Je, kila Taifa lina shetani wake analiongoza?

Hata Shetani mwenyewe ni ushairi tu, hayupo. Ni tungo za watu tu.


Mungu aliyeandikwa kwenye hivi vitabu kama Biblia na Quran pia hayupo.

Ni hekaya za watu tu.

IMG_8413.JPG
 
Buana wewe nimewahi kusikia mala nyingi kua kuna viumbe kama majini mizumu inasaidika kua hao viumbe wanaishi hua sipati majibu maana hakuna anayenithibitishia kwa macho nikashuhudia je unautambuzi na hivi vitu tuanzie hapo
Kuna mambo mengi tunakwenda kwa mazoea tu.

Kuna jamaa mmoja aliketq story hapa, kaenda Rukwa huko karibu na ziwa, watu hawana elimu, hawana maji safi, kipindupindu kipo nje nje. Watu wakapata kipindupindu, wakawa wanakufa, lakini wanakijiji wanashabikia uchawi, wanasema wamelogwa.

Kibaya zaidi, hata wataalam wa afya wao nao wanaamini hayo mambo, kwa sababu, hata kama wamekuja kusoma baadaye, utotoni wamelelewa katika mazingira ya kuamini uchawi. Old habits die hard.

Mimi sikatai kwamba huwnda kuna vitu hatuvioni. Mpaka miaka 500 iliyopita vijidudu kama bacteria na virus vilikuwa havionekani. Watu wakajioanga, wakasema hapa kuna vitu hatuvioni vinasababisha magonjwa. Wakatengeneza darubini nzuri mpaka wakaviona. Ikawa establishwd acientific fact. Unaweza kutest hata wewe kwa kununua darubini zinazotqkiwa kuwwza kuona bacteria na virus.

Sasa hao viumbe majini na mizimu, utathibitishaje wapo kweli na si hadithi za watu tu?

Maana huko kwetu sehemu nyingibhakuna umeme, watu wanakaa gizani usiku, watoto wanalia kwa kuogopa giza, mama zao wanasema mtoto analia kwa sababu kaona jini. Na mtoto akisikia hivyo mama yake kasemq anakua huku akiamini habari za majini, hata kama ni hekaya za uongo.

Kibaya zaidi hata kwenye vitabu vya dini vunavyoaminiwa na watu bila kuhoji wanataja mambo ya majini na uchawi. Watu wanaamini.

Ukiwataka wakupe proof ya kuwapo majini na uchawi wanashindwa.

Twende kwa proof. Tuache hekaya.

Wapi proof ya kuwepo majini?
 
Kupigana si lazima kwa ngumi na mawe. Kuna kupigana kisheria, kimaneno, kisiasa, kiimani.
Nikizumgumza jambo ukanipinga na mm nikaanza kukupinga hapo tunapigana kwa maneno au tunabishana.
So ?
 
Shetani wa bongo anaweza kuwa nani?
Ukisoma kitabu cha Daniel. Kuna kipindi Daniel wakati yupo huko Uajemi aliamua kufunga kwa wiki tatu. Hakuoga, hakunywa pombe(divai), hakula nyama wala msosi wowote mzuri. Sasa kumbe malaika aliyekuwa ametumwa kuleta majibu wakati analeta akakutana na mkuu wa ufalme wa Uajemi, wakaanza kupigana kwa siku 21. Malaika akaelemewa hadi alipokuja Mikaeli, malaika mkuu kumsaidia. Kwa hiyo yeye akapeleka ujumbe na kumuacha Mikaeli akimalizana na mkuu wa Uajemi na waambata wake.

Sasa huyu mkuu wa ufalme wa uajemi aliyeweza kupambana na malaika na kumzidi nguvu hadi Malaika mkuu akaja kumsaidia ni nani? Inawezekana alikuwa ni binadamu? Au ni aina ya shetani?

Je, kila taifa lina shetani wake wa kuliongoza?

Hapa ni Daniel sura ya kumi kuanzia mstari wa 11 lakini ishu yenyewe ni huo mstari wa 13.

11 Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.

12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.

13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.

15 Na alipokwisha kusema nami
 
Uajemi imetumika kama nchi au mkoa fulani.
Na vita inayozungumziwa hapa ni ya kiroho kati ya shetani na MUNGU.

Kwenye kila nchi au eneo fulani kuna madhabahu za kishetani zinazotengenezwa na binadamu wanaomuabudu shetani ili kusimamisha au kuwakilisha utawala wa shetani hapa duniani.

Hizi madhabahu zinatawaliwa na majeshi ya kipepo (wawakilishi wa shetani maana shetani ameshafungiwa kuzimu). Kazi kubwa ya hawa mapepo au "wakuu wa giza" ni kupinga au kuzuia baraka za wanadamu zinazotoka kwa Mungu "Efe 6:10-13".

Ndio maana sehemu zenye wachawi/ washirikina wengi ni ngumu kufanikiwa endapo hutakuwa na msaada wa NGUVU ZA MUNGU; Vinginevyo uungane nao.
Ndo malaika alishindwa na hizo nguvu
Kwanza ki roho ni nini....❓
Vita vya kiroho vikoje hivyo unapigana kwa kuhisi tu kua unaadui bila kumuona ama imekaaje hapo ebu nieleweshe
 
Ndo malaika alishindwa na hizo nguvu
Kwanza ki roho ni nini....❓
Vita vya kiroho vikoje hivyo unapigana kwa kuhisi tu kua unaadui bila kumuona ama imekaaje hapo ebu nieleweshe
Ili nijue naanzia wapi kukuelewesha,
Je unafahamu kuna uchawi?
 
Ukisoma kitabu cha Daniel. Kuna kipindi Daniel wakati yupo huko Uajemi aliamua kufunga kwa wiki tatu. Hakuoga, hakunywa pombe(divai), hakula nyama wala msosi wowote mzuri. Sasa kumbe malaika aliyekuwa ametumwa kuleta majibu wakati analeta akakutana na mkuu wa ufalme wa Uajemi, wakaanza kupigana kwa siku 21. Malaika akaelemewa hadi alipokuja Mikaeli, malaika mkuu kumsaidia. Kwa hiyo yeye akapeleka ujumbe na kumuacha Mikaeli akimalizana na mkuu wa Uajemi na waambata wake.

Sasa huyu mkuu wa ufalme wa uajemi aliyeweza kupambana na malaika na kumzidi nguvu hadi Malaika mkuu akaja kumsaidia ni nani? Inawezekana alikuwa ni binadamu? Au ni aina ya shetani?

Je, kila taifa lina shetani wake wa kuliongoza?

Hapa ni Daniel sura ya kumi kuanzia mstari wa 11 lakini ishu yenyewe ni huo mstari wa 13.

11 Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.

12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.

13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.

15 Na alipokwisha kusema nami
Kwenye ulimwengu wa roho, anga huwa zina wakuu wake, Katika hili Malaika ambaye ni messenger, alikutana na malaika mpigana vita wa upande ule mwingine. Malaika Gabriel ni special kwa ajili ya kupeleka jumbe tu na si kwa ajili ya kupigana vita. na ndiyo maana alijaribu lakin akashindwa. Malaika special kwa ajili ya vita ni Mikael. Kumbuka kuwa huyu aliyekuwa amebeba ujumbe wa Daniel. ndiyo huyo huyo alyepeleka ujumbe kwa Mariam kumweleza kuwa atamzaa mtoto Yesu
 
Hoja kuu hapa ni kwamba iweje malaika huyu azidiwe uwezo na shetani?

Luka 4:5 Basi akampeleka juu na kumwonyesha mara moja falme zote za dunia inayokaliwa.6 Kisha Ibilisi akamwambia: “Nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, nami humpa yeyote ninayetaka.7 Kwa hiyo, ukifanya tendo la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.”
 
Kupigana si lazima kwa ngumi na mawe. Kuna kupigana kisheria, kimaneno, kisiasa, kiimani.
Nikizumgumza jambo ukanipinga na mm nikaanza kukupinga hapo tunapigana kwa maneno au tunabishana.
kwa hiyo;
MUNGU anayeweza kukupa mamlaka na bado mamlaka hayo yakapingwa na kiumbe kingine?

kama jibu ni NDIO kwa hiyo mungu anaweza mengi na sio yote?

kama jibu ni HAPANA hao wafalme wa uajemi walipata wapi nguvu ya kumpinga malaika alietumwa na MUNGU mpaka siku 21 zinapita?
 
Back
Top Bottom