiwa lugha nyonge.
 
Mi naunga mkono hoja, uliposema lugha ya kiingeleza ifundishwe kama somo mojawapo, kama ilivyo shule za msing za serikal; alaf kiswahil iwe lugha rasm ya kufundishia na pia kifundishwe kama somo ktk ngaz zote za elimu, il kuwapata watalam wa kiswahili.

Cha kushangaza ktk taifa hili, kitaifa lugha ya mawasiliano ni kiswahili, na pia lugha ya ofisin ni kiswahil. Lakin mashulen hususan secondary na elimu ya vyuo, lugha ya mawasiliano na ya ofisini ni kiingreza.

Lugha ya kighen ndo imepewa nafas kubwa kuliko lugha mama kiswahili ambapo tulitegemea lugha ya kigen ndo ifundishwe kama somo mojawapo na kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia na pia lugha ya mawasiliano kwa ngaz zote za elimu.

Jambo hil linathibitisha ukolon mambo leo, kwamba kwa kujitambua kwetu ama la bado tuna-tumeukumbatia ukoloni huu wa kuendelea kutawaliwa kiutamadun.

Ujeruman, Ufaransa, China, Italia, Hispania n.K. Walikataa upuuzi huu, na bado wako juu kiuchumi, na ndo nchi zenye ushawishi mkubwa duniani.
 
Husichanganye lugha ya elimu na lugha ya mawasiliano,lugha ya elimu ni mahususi kwa kuweka ujuzi na maarifa vichwani mwa watumiaji.KISWAHILI inapaswa iwe lugha ya kufundishia na lugha nyingine ziwe za mawasiliano.

Mfano mwepesi hakuna binadamu anayeota ndoto kwa lugha ambayo si asili yake. KISWAHILI ni miongoni mwa lugha 5 duniani kwa kuenea, hakuna maarifa yanayopatikana kwa lugha ya kigeni

na Waingeleza waliliona hilo wakafuta KIRATINI katika elimu wakatumia lugha yao ya kiingeleza kipindi hicho ikiwa lugha nyonge.

hapo pa kuota napinga, mi ding angu akilala anaotaga kwa saut tena anaongea english 2 ,cjawai kumsikia akiota lugha nyingine, cjui n kwanin yan
 
Jamani tupende lugha yetu, hakuna mtu anayepinga kujua kiingereza na sio kiingereza tu hata lugha nyingine yoyote mfano kujua kichina miaka ya siku hizi ni dili zaidi kuliko hicho kiingereza na hii inatokana na wachina wenyewe kuheshimu lugha yao.

Hapa suala la msingi ni watu kupata maarifa halafu mtu akatumie hayo maarifa kwa lugha anayotaka, na haya maarifa tutapata vizuri tukitumia lugha yetu kwenye kila kitu.
 
ENGLISH is for (ENGLISH,AMERICANS,) and KISWAHILI ni kwa ajili ya WATANZANIA...hakuna English for Tanzanians hata siku moja...lakini kwa hatua tuliyofikia kubadilika inahitaji nguvu nyingi zaidi...
 
Ruttashobolwa

Mkuu ulichokiongea wewe ni tatizo la sera yaani watunga sera ndio waliofanya hicho ulichokisema kiwe hivyo! Bado sijaona hoja yako!
 
Last edited by a moderator:
Msitudanganye kiswahili sio deal, kiingereza kiliishatupiga bao karne nyingi acheni tutaumia wenyewe. Mfano mdogo tu kupata kazi UN interview iko kiingereza hujui unaachwa.

Mkifanya hivyo wenye uwezo watahamisha watoto wao kusoma nje ya nchi, tunabaki na kiswahili, mi niko wazi Msitudanganye kiswahili hakikufikishi popote tuliishapigwa bao karne nyingi.

Tatizo lako unawaza kuajiliwa, wewe inafikiria interview tu wala huwazi kupata ujuzi na maarifa! Haya ndo madhara ya ukoloni mamboleo! Saud arabia kwani hawajendelea? Ndo nyie mtoto akiongea kiingereza basi unajua mwanao msomi!

Ukoloni mamboleo!
 
Elimu ya tanzania inaporomoka kwa sababu ya hii lugha ya kufundishia, binafsi naamini ktk utendaji wa mtu. Kuna watu ni mabingwa wa kukariri bila hata kuelewa na ndio wanaoenda hadi chuo kikuu mwisho wa siku unakuta hana anachojua.

Leo kiingereza mnasema kipo juu ndo maana mnakitumia na siku kifaransa kikiwa juu mtakiacha kiingereza?

Elimu yetu siku hizo inapimwa kwa mtu kufahamu kuongea kiingereza, nchi zilizoendelea zinacheza na akili zetu!

Mi naona km lengo la kiingereza ni kwaajili ya mawasiliano basi kifundishwa km somo kwa misingi ya watu wapate uwezo wa kuwasiliana kwa lugha hiyo na wageni na kiswahili kitumike kufandishia masomo mengine kwa lengo la kuwafanya wanafunzi wapate na waelewe vyema kinachofundishwa!

Wanafunzi wanapata ugumu sn kuuliza maswali kwa sababu ya kikwazo cha lugha na majibu yao yamebaki kuwa 'YES'. Hiki kitu kinaturudisha nyuma sn kitaaluma watoto wanahitimu kidato cha nne hana anachojua zaidi ya kukariri defination ambazo haelewi hata zina maana gani.

KUKIPINGA KISWAHILI NI UWOGA WA KUJITEGEMEA.
 
Husichanganye lugha ya elimu na lugha ya mawasiliano,lugha ya elimu ni mahususi kwa kuweka ujuzi na maarifa vichwani mwa watumiaji.KISWAHILI inapaswa iwe lugha ya kufundishia na lugha nyingine ziwe za mawasiliano.

Mfano mwepesi hakuna binadamu anayeota ndoto kwa lugha ambayo si asili yake. KISWAHILI ni miongoni mwa lugha 5 duniani kwa kuenea,

hakuna maarifa yanayopatikana kwa lugha ya kigeni na Waingeleza waliliona hilo wakafuta KIRATINI katika elimu wakatumia lugha yao ya kiingeleza kipindi hicho ikiwa lugha nyonge.

Wewe ndio mfano wa watu wanaopaswa waachane kabisa na kiswahili, angalia umekitumia kwa muda gani na bado huwezi kutofautisha lati ya L au R
 
Kukikataa Kiswahili ni Kujikataa ni kujikana, kuona kiingereza ni lugha bora kuliko Kiswahili ni utumwa mays kabisa! Kiingereza hakikufika hapo kilipofika kwa bahati mbaya waliweka mipango thabiti wakawekeza sasa wanafaidi matunda! Badala na sisi kufanya hivyo tunaishia kuiponda lugha yetu mtazamo wa kipuuzi sana huu
 
Mfano mwepesi hakuna binadamu anayeota ndoto kwa lugha ambayo si asili yake. KISWAHILI ni miongoni mwa lugha 5 duniani kwa kuenea,
I can prove you wrong! Mara kibao tu watu tunaona na tunaongea maneno ya kimombo kama Ooh...my God, Jesus help me. Kuna watu wanaota na utaskia https://jamii.app/JFUserGuide, ooh...https://jamii.app/JFUserGuide it!
 
KINGEREZA ISIWE LUGHA YA KUFUNDISHIA TANZANIA

Mfumo lugha kufundishia kumewaathiri wengi sana ikiwemo na mimi kwa sababu zifuatazo.

1 lugha gani na mpya
mwanafunzi hulazimika kuchukua mda mrefu kujisomea kwa kukariri wakati mwingine huwalazimu wanafunzi kutunga wimbo ili alazimishe kukiriri vizuri anachokisoma.

2, mfumo huu kweli unarundisha nyuma uwezo wa mtoto katika hali ya kutafakari kimpya.
nakumbuka mimi wakati nasoma nilazimika kila wakati nikitembea nikiwa natafakari mawazo yangu ni KUKARIRI misamiati ya kingereza tu, lakn siyo kutafakari na nakuwaza kile nilichofundishwa.

3, mfumo huu unaumiza akili, kwa sababu utalazimisha kuelewa na unapotaka kupata jibu kamili kile unachotaka kukielewa unakutana na msimiat migumu wa kingereza matokeo yake unakataa tamaa, kuendelea kuutafuta ukweli.

4, hurundisha nyuma parformance ya mwanafunzi.
mimi nakumbuka nikiwa nasoma shule za msingi parfomance yangu darasani ilikuwa zuri sana, tena bila hata kujisomea..
 
Shy land

Ni kweli uliyosema shyland lkn hicho KISWAHILI watoto wanafeli hawajisomei Kama ww ulivyosema ulikua unafauru bila ya kusoma.

Masomo yakifundishwa kwa kiswahili watoto watafauru lkn ndo watakua wajinga zaidi.
Wanafunzi wetu hawajui Ku reason kabisa wao ni kupokea tu anachoongea mwl.

Co kua napinga kiswahili kisitumike ila kuwe mkakayi Wa hali ya juu kihakikisha wanafunzi wanajisomea na wanaweza kuijtambua.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom