Kuielewa Biblia inahitaji kuwa na Roho Mtakatifu na Kuwa na imani kubwa sana, Kwanza Hapa wenye imani dhaifu umewayumbisha zaidi.. Biblia haisemi hivi hata kidogo ila hii ni tafsiri yako Potofu.. kwa Kiingereza Biblia inasema Adam made love to his wife Eve, and she became pregnant and gave birth to Cain.Mwanzo 4:1
1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA
Alama yaani aligundua hawa ana mimba ya Cain..... Adam alitambua tu Hawa ana mimba basi ila zaidi ya hapo hakumpa manii yeyote na ndio maana nmeweka hapo mstari unaoonyesha seth ndio alikuwa na mfanano wa Seth na pia Hata agano jipya halimtambui Cain kama mtoto wa ADAM.Adam aligundua alama au tofauti gani iliyopelekea Hawa kupata mimba? Kumbuka mimba inatajwa baada ya Adam kumjua (Kugundua tofauti) Hawa. Unaweza kuelezea kidogo uhusika wa Adam kwenye ujauzito wa Cain?
Mkuu nimeweka hapo tafsiri ya YADA na ETH kayatafute maana yake pia katafute biblia ya NEW JERUSALEM TRANSLATION inasema hivo hivo kama navyodai humu so mimi sijatunga chochote nmetoa kwenye hizo source nlizoziweka hapo. Unless NJT bible huitambuiKuielewa Biblia inahitaji kuwa na Roho Mtakatifu na Kuwa na imani kubwa sana, Kwanza Hapa wenye imani dhaifu umewayumbisha zaidi.. Biblia haisemi hivi hata kidogo ila hii ni tafsiri yako Potofu.. kwa Kiingereza Biblia inasema Adam made love to his wife Eve, and she became pregnant and gave birth to Cain.
She said, “With the help of the Lord I have brought forth a man.”
Hapa Chini ni Maneno ya Mstari Huo Huo Kwa Lugha ya Kiebrania ambayo Ndio Biblia imeandikwa nayo..Tafsiri yake kwa Kiingereza..
Hakuna Mahali Biblia imeonesha Kama anavyosema mtoa Mada..
Kitu Kibaya sana nilichogudua watu Hupenda sana Kuamini Conspiracies Kuliko Ukweli..Hauwezi kumaliza list za conspiracies zipo nyingii Mno.. hasa kwenye haya Maswala ya imani ambayo sayansi Haiwezi Kuprove..Believe the Bible its Right.. it has No Contradiction..
Architectus
Alama yaani aligundua hawa ana mimba ya Cain..... Adam alitambua tu Hawa ana mimba basi ila zaidi ya hapo hakumpa manii yeyote na ndio maana nmeweka hapo mstari unaoonyesha seth ndio alikuwa na mfanano wa Seth na pia Hata agano jipya halimtambui Cain kama mtoto wa ADAM.
Bible nimeweka hapo mkuu haimtambui CAIN kama uzao za AdamNatamani nijifunze na nijue zaidi ILA NAOGOPA ku-corrupt my mind na maandiko haya mengine ya ziada. Biblia jinsi ilivyo iwe ni summary of summary ya kile kilichotokea, basi yanitosha.
Wengine karibuni kwa mada
Hapana hyo hadithi ya TUNDA ni ngono haipo kwenye biblia hiyo imetoka kwenye vitabu vya kiyahudi niliyoquote hapo juu ambavyo havionyeshi Mungu alitoa hyo ruhusa ila kinaeleza hyo story ambayo inadai hawakuwa na ufahamu mambo ya ngono maana wangezaliana ila baada ya shetani kumwambia Hawa kwamba ukilala na mwanaume utazaa mtoto yaani utakuwa na uwezo wa kuumba mwanadamu kama Mungu ndio akabeba mimba ya Cain na ilipelekea Mungu kukasirishwa na kuwaadhibu.Mkuu baada ya Eva kula tunda alimpa na Adam akala,kama tunda hilo ni ngono au kuzini(kama unavyodai) je Adam alifanya kosa gani kwa kufanya ngono na Eva wakati alikuwa kapewa ruhusa ya kufanya hivyo na Muumba?
Hata kama tutasema basi kumjua ina maana moja tu ila bado kwenye issue ya Adam na Hawa biblia inasema kupitia NJT kwamba alitokana na MALAIKA ila kwenye uzao wa Henoko sikuona Cain akisema HENOKO katoka kwa malaika sijui tofauti unaiona hapo mkuuTukienda kwa muktadha wa kiuandishi, unafaham imeandikwa Kaini akamjua mkewe akamzaa Henoko..Mwanzo 4:17, hiyo unaielezeaje mkuu? Henoko hakua mtoto wa Kaini?
Mkuu nimefurahi sana kuona umekuja kwenye nyuzi yangu hii maana siku hizi hupatikani kabisa.... Bila shaka uzi utakaofuata utazungumzia hoja uliyotaja hapo juu ili mje mtiririke na kutuongezea maarifampendwa zitto junior uzi wako fikirishi sana hasa unapotoka nje ya bible na kuna moja ya kitu umekielezea ambacho ni moja ya sababu iliopelekea kutokukubalika kwa baadhi ya vitabu hasa vya agano la kale (kutokukidhi canon ya palestina,kwa biblia ya kiebrania na canon ya aleksandria, kwa septuangita)
pia inazusha swali kwamba ni kwa nini vitabu vingine viliachwa havikujumuishwa ktk biblia ???
mpendwa kwanza kabisa napenda kukushauri kidogo jinsi ya kuisoma Biblia Takatifu.Kuna topic moja mtu aliuliza, kwa mapokeo, tunaambiwa yule Cain mtotowa Adam, alipofukuzwa Eden, aliondokana kuoa mbalihuko.
Sasa kama Adamndiye mtu wa kwanza, huko mbali alioa nani?
Wataalam wakawa na majibu mawili.
Moja wakasema alioa dada yake. Jibu hili linaelezea habari kwamba Adamna Hawa walikuwa na watoto tofauti.
Lakini halijitoshelezi, tunaambiwa Adamna Hawa na uzao wao walikuwa Eden, kama walikuwa na watoto wao kabla ya Cain kufukuzwa, hao wangekuwa Eden nao.
Hao watoto wao waliofika nje ya Eden bila kufukuzwa walikuwa nani? Wlaifikaje huko? Mbona habari zao za kufika huko hazikuandikwa?
Kukatolewa jibu la pili, la kisomi zaidi kuliko kimapokeo. Wanasosholojia wanasemakwamba waandishi wa Kiyahudiwameandika mambo kingano zaidi ya ukweli. Kwamba si ajabu kwa watu wa kabila moja, wanapoandika hadithi za mwanzo wa kabila lao, kuandika mwanzo wa kabila lao kama mwanzo wa watu wote, na si ajabu, katika enzi hizo, watu waliokaa pamoja waliwahesabu watu wengine wa mbali nao kwamba si watu kamili.
Kwa hivyo, kulikuwapo na watu kablaya Adam wanaishi sehemu nyingine mbaona uzao wa Adam, ila watu wa uzao wa Adam haukuwahesabu hawa watu kama watu kamili, na Cain alivyofukuzwa Eden akaenda kuoahuko.
Hili jibu la pili lilinifanya niseme kwamba, hizindizohabari ninazosema mara kwa mara hapa.
Kwamba, hivi vitabu ni mythologies, si fact, watu wengi wanavisoma kama fact.
Habari yenyewe imeandikwa kirefu zaidi hapa
https://www.biblicalarchaeology.org/daily/biblical-topics/hebrew-bible/who-was-the-wife-of-cain/
mpendwa hiyo bible ninaweza kupata hardcopy ?biblia ya NEW JERUSALEM TRANSLATIO
Mkuu kuhusu hilo swali lako nafkiri Biblia ilishasema watatokea manabii wa uongo hivyo sio kila tukisomacho, tukionacho na kukisikia ni ukweli hivyo ni heri tushike imani kuliko KITABU!! Mfano ukisoma biblia kuna incosistence nyingi ambayo labda ni makosa ya waandishi tu lakini unajiuliza kwanni Mungu ameruhusu watu wafanye makosa kwenye kitabu kinachoshikilia imani ya ukristo mifano iko mingi na inastahili uzi wake hivyo jibu ni kwamba Mungu karuhusu ila inatakiwa kabla hatujasoma mstari wowote basi tumuombe Mungu atufunulie tafsiri sahihi ya maandikoasante mkuu zitto junior kwa mada nzuri na yenye kufikirisha.
wazo langu nadhani kuendelea kujifunza haya mambo iya kiimani taratibu ili tusipotee moja kwa moja.
kwanza lazima tukubali kwa vyovyote vile alivyo Mungu yupo. na kama Mungu yupo, wapo na walikuwepo na watakuwepo wajumbe wake wakituelezea yanayo muhusu Mungu.
ila siku zote najiuliza na kukosa majibu kwamba kwanini baadhi ya habari za Mungu zimefichwa au zimepotoshwa na hali ya kua M ungu yupo na anaona mbali kuliko mwanadamu awae yote? je ni kwa ridhaa yake? au amekusudia jambo fulani ndio maana akaridhia hivyo?
kwa kua nilikosa jibu la maswali hayo basi nabakiwa na kile nilichofundishwa kwamba Hawa hakuzini na nyoka bali nyoka alimshawishi kula aina ya tunda la mti uliozuiliwa kuliwa matunda yake alipewa adhabu na kwa bahati mbaya mtoto wake wa kwanza alipata laana kutokana na makosa ya mama na baba yake .
TUOMBE UZIMA WA ROHO NA AFYA YA MWILIBila shaka uzi utakaofuata utazungumzia hoja uliyotaja hapo juu ili mje mtiririke na kutuongezea maarifa
Hapana mkuu ipo soft copy.... Hard copy sijafanikiwa kukutana nayompendwa hiyo bible ninaweza kupata hardcopy ?