Je, inawezekana mtu akalala na mwenye UKIMWI tena peku na asipate UKIMWI?

Wadau,

Nimeisoma kwa umakini mkubwa sana thread ya mdau mmoja aliyekata shauri na kuamua kwenda kupima HIV!

Kiukweli kabisa toka katika uvungu wa moyo wangu nampongeza sana na Mwenyezi Mungu amuokoe huyu ndugu! Lakini kati ya wachangiaji waliosimama kidedea kuchangia thread hii, mchangiaji mmoja nimemnukuu akisema, "hukujua kuwa kupata UKIMWI ni kazi ngumu sana.."

Na kwa bahati mbaya alipoombwa kutoa elimu na uzoefu wake na baadhi ya wadau, hakuonekana tena! Usemi huu umeibua tafakari na tafakuri nyingi katika halmashauri yangu ya kichwa, nikirejea na siku za mgongoni nikiwa darasani mwalimu pia aliwahi kusema maneno sawia na ya mchangiaji wa leo na toka ya hapo, swali hili limetoka katika tawala za kichwa changu kwamba, "Je, inawezekana mtu akalala (siyo kulala huku kwa kawaida, tafsida imezingatiwa) na mtu mwenye UKIMWI tena bila condom na asipate UKIMWI?".

Nisaidieni wadau.

Nawasilisha.

======
 
Mkuu Deception ni kweli kabisa siyo wote watakuelewa na siyo wote watafuata kile unachosema. Sababu ni kwamba watu wengi hatuna kasumba ya kusoma zaidi ya kile tulichofundishwa, pia hatuna kasumba ya kuuliza nje ya kile tunachofundishwa. Mimi sina hata chembe ya udaktari, lakini haya matibabu ya asili nimeanza kuyafuatilia baada ya kuanza kujiuliza maswali mengi bila kupata majibu ya maana, nikawa na interest ya kusoma zaidi habari zake ndo nikagundua ni kinga nzuri tu.

Hizi dawa au kinga asili zinatumika pia hata kwenye mifugo. Kule jukwa la biashara kuna uzi umegusia tiba za asili. Sasa mimi kwa vile tayari nazitumia, sikupata tabu kuamini kuwa zinafaa kwa mifugo pia. Kifupi mi nafuga kuku, wachache tu kama mia hivi wa kienyeji kwa matumizi ya familia. Hawa kuku natumia sana kinga asili na wako poa, magonjwa ya mlipuko yanaibuka kuku wajirani wanakufa wangu wapo tu, nikiwaambia nachotumia hawaamini wanabaki kunishangaa tu. Ila napo inapotokea ugonjwa fulani naanza na hizi za madukani zinazofanya kazi fasta then naendelea na asilia zangu kama kawaida. Tena hata hivyo nimekunja kugundua magonjwa yanaibuka pale ninapozembea kuwapa kinga za asili au ninapokuwa nimesafiri kwa muda mrefu waliopo wakazembea kuwapa. Lakini ukiifanya kama sehemu ya diet mbona magonjwa utayasikia kwa jirani tu.
Mkuu naomba inijuze nami kuhusi hiyo kinga unayoitumia kwa mifugo. Nami nina kuku wakienyeji nafuga huko shamba.
 
Rafiki yangu ambaye nimesoma nae o level baada ya kufeli kuendelea na masomo alifanya uamuzi wa kuoa ila mwisho wa siku mke alipata ujauzito na wakaenda kupima kama wazazi wa mtoto, mwanamke alikutwa na maambukizi ila mwanaume hana almost two years katika ndoa,
nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimemfuatilia sana Deception toka alivyoanza kuelezea kuhusu UKIMWI, VVU na ARV
Kwa uelewa wangu ni kuwa UKIMWI ULikuwepo miaka mingi iliyopita ila VVU wamekuja kuitangaza 1980's na kudai ndio inasababisha UKIMWI.
Baada ya Dr.galo kuitangaza VVU kuwa ndio chanzo cha UKIMWI wakaja jopo la madaktar akiwepo dokta margareth kutangaza ARV kuwa zinasaidia kufubaza kirusi ie.VVU.na hapo biashara ya ARV ikakua na ARV ndizo zinazosababisha vifo kwa watu wengi kutokana na madhara yake.
Mimi nakubaliana na Deception ARV zinamadhara sana
Upo sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi binafsi kuna kitu kimenifungua akili, aunt yangu alikuwa na mgogoro na mume wake aliyekuwa na mahusiano nje ya ndoa muda mrefu tena ulifikia pabaya baada ya mumewe kuzaa na mmoja wa wanawake zake, kukafanywa vikao mume akaomba msamaha ila aunt akasisitiza hatoweza shiriki naye tendo la ndoa mpaka wapime HIV, mume akakubali mbele ya kikao eehhh walivyoenda kupima jamani aunt yangu akakutwa ameathirika na mume hajaathirika, hii imemfanya aunt azidi kudhoofika kwasababu mume ambaye hakuwa mwaminifu ndo mzima jaman yaan ana mawazo sasa imekuwaje au mume ni carreer yaan hamna anayeelewa, ila baada ya kusoma hapa kuna kitu nimepata i wish nimuonyeshe asome hapa apunguze stress maskini maana ndo znamfubaisha sababu huyo mwanamke aliyezaa na uncle anamsimanga maskin mpaka huruma
Ulete mrejesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu mwenye akili timamu unakaa kwenye keyboard na kusema eti viongozi wakikataa deal la dawa za ARV watatolewa madarakani. Mbona dunia iko wazi sana soma ndugu yangu na fuatilia vitu . Jiulize katika africa nchi ngapi zinawapa wananchi wake ARV. Na why zinawapa na je zile zisizowapa inakuwaje . Just simple fuatilia nchi jirani kama kenya , uganda , mozambique ......kumbuka ukimwi upo dunia nzima . So na dunia nzima watu wanapimwa . Wewe unasema vipimo FAKE sasa hivyo vipimo fake ni bongo peke yake au dunia nzima ? Kama una ukimwi na unatumia ARV acha kwa mpango wako . Kama huna imani na afya yako na unaogopa kupima acha kwa binafsi yako usidanganye watu......kama hutaki kutumia condom kwa sababu zako binafsi pia acha wewe mwenyewe usipotoshe watu.
Wewe ndo hujui kitu.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom