Je, George Floyd ni mtume?

Je, George Floyd ni mtume?

Nawajua sana na katika hao watano hawa wapo.
Waislam wameambiwa katika kitabu chao kuwa wako wengi,wanne wamepewa vitabu wawaongoze binaadamu kutokana na Amri za Mungu

Mitume 125.wametajwa kwenye vitabu na wengine hawajulikani lakini wapo
 
Amufikishaje huo ujumbe ? Kwa ufupi umekosea kumlinganisha na mtume na hii imetokana na kutokuwa na maarifa ya kutosha juu ya utumd na mitume.
Sawa Mkuu, George ametumwa kujitolea muhanga Kama alivyojitolea muhanga Yesu,ili liwe fundisho kwa Binaadamu

Kifo George na Yesu hakina tafauti
 
Habari za mitandaoni Dunia nzima Ni kuhusu kifo cha Mmarekani Mweusi George Floyd.

Katika dini ya Kiislam Mitume iko mingi wengine wanajulikana na wengine hawajulikani. Kuna Mitume Kama 123 ambayo inajulikana, kuna Mitume inaliyopewa vitabu na isiyopewa vitabu.

Mitume inafanya kazi ya Mungu katika jamii iliyomzunguka au hata kuleta mabadiliko Dunia nzima. Yesu aka Issa aka Jesus kabadilisha Dunia, Muhamad kabadilisha Dunia, kuna akina Musa, Sulemani nk ambao wamebadilisha jamii zao.

Uonevu kwa watu weusi unaofanywa na Polisi katika nchi ya Marekani haujaanza leo. Kifo cha George Floyd kimeleta mtazamo mwengine katika vitendo vya uonevu vinavyofanywa na Polisi kwa watu weusi.

Hivi sasa dunia nzima, nchi za Ulaya, Marekani, Australia nk watu wanaandamna mbele ya balozi za Marekani kupinga unyanyasaji wa Polisi kwa watu weusi.

Katika Jimbo la California Polisi leo wameungana na waandamanaji kupinga vitendo vya unyanyasaji wa watu weusi. Cha kushangaza, wengi wa waandamanaji ni watu weupe; cha kushangaza zaidi, nchi za Kiafrika ambazo ni chimbuko la watu weusi hamna hata nchi moja watu wameandamana kupinga uonevu huo.

Donald Trump leo kalazimika kupelekwa kwenye handaki chini ya White House kwa usalama wake baada ya waandamanaji kuandamana mbele ya White House.

Jeshi limeingia mitaani kuungana na Polisi, kafuu ya kukataaa watu wasitoke majumbani mwao imewekwa nchi Marekani. Haijawahi kutokea, Marekani kama vile kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Je, George Floyd ni Mtume asiejulikana alietumwa na Mungu kuibadilisha mitazamo ya watu kuhusu mtu Mweusi nchini Marekani?
Mcheza picha za ngono hawezi kuwa mtume wa Mungu labda hizo dini mnazoanzisha za kujipatia kipato.
 
Mcheza picha za ngono hawezi kuwa mtume wa Mungu labda hizo dini mnazoanzisha za kujipatia kipato.
Hamna Kaka,sio.hivyo hao ni mawazo yako binafsi

Yesu hakuwahi kuowa, Muhamad kaowa zaidi ya wake kumi moja,aliwahi kuowa mtoto mdogo..

Kila Kitu kimeletwa na Mungu hapa Duniani,ila inategemea utakichukulia vipi

Kucheza filam za ngono haina tafauti na kucheza unyago katika baadhi ya Makabila hapa Tanzania

Madhumuni ya Unyago na Filam za Ngono ni kuielisha jamii kuhusu NGONO
 
Ila kusema ukweli ubaguzi unaofanyika huko majuu umenifanya niichukie hii tittle ya kujiita 'diaspora'. Bora tu kunyuti huku huku 'nyumbani' Africa, madiaspora mnisamehe.
mkataa kwako mtumwa hi kauli and ilikuwa na maana saana
 
1---Nani kakudanganya kwamba Mungu anaweza kufanya KITU CHOCHOTE hata cha kijinga ???

2--Nani kakudanganya kwamba Mungu anahitaji kutoa maisha ya Mtu (kafara) ili jambo fulani litimie??

3---Kama ni kafara je kwanini Mungu hakuwaambia mapema Yesu na Floyd kwamba angewatoa kafara kwa sababu fulani???

4---Mbona hao wote Yesu na Floyd walipokuwa wanatokewa hiyo unayoiita "kafara" walikuwa Wakilia kwa uchungu wa maumivu ya "kafara', Yesu alilia; Eloi Eloi lamasabachtan, na Floyd alilia; nashindwa kupumua.

5---Je ukiambiwa "kafara" hiyo unayoisifu ni ukatili dhidi ya binadamu utakataa??

6---Je, Kama ni kweli ni kafara kutoka kwa Mungu, watu wakisema Munguu ni katili watakuwa wamekosea ??? (Mungu hawezi kuwa katili aslan).

7---Je ungekuwa ni wewe, ungependa utolewe kafara kama huyo G, Floyd au Yesu???

8--- Je wale wanaotoa kafara kwa kuua watu kama Albino ili wapate dhahabu machimboni na utajiri wapo sahihi???

9--- Je watoto na ndugu na jamaa wa G. Floyd watakubaliana na wewe unaposema huyo mpendwa wao ni Mungu aliyemtoa kafara???

10---- Nabii Ibrahimu aliota anamchinja mwanaye wa pekee, na alipoamka asubuhi akataka kumchinja huyo mwanae kidhahiri lakini Mungu akamkataza na kumwambia achinje kondoo, kwa nini alimkataza na wakati huohuo, kwa mujibu wako, Yeye Mungu kamtoa kafara G. Floyd na Yesu "kafara" ??
Mungu ni Mjuzi wa kila Kitu,kila anachokifanya anakifanya kwa sababu zake wakati wake..

Kuna aliowambia amtoe kafara mtoto wake kwa kumchinja

Kuna aliwaweka msalabani

Kuna aljowazamisha baharini wakaliwa samaki

Kuna waliozalowa bila Mama

Kuna waliozalowa bila Baba

Kuna waliombwa kwa udongo no

Hakika Acha MUNGU aitwe MUNGU
 
Waislam wameambiwa katika kitabu chao kuwa wako wengi,wanne wamepewa vitabu wawaongoze binaadamu kutokana na Amri za Mungu

Mitume 125.wametajwa kwenye vitabu na wengine hawajulikani lakini wapo
Unaweza kuwataja hao mitume 125 au kutupa ushahidi tunapata wapi hiko ulichotuandikia ?

Kwahiyo tunakubaliana ya kuwa mtume lazima apewe muongozo, hasa kitabu ? Sasa huyu sasa huyu uliyemzungumzia mbona hana sifa zote hizi ?
 
Nachoona Floyd atazidi kuonyesha kuwa Lockdown kwa marekani sio muhimu tena hili swala likiisha watu hawata rudi ndani tena.
 
Sawa Mkuu, George ametumwa kujitolea muhanga Kama alivyojitolea muhanga Yesu,ili liwe fundisho kwa Binaadamu

Kifo George na Yesu hakina tafauti
Simchenzo hii kauli nawaachia wakristi wenyewe watakuja kukujibu. Ila kwetu sisi tunaamini hafanani kwa lolote na Mtume Issa isipokuwa tu waote ni binadadamu,na mtume Issa/Yesu kwa mujibu wetu sisi Waislamu ni kuwa hajafa wala hakusulubiwa.

Ahsante.
 
Hapana.
Kile kifo chake kinasikitisha.
Maana amewekewa GOTI shingoni.
Kifo chake kilikuwa ni hatua kwa hatua.
Huku analalamika 'SIWEZI KUPUMUA".
bora angepigwa risasi kidogo tungesema ni bahati mbaya lakini kifo chake kinaonyesha muuaji alidhamiria
 
Back
Top Bottom