Mungu alipofanya Sample yake kwa Wana wa Israeli,
Alitumia Manabii wengi sana na waliandika vitabu vingi sana ambapo vipo katika kumbukumbu za vitabu vya
Torati
Zaburi
Manabii
Wafalme
Nakadhalika nakadhalika.
Watu wa Dini na Imani wakaanza kuvikusanya na kuviweka katika kitabu kimoja wakakiita Biblia.
Waroma wakachukua vitabu 72 nadhani.
Wapentekoste wakachukua vitabu 66
Wamomoni nao wakachukua vitabu wanavyopenda.
Ingawa maandiko yalipishana sehemu kadhaa chache lakini mambo ya msingi yalibaki kama yalivyo.
Kwa mfano
Amri kumi za Mungu ziko vile vile.
Zaburi iko vilevile katika vitabu vyote
Nakadhalika.
Againo la Kale lilikuwa maalum kwa Ajiri ya Watu wa Israeli.
Yaani liliwahusu wao tu.
Ndio maana katika hilo hilo Agano Mungu alisema hivi
" Yeremia 31:31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
Yeremia 31:32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
Yeremia 31:33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Yeremia 31:34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena."
Againo Jipya lenyewe ndo hili ambalo alikabidhiwa Yesu Kristo.
"Luka 22:14 Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.
Luka 22:15 Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;
Luka 22:16 kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.
Luka 22:17 Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;
Luka 22:18 Maana nawaambia ya kwamba tangu sasa sinywi mazao ya mzabibu hata ufalme wa Mungu utakapokuja.
Luka 22:19 Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
Luka 22:20
[emoji117] Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu."
Hivyo basi azma ya Mungu kuwaleta Neno lake kwa Binadamu wote lilitimia katika kuileta Injiri kwa watu wote.
Ndio mana Yesu alisema
(Enendeni ulimwenguni pote mkaihubiri Injiri kwa watu wote)
Kuhusu Amri kumi kwamba je zinatuhusu.
Amri kumi zilikuwa na mapungufu mengi sana.
Mfano, jirani tuliambiwa
Tusimwibie
Tusimwue
Tusitamani mali au mke wake
Tusizini naye
Tusimwambie uwongo.
Lakini kuna mambo zaidi ambayo jirani inabidi tusi mtendee.
Mfano vipi maswala ya kumpiga ngumi ya utosi bila kumwua, kumtemea mate je ?
Ndio maana Yesu katika Injiri akaleta Amri kuu mbili
1. Mpende sana Mungu
2. Mpende sana jirani.
Amri hizi mbili ndio Amri Kuu zina zina funika Amri Kumi.
Kuhusu vitabu kama vya Henoko, Barnaba nk.
Ni kwamba Biblia ambayo imekamilishwa na Injiri, huko nyuma vitabu vilikuwa vingi tu watu wakachagua kutokana na mitazamo yao.
Mfano Wapentekoste wamekiondoa kitabu cha Yoshua Bin Sira kwakuwa Sira ameruhusi kunywa pombe kwa kiasi.
Waroma wanakunywa Uransi kidogo ndio maana wamekichukua.
Vilevile vitabu vingine.
Naskia Waislamu wanakikubali kitabu cha
Injiri ya Barnaba.[emoji16][emoji16][emoji16] lakini sijui kwanini hawaja kijumuisha ktk Qurani.
Lengo la sasa hivi ni kuisikia Injiri yaani Agano Jipya na kutenda kama alivyo agiza Yesu Kristo.
Na Wataalamu wa teolojia, wamejitahidi kuichukua Injiri kama ilivyo.
Ziko tofauti ndogo tu kwenye lugha
Mfano neno
(Kuokoka) Waroma wanaandika (Kusalimika)
Lengo likibaki lilelile.
Mambo ya msingi kama
Kubatiza,
Kukiri Yesu Kristo ni Bwana na Mwokozi
Linabaki pale pale.
Sasa kuhusu ukweli wa Biblia ipi inategemea wewe unamsimamo gani
Unahitaji mafundisho ya Yoshua Bin Sira au la.
[emoji847] Nawasilisha kwa kurekebishwa