Je, huu ni ukweli uliofichwa kwa miaka mingi?

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
18,914
28,524
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo hivyo ningependa tuisome kwa umakini,tujifikirishe na tujadiliane kwa mapana bila kashfa za kidini,kejeli,matusi,hasira n.k maana mada hii ni kwa ajili ya kujifunza na kubadilishana mawazo,maarifa,elimu n.k sio uwanja wa vita
eve_by_karichristensen-d5ts9pp.jpg

Mada ya leo ni kuhusu ukweli wa mzazi halisi wa Cain ama tuseme kizazi cha nyoka na kizazi cha Adam. Ikumbukwe nyoka anyeongelewa hapa sio nyoka huyu wa sasa anayetambaa naongelea yule wa kabla ya tunda kuliwa.

Reference yangu itakuwa vitabu vya dini kadhaa kuanzia uyahudini,biblia,apocrypha,pseudipigraphi, maandishi ya wanatheolojia na vitabu vya kihistoria.

UTANGULIZI
Kupitia nadharia hii, yote yanaanzia kwenye bustani ya Eden ambapo tunaona shetani kupitia nyoka akimshawishi Hawa "kula tunda" na katika tunda hilo inaaminika linahusianisha ngono ambapo nyoka alimlala Hawa na kumpachika mimba ambayo baadae alikuja kuzaliwa Mtoto wa uzao huo yaani kizazi cha nyoka yaani Cain ili shetani aweze kuharibu uumbaji wa Mungu.

KWANINI NADHARIA HII?
Ili tuamini Nyoka alilala na mwanamke tunaweza tumia vigezo vifuatavyo

1. Adhabu kubwa ya Mungu kwa mwanamke ilikuwa ni kwenye sekta ya ngono sababu ndipo alipoanguka ndio maana Mungu akamhukumu sababu ya tendo la ndoa na mimba aliyobeba pia.

Mwanzo 3:
16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala

Pia shetani tukisoma kwenye kitabu cha biblia (madhehebu kadhaa hukitumia) cha Apocalypse of moses 26:1-4 tunaona hukumu ya Mungu kwa shetani kuwa atamtoa masikio,mabawa na UUME!!!!

Hivyo nadharia hii kuwa ngono ilihusika inapatiwa nguvu kupitia mistari hii

NANI BABA WA CAIN?
Biblia ya kiswahili inasema

Mwanzo 4:1
1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA

Lakini tafsiri iliyofanyiwa uhakiki kupitia New jerusalem Translation inasema hivi kwa kiswahili

...... Nimepata mtoto kutoka kwa malaika wa Bwana

Hivyo kama tafsiri hii ya NJT ina maanisha Adam alikiri kuwa mtoto sio wake ila wa MALAIKA ambaye kwa muktadha huu ni lucifer.

Kwenye biblia ya kiebrania neno lililotumika kwa KUMJUA ni Yada na Eth ambapo Yada baada ya kufanyiwa utafiti mpya limeonekana haimaanishi tu ni kumlala mwanamke bali inamaanisha KUTAMBUA KITU na Eth ina maanisha ALAMA FULANI(mabadiliko) hivyo tukiuandika mstari huu upya kutumia tafsiri ya maneno haya itakuwa hivi;

Adamu akatambua alama/ishara ya mabadiliko juu ya Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kutoka kwa malaika wa BWANA

Kwahiyo mpaka hapa tumeshapata maana tofauti kabisa ya mstari huu si ndio wakuu??

JE KWANINI NASEMA CAIN SIO MWANA WA ADAM
1. Biblia huko mbele inamtaja Cain kama alitokana na ''yule mwovu'' yaani shetani

1 Yohana 3:12
12 si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
blood_by_karichristensen-d6326t2.jpg


2. Biblia inamtambua seth kama mtoto pekee wa Adam maana inadai Henoko alikuwa mtu wa 7 baada ya Adam na ukihesabu utagundua imetaja uzao wa seth peke yake na imemuacha Cain peke yake hivyo ikimaanisha Cain hakutambuliwa kma mwana wa Adam

Yuda 1:14
14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao
Screenshot_2018-08-06-15-44-07-1.png


3. Tunaona hata seth ndio biblia inaonyesha alizaliwa kwa mfano wa sura na mfano wa adam

Mwanzo 5
3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi

Hii yote ikimaanisha Cain hakuwa uzao wa Adam ndio maana hakufanana naye Adam kwa lolote hivyo muandishi hakuona sababu ya kujumuisha jambo hilo alipozaliwa cain.

4. vitabu vinavyotambuliwa na dini ya kiyahudi kama Zohar Pekudei 21:5 kinakubali hoja hii.

Baada ya adam na mke wake kufanya dhambi, na shetani kumjua Hawa na kumnajisi, Hawa alimzaa Cain. Alikuwa na umbo la duniani na kuzimu. Hivyo,alikuwa wa kwanza kuleta kifo duniani,iliyosababishwa na upande wake wa kuzimu,sababu alitokana na uchafu wa najisi ya nyoka (kwa hawa). Asili ya nyoka(shetani) ni udanganyifu,mauaji,na Cain,alijifunza nyendo zake. (Utafsiri binafsi)

HITIMISHO
Kupitia hayo maandiko machache nlioweza kupata ninaweza kufikia hitimisho kuwa kuna uwezekano tumefichwa kwa muda mrefu kuhusu uhalisia wa kilichotokea Eden nikaona nilete nadharia hii JF ili tuweze kufikiri pamoja na kupata ukweli wa jambo hili.

NB: Naomba Moderator msiunganishe nyuzi hii na zingine juu ya bustani ya edeni maana hii imejikita zaidi kwa Cain na sio maisha ya bustanini

Naomba kuwasilisha
 
Ila Biblia inamtambua Seth pekee kama mtoto wa kwanza wa Adam..... Ila seth ni mtoto wa 3 wa Hawa!!! Ikimaanisha abel na cain hawakuwa watoto wa Adam labda kama una chanzo tofauti unaweza kutuelimisha zaidi
niliyekuwa nikimtambua kwa maana ya uzao wa ADAM ulianzia kwa abeli na kuendelea,lakn CAIN peke yake ndio damu ya NYOKA kwa kuwa hata mimba yake ilitungwa wakiwa bado edeni.maelezo zaid kama hautojal ningependa unielimishe maana haya maswala ili uyajue undani wake ni lazma uchimbue kwa kina
 
niliyekuwa nikimtambua kwa maana ya uzao wa ADAM ulianzia kwa abeli na kuendelea,lakn CAIN peke yake ndio damu ya NYOKA kwa kuwa hata mimba yake ilitungwa wakiwa bado edeni.maelezo zaid kama hautojal ningependa unielimishe maana haya maswala ili uyajue undani wake ni lazma uchimbue kwa kina
Kwa hiyo unakubaliana na hoja kwamba Cain hakuwa mtoto wa Adam?? Nafkiri hapa ndio nataka kuelewa
 
niliyekuwa nikimtambua kwa maana ya uzao wa ADAM ulianzia kwa abeli na kuendelea,lakn CAIN peke yake ndio damu ya NYOKA kwa kuwa hata mimba yake ilitungwa wakiwa bado edeni.maelezo zaid kama hautojal ningependa unielimishe maana haya maswala ili uyajue undani wake ni lazma uchimbue kwa kina
Nakubaliana na wewe kwamba mzao wa kwanza wa Adam ni Abel. Ila nijuavyo hakuwa na uzao kwa sababu maisha yake yalikatishwa ghafla kwa hila ya kaka yake Cain.
 
Mwanzo 4:1-2
[1]Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA.
[2]Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.
Mkuu mleta mada mbona kitabu kitakatifu kinasema adam alimjua hawa ndo akampata Kaini wapi wamesema nyoka
 
Umechambua vizuri Sana but ukija kwenye uhalisia wenyewe kuna mambo mengi sana yamefichwa hasa kwenye biblia takatifu,nchi kama ulaya huko wameamua kuachana kabsa na mambo ya dini hasa dini zenye kutumia biblia kama chanzo cha kujua ukweli...tumebaki sisi Africa kutumia biblia kama reference ya chimbuko la uhai wa human race katika ulimwengu huu...kama ni hivyo kwanini sasa nchi zilizoendelea zimeachana na habari kama hizo za kutumia bible kama reference point ya kukuonesha original ya mwanadamu?? do you think kuna uhalisia hapo,?? kama maandiko menyewe kuyaelewa mpaka uconnect dot flan ndo unaanza kupata ukweli..!! kwanini kama ni uhalisia usiwekwe na mwandishi mmoja ila et ukweli mpaka uanze kugess maandiko ya flani na flani ndo unapata connection..dont we see that we are wrong from point of contradiction...??

Unajua kuna point mimi najaribu kujiuliza kwanini mzungu kaachana na mambo ya bible kwenye kutafuta reality that put human being into existance ila kajikita zaidi na evolution ya cosmos ilivyotokea..?? binafsi swala la biblia kama reference ya kunifanya nidig where I evolved nishaanza kuiacha kabsaa make kuna nadhalia nyingi sana zinaelezea jinsi bible ilivyokuja kuvurugwa na mrumi na kupelekea kufanya inversion na edition tofauti za kurasa ,kitu kilichopelekea watu kutokuielewa vizuri bible kwa undani zaidi...

kuna documentary moja nimeisoma inagusia jinsi vatcan alivyokuja kuedit baadhi ya verses katika bible na kufanya msomaji kupata difficultness namna ya kuelewa the real chronological order ya bible ilivyokuwa...inasemekana kuwa, the real original bible was written in ascending order of knowlege yani imeanza kuelezea namna how the universe arose,na how cretures got into existance and finally how human races got to evolve in this world( universe) ,lakini kutokana na hao mageniuz wa dunia ambao hawakutaka kuuruhusu msahafu huo kusomwa na kila mtu ndo wakaugawanya into different categories na kuchanganya chapters kias kwamba ukisoma mstari wa matayo pekee huwezi kuuelewa mpaka ukajazilizie kwa marko ndo unaanza kupata picha na badae uende matendo ya mitume mpaka waefeso ndo upate half of its reality and robo ya ukweli (truth),,hatuoni kuwa ukweli kuwa bible was real put under several manipulations and editions za kufa mtu ndo mana tunakesha kuujua ukweli...nanukuu maneno ya papo John Paul the second anasema" The bible under its verses has a meaning inside " ndo mana kumepelekea waumiza vichwa nchi za wenzetu kushitukia mchezo huo make unashangaaa watu wanaumiza vichwa miaka nenda rudi lakini hakuna mtu anayeweza kuconnect dots kwenye bible na kucome up na general consensus juu ya uhalisia wa kilichoandikwa kwenye bible...ila inawezekana kabsaa ni kweli the reality was put through the bible but manipurated to loose its truth to the people but for the sake of few ones to understand how nature is.....

Lakini ndo tuseme kuwa bible iwe ngumu kueleweka kiasi hicho kuzidi syllubus ya masomo ya engenering na medicine ambayo ni magumu lakini watu wanasoma wanaelewa na wanaput into practise na kuelewa mfumo mzima wa mambo yaliyoelezewa kwenye mitaala hiyo lakini kwanini bible imekuwa kitendawili kuelewa ukweli wa mambo ndani yake.?? kwanini bible imechanganya zaidi!?? inanifanya nianze kuamini documentary inayosema kuwa ni kweli the bible was written explaining everything what happened since bustan ya eden mpaka anguko la dhambi but it was reversed and edited and some points were hidden to make a meaning got lost ....

Naumiza kichwa sana juu ya tafsiri ya maneno yaliyomo ndani ya biblia ya sasa inapojaribu kuelezea jinsi uzao uliopo ulipotoka lakini stili inafell kuelezea how different races zilivyokuja kutokea au ndo kusema kwamba shetani aligawanya hizi race katika hali tofauti tofaut kulingana na pendekezo lake...?? ngumu kumeza hii ...sometimes if you stick yourself to get the meaning from the bible you will finally land into errors when comes a matter to understand how the reality is....

Ila kuna principle ambayo binafsi naiamini na inasema kuwa ," aliyekuzidi kukutangulia pia ,tukiangalia watu waliokuletea bible ndo kwanza waiweka mbali na upeo wa macho yao and they are busy to open another window to know the reality ,why are we still finding the unknown inside the edited writtings...?? do you think kwamba tutaweza kuupata ukweli namna uzao huu ulipotoka kupitia maneno yalioandikwa ndani ya biblia ya leo..?? najaribu kujiuliza kwa kichwa tu....

Mwisho nahitimisha kwa kusema kuwa " inasemekana lakini eti kuna kiwango ambacho ukifikia hasa katika mambo ya dini unapewa some real documentary ya mshahafu mzima unavyoelezea how descendant of human race came to arise ...

Na miongoni mwa watu waliosoma baadhi ya mtiririko huo ni Leonardo DA VINCI na ISAAC NEWTON as one of the former seminarians walioaminika na kuambiwa watunze siri hiyo ,mtu mwingine aliyesoma mtiriko huo ni bwana mdogo Raphael aliyekuwa geniuz wa kudraw huko Basilia,Roma....haya maneno niliambiwa na jamaaa mmoja yupo mwaka wa 6 upadri na alinidokezea sana kwa hiyo ilikuwa ni katika kujaribu kuelezea how the truth is inside the current bible...
 
Hahhahaha mkuu za siku..... Naheshimu mawazo yako ila je unaweza tusaidia kwanini biblia inamtambua seth pekee kama mtoto wa Adam??? Tuanzie hapo kutuelimisha
Mkuu biblia ni pana sana! Mtiririko wa biblia unaeleza tu kwa wale wanao hitajika mfano Musa anaelezewa yeye tu au Daud pia Yesu mwenyewe hakuna story kuwahusu ndugu zake. Biblia yenyewe inasema kama vyote vingeandikwa dunia isinge weza kubeba.
 
Mwanzo 4:1-2
[1]Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA.
[2]Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.
Mkuu mleta mada mbona kitabu kitakatifu kinasema adam alimjua hawa ndo akampata Kaini wapi wamesema nyoka
Soma uzi upya mkuu nimeshaelezea huu mstari kutoka tafsiri ya kiebrania na haukumaanisha hivi kabisa.... Rudia kusoma utapata majibu
 

Similar Discussions

69 Reactions
Reply
Back
Top Bottom