Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,952
- 62,848
Ngoja nikunukuu,unasema hivi "Mungu alipo mwagiza Musa aandike mafundisho yake Mitume na Manabii wote waliofuatia walitii Agizo la Mungu la kuandika mafundisho ya vitabu vyote "Biblia ni Mafundisho ya Mungu yenye mtiririko tokea Totari hadi Injiri.
Ndio maana kikaunganishwa na kuitwa Biblia.
Mungu alipo mwagiza Musa aandike mafundisho yake Mitume na Manabii wote waliofuatia walitii Agizo la Mungu la kuandika mafundisho ya vitabu vyote vilivyofuatia.
Kuandika ni kutii maagizo ya Mungu kile alichomuaguza musa.
Ni kama hizi Amri hapa.
............
[emoji117]Kumbukumbu la Torati 5:6
Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
8 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini ya nchi.
9 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
10 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
11 Usilitaje bure Jina la Bwana, Mungu wako; maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia, mtu alitajaye jina lake bure.
12 Ishike siku ya Sabato uitakase, kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru.
13 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
14 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng'ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako ye yote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile vile kama wewe.
15 Nawe utakumbuka ya kuwa wewe ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, na ya kuwa Bwana, Mungu wako, alikutoa huko kwa mkono wenye nguvu, na mkono ulionyoshwa; kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wako, alikuamuru uishike sabato.
16 Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
17 Usiue.
18 Wala usizini.
19 Wala usiibe.
20 Wala usimshuhudie jirani yako uongo.
21 Wala usimtamani mke wa jirani yako; wala usiitamani nyumba ya jirani yako, wala shamba lake, wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala kitu cho chote alicho nacho jirani yako.
22 Haya ndiyo maneno ambayo Bwana aliwaambia mkutano wenu wote mlimani kwa sauti kuu toka kati ya moto, na wingu, na giza kuu; wala hakuongeza neno. [emoji117]Akayaandika juu ya mbao mbili za mawe, akanipa
................................................................
Hizi ni Amri Kumi za Mungu alizopewa Musa kwanda kuyafundisha watu wake, Mungu mwenyewe aliziandika na kumpa Musa.
Maagizo Mengine alimwambia Musa aandike.
Kutoka 17:14
Bwana akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.
Kutoka 24:4 Basi
Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli,
................................................................
{Hapa tunaona Mungu wa kwenye Biblia ndio Mwandishi Mkuu wa Mafundisho yake.
Musa alijifunza kwa Mungu wake kuandika.
Manabii na Mitume wengine walijifunza kwa Musa kuandika maagizo ya Mungu}
................................................................
Swali kwa Waislamu.
[emoji117]Ni wapi Allah karuhusu kuandika Maafundisho ya kwenye kitabu cha Qurani ?
Naomba Jibu, La sivyo ijulikane wazi kwamba
[emoji117]Kitabu cha Qurani ni Batili.
Sasa kumbe jibu unalo, na ndo maana na Qur'an iliandikwa na kuwekwa kwenye kitabu kwa sababu wewe mwenyewe hapo juu umeshakiri kuwa agizo la kuandika maneno ya Mungu lipo toka zamani kabla hata hiyo Qur'an haijafundishwa na Mungu.
Sasa ili hoja yako kuwa Qur'an haikuandikwa kwa agizo la Mungu iwe na maana basi labda lete andiko kutoka kwenye kitabu cha Mungu kuwa Mungu alifuta agizo la awali la manabii wanaofuata baada ya Musa linalowataka waandike maneno yake.
kama hilo agizo jipya halipo basi agizo la zamani liliendelea mpaka wakati wa Qur'an ilipokuja kwa sababu Qur'an ni maneno ya Mungu tena yasiyo na shaka ndani yake