(Mafundisho ya Biblia, katika Agano la Kale mengi yalikuwa ya nguvu na vitisho)
Ambapo Mungu alitaka kudhihirisha uwezo wake, kwakuwa baadhi ya Jamii hazikumwamini, ziliamini kuwa iko miungu yenye nguvu zaidi ya Mwenyezi Mungu.
Ndio maana Nabii Musa alishindana kufanya miujiza mikubwa na Manabii wa Miungu mingine na akawa mshindi)
(Nabii Eliya pia alishindanishwa na Manabii wa mungu Baali.)
(Mafundisho ya Agano la kale yalitumia Nguvu zinazoweza hata kuua watu wengi, Kifo ilichukuliwa kama Adhabu.)
Mwanzo 2:17
walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Mwanzo 20:7 Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao.
(Na adhabu ya kifo kubwa zaidi kuwahi kutolewa ni ile ya Ghalika Kuu. Chini ya Uongozi wa Nuhu )
Mwanzo 7:23
Kila kilicho hai juu ya uso wa nchi kikafutiliwa mbali tangu mwanadamu hata mnyama wa kufugwa, na kitambaacho, na ndege wa angani; vilifutiliwa mbali katika nchi, akabaki Nuhu tu, na hao walio pamoja naye katika safina.
(Mafundisho mengi yalikuwa ya ukali.)
Mambo ya Walawi 20:27
Tena mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu yao itakuwa juu yao.
Kutoka 21:24
jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
Kutoka 21:25
kuteketeza kwa kuteketeza, jeraha kwa jeraha, chubuko kwa ajili ya chubuko.
Mambo ya Walawi 24:16
Na yeye atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana atauawa.
Kumbukumbu la Torati 19:20
Na watakaosalia watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako.
Kumbukumbu la Torati 19:21
Wala jicho lako lisiwe na huruma; uzima kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.
(Amri zilikuwa kama hizi)
Mambo ya Walawi 20:2
Tena uwaambie wana wa Israeli, Mtu awaye yote miongoni mwa wana wa Israeli, au miongoni mwa wageni waketio katika Israeli, atakayetoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, sharti atauawa; wenyeji wa nchi watampiga kwa mawe.
Mambo ya Walawi 20:6
Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.
Mambo ya Walawi 20:8
Nanyi zishikeni sheria zangu, na kuzitenda; Mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi.
Mambo ya Walawi 20:9
Kwa maana kila mtu amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa, amemlaani baba yake na mama yake; damu yake itakuwa juu yake.
Mambo ya Walawi 20:10
Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.
Mambo ya Walawi 20:11
Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
Mambo ya Walawi 20:12
Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.
Mambo ya Walawi 20:13
Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
Mambo ya Walawi 20:14
Tena mtu mume akimwoa mke pamoja na mama yake, ni uovu mkuu; watachomwa moto, yeye mume na hao wanawake pia; ili kwamba usiwe uovu kati yenu.
Mambo ya Walawi 20:15
Tena mtu mume akilala na mnyama, hakika atauawa; nanyi mtamwua huyo mnyama.
Mambo ya Walawi 20:16
Tena mwanamke akimkaribia mnyama ye yote, na kulala pamoja naye, mtamwua huyo mwanamke, na mnyama pia; hakika watauawa; damu yao itakuwa ni juu yao.
Mambo ya Walawi 20:17
Tena mtu mume akimwoa umbu lake, binti ya baba yake, au binti ya mama yake, na kuuona utupu wake, na huyo mwanamke kauona utupu wake huyo mume; ni jambo la aibu; watakatiliwa mbali mbele ya macho ya wana wa watu wao; amefunua utupu wa umbu lake; naye atauchukua uovu wake.
Mambo ya Walawi 20:18
Tena mtu mume akilala na mwanamke aliye na ugonjwa wake, na kufunua utupu wake; amelifunua jito la damu yake, naye mwanamke amefunua jito la damu yake; wote wawili watakatiliwa mbali na watu wao.
(Hivyo Agano la Kale lilikuwa gumu kwa Watu. Mashoga, Wasagaji, Wazinzi wote ilikuwa ni Kuuawa.)
(Baada ya Mungu kudhihorisha Nguvu zake dhidi ya miungu wengine na kuambiwa na Mataifa, akaona ni vema kuondokana na misumali ya Agano la Kale.)
Yeremia 31:31
Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
Yeremia 31:32
Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
Yeremia 31:33
Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Yeremia 31:34
Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.
(Ambalo lilikamilishwa kwa Neno la Kristo Masihi {siyo Issa} Yesu wa Myahudi wa Nazareti)
Luka 22:19
Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
Luka 22:20
Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]
(Katika Agano Jipya ambalo Mungu amefanya na Wanadamu kama mfunulia Nabii wake Yeremia 31:3, hakuna tena Adhabu kali za kifo kutekelezwa na Binadamu hapa Duniani. Amri zote zilitangaza UPENDO)
Mathayo 22:34
Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja.
Mathayo 22:35
Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
Mathayo 22:36
Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
Mathayo 22:37
Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Mathayo 22:38
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
Mathayo 22:39
Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Mathayo 22:40
Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
( ambapo imesisitizwa kabisa)
Mathayo 5:43
Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
Mathayo 5:44
lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Mathayo 5:45
ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
Mathayo 5:46
Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
Mathayo 5:47
Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
Mathayo 5:48
Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
(Yale mambo ya Jino kwa Jino, Shoga auwawe, yalikoma hapo)
Mathayo 5:38
Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;
Mathayo 5:39
Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.
Mathayo 5:40
Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.
Mathayo 5:41 Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili.
Mathayo 5:42
Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
Mathayo 5:43
Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
Mathayo 5:44
lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Mathayo 5:45
ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
[emoji117]Sasa
[emoji523][emoji525]
Leo linapokuja fundisho tena la kumwua shoga, mchawi, mzinzi, anayemkufuru Mtume au Mungu.
Tunabaki kujiuliza,
Hili ni Agano Gani Tena ?
Mbona mambo ya Jino kwa Jino yalishapita katika Agano la Kale
[emoji848][emoji848][emoji848]....!
Naomba majibu Wajuzi,
Hili tena ni Agano gani ?
Na lilisemwa kwa Unabii upi ?
Na Lini ?