Hivi wewe unayebandika Bango linalosema.
"Wanawake Saba wa Yesu Kristo"
tukuchulie upo timamu kweli ?
Timamu ya kuuliza swali na kutaka kujibiwa ili uelewe jambo.
Kama Historia ya Yesu Kristo mnaichukua kwa Makuresh wa Saudi Arabia, badala ya kwake Israeli, mtawezaje kuchukuliwa kuwa ni watu wenye uelewa wa jambo hata dogo tu basi.
Mbona mnajitoa ufahamu kwa kiasi hicho ?
Tatizo nini hasa.
Majini au.
Huenda tatizo lilianzia hapa.
72:1 - Sema: Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini lilisikiliza, na likasema: Hakika sisi tumeisikia Qur'ani ya ajabu!
72:2 - Inaongoza kwenye uwongofu, kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu Mlezi.
72:3 - Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu Mlezi umetukuka kabisa; hana mke wala mwana.
72:4 - Na kwa hakika wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema uwongo ulio pindukia mipaka juu ya Mwenyezi Mungu.
72:5 - Nasi tulidhani kuwa watu na majini hawamzulii uwongo Mwenyezi Mungu
72:6 - Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi.
72:7 - Na kwa hakika wao walidhani, kama mlivyo dhani nyinyi, ya kuwa Mwenyezi Mungu hatamleta Mtume.
72:8 - Nasi tulizigusa mbingu, na tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na vimondo.
72:9 - Na hakika tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza; lakini sasa anaye taka kusikiliza atakuta kimondo kinamvizia!
Kama inafikia mahali mnayaamini Majini matokeo yake ndio hayo.