Je, kila Taifa lina shetani wake analiongoza?

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Ukisoma kitabu cha Daniel. Kuna kipindi Daniel wakati yupo huko Uajemi aliamua kufunga kwa wiki tatu. Hakuoga, hakunywa pombe(divai), hakula nyama wala msosi wowote mzuri. Sasa kumbe malaika aliyekuwa ametumwa kuleta majibu wakati analeta akakutana na mkuu wa ufalme wa Uajemi, wakaanza kupigana kwa siku 21. Malaika akaelemewa hadi alipokuja Mikaeli, malaika mkuu kumsaidia. Kwa hiyo yeye akapeleka ujumbe na kumuacha Mikaeli akimalizana na mkuu wa Uajemi na waambata wake.

Sasa huyu mkuu wa ufalme wa uajemi aliyeweza kupambana na malaika na kumzidi nguvu hadi Malaika mkuu akaja kumsaidia ni nani? Inawezekana alikuwa ni binadamu? Au ni aina ya shetani?

Je, kila taifa lina shetani wake wa kuliongoza?

Hapa ni Daniel sura ya kumi kuanzia mstari wa 11 lakini ishu yenyewe ni huo mstari wa 13.

11 Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.

12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.

13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.

15 Na alipokwisha kusema nami
 
Luka 4:5 Basi akampeleka juu na kumwonyesha mara moja falme zote za dunia inayokaliwa.6 Kisha Ibilisi akamwambia: “Nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, nami humpa yeyote ninayetaka.7 Kwa hiyo, ukifanya tendo la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.”
 
Mfalme wa Uajemi ni lugha ya kinabii tu lakini kiuhalisia alimaanisha Shetani ndiye aliyekuwa anapambana naye
Mmmh!
Waefeso 6 12
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

... mfalme wa uajemi analala hapo kwenge falme ( principality ) huyu anapokea wazo au task kutoka kwa lucifer ( satan ).. anaeipeleka kwa authority ( mamlaka ) hawa ni malaika waasi ila pia na kwa Mungu kuna malaika wenye lank hizi.. ila hawa wanao fanya kazi na lucifer ni waasi ila wapo kwenye hizo hizo la lank za ki utendaji.. kina eneo huwa lina kuwa na hizo spirit katika huo huo mtililiko
 
Nshayakanyaga tayari kwa ninavokujua ngoja nikae pembeni kuusoma mchezo
Tunaeleweshana tu.
Ubuntu.

Mimi nafikiri, tukichunguza sana, tutakuta habari mpya kabisa ambazo zinashangaza mara nyingi sana kuliko hadithi za Mungu.

Ukisoma Quantum Physics na relativity utaona mambo ya time and space not being absolute.

A lot of our misconceptions are narrow minded, because we are slaves to the scale of our existence in the universe.

Ukienda kwenye quantum level, kwenye cosmic levels, at the centers of black holes, kuna maajabu mengi sana bado hatujayaelewa.

Na kabla ya kuyaelewa hayo tunakimbilia hadithi ya kitoto ya Mungu kuumba vitu.
 
Oya Tofautisha kupinga na kupigana.
Kupigana si lazima kwa ngumi na mawe. Kuna kupigana kisheria, kimaneno, kisiasa, kiimani.
Nikizumgumza jambo ukanipinga na mm nikaanza kukupinga hapo tunapigana kwa maneno au tunabishana.
 
Kupigana si lazima kwa ngumi na mawe. Kuna kupigana kisheria, kimaneno, kisiasa, kiimani.
Nikizumgumza jambo ukanipinga na mm nikaanza kukupinga hapo tunapigana kwa maneno au tunabishana.
Vita ni vita mdhee na kiuhalisia hakuna vita vya maneno eti vikaitwa vita hayo ni mabishano malumbano. Nk
 
Tunaeleweshana tu.
Ubuntu.

Mimi nafikiri, tukichunguza sana, tutakuta habari mpya kabisa ambazo zinashangaza mara nyingi sana kuliko hadithi za Mungu.

Ukisoma Quantum Physics na relativity utaona mambo ya time and space not being absolute.

A lot of our misconceptions are narrow minded, because we are slaves to the scale of our existence in the universe.

Ukienda kwenye quantum level, kwenye cosmic levels, at the centers of black holes, kuna maajabu mengi sana bado hatujayaelewa.

Na kabla ya kuyaelewa hayo tunakimbilia hadithi ya kitoto ya Mungu kuumba vitu.
Buana wewe nimewahi kusikia mala nyingi kua kuna viumbe kama majini mizumu inasaidika kua hao viumbe wanaishi hua sipati majibu maana hakuna anayenithibitishia kwa macho nikashuhudia je unautambuzi na hivi vitu tuanzie hapo
 
Uajemi imetumika kama nchi au mkoa fulani.
Na vita inayozungumziwa hapa ni ya kiroho kati ya shetani na MUNGU.

Kwenye kila nchi au eneo fulani kuna madhabahu za kishetani zinazotengenezwa na binadamu wanaomuabudu shetani ili kusimamisha au kuwakilisha utawala wa shetani hapa duniani.

Hizi madhabahu zinatawaliwa na majeshi ya kipepo (wawakilishi wa shetani maana shetani ameshafungiwa kuzimu). Kazi kubwa ya hawa mapepo au "wakuu wa giza" ni kupinga au kuzuia baraka za wanadamu zinazotoka kwa Mungu "Efe 6:10-13".

Ndio maana sehemu zenye wachawi/ washirikina wengi ni ngumu kufanikiwa endapo hutakuwa na msaada wa NGUVU ZA MUNGU; Vinginevyo uungane nao.
 
Back
Top Bottom