Je, baada ya James Rugemalira wa IPTL kuachiwa huru, nini hatma ya majizi waliotajwa bungeni na Mh. Tundu Lissu?

Mkapa aliiba mamilioni, akaja Kikwete akaiba mabilioni, akaingia dhalimu mwandakuzimu akaiba matrilioni sijui anayefuatia ataiba ngapi...maquadrilioni? Yupi kati ya hao wote hakusukumiziwa madaraka na chama king'ang'anizi kilichochoka CCM? Halafu tunashangaa kwa nini nchi masikini! Kweli adui wa taifa hili ni CCM.
 
Unacho shangaa ni kipi !!?
Magu aliwaweka ndani majizi mkapinga kweli kwa kumuita dikteta.....
Amekufa leo mafisadi yanatoka yaanze kutamba unashangaa!!!
Dhalimu mwendakuzimu mwenyewe aliiba hadi akapigwa stop na corona au huna habari?
 
Kupambana na ufisadi chini ya CCM ni kujilisha upepo maana uongozi ndani ya chama unatoka na na rushwa na hivo viongozi wake ni zao la rushwa Sasa hapo ni ujinga kiamini CCM inaweza pambana na ufisadi .Sulihisho ni kuwatoa madarakani
 
Kumbuka hakushinda kesi bali imefutwa na Jamhuri
 
Hakika sema wadanganyika wengi bado hawajajua hii siri

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
 
Povu hizi zinadhihirisha kauli ya jamaa kwamba ADUI namba Moja wa Tz ni CCCM ...Nchi hii siinaongozwa na cccm

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
 
Unatakiwa upigie mstari: 'ADUI MKUBWA WA NCHI HII NI CCM'.
 
Tunasema ni CCM maana waliovuta mgao ni wana CCM na hawajaguswa mpaka leo. Imagine Mbowe angepewa hata laki 1 na Seth hivi asingekua amenyongwa? Hakuna kesi ya ufisadi nchi hii ambao mwanasiasa wa CCM ataburuzwa kortini tuliona hilo kwenye makinikia,EGMA,Escrow,lugumi, Kashfa ya Lugola na tenda hewa na hta huyo JPM hakufanya lolote kuwakamata.

CCM ni ileile ndio maana wanalindana
 
Tanesco walipaswa kumlipa ile pesa lakini siyo yote.

Utaratibu uliotumika kuzitoa pesa haukufuata taratibu.

Pesa ya serikali ikiwemo kodi baada ya mauzo ya hisa haikukatwa n.k

So pesa zilikua na ufisadi na ndio maana mgao ulitembea.

Ambacho wapinzani akiwemo Lissu walipinga ni kuwakamata Seth na Ruge huku wahusika wengine walio facilitate hili dili upande wa serikali/CCM wakiacha kushtakiwa.

So ilionekana kama wamewatoa kafara hawa jamaa ili kuisafisha serikali ilihali kina Ngeleja na Chenge waliohusika 100% wakiendelea kupeta bungeni.

Bila kukamata majizi yaliyopo CCM vita ya ufisadi ni maigizo tu
 

Msomeni Lema, “I can imagine then joy of the family”!
Mambo ni mengi muda ni mchache!

Ninamalizia, “I can imagine those billions of escrow could have saved many lives and brought so much joy to many poor families”!
 
Naamini wewe kidogo ubongo unafanyakazi! Hoja yangu ni kuwa, mwanaCCM anapofisadi na tukamjumisha katika CCM wote baadala ya kumsingoauti huyo fisadi, basi hoja huwa imeisha nguvu. Napendelea kupambana na fisadi kama fisadi mwenyewe baadala ya kumficha fisadi katika kivuli cha chama cha siasa. Chama cha siasa hakiwezi kuwa fisadi bali mwanachama mmoja mmoja.

Hapa JF ni mabingwa wa kuua hoja za ufisadi kwa kuwabandika mafisadi katika vyama vyao. Huu ni ujuha. Mfano CCM haikumtuma JK afisadi hela za escrow! Hivyo JK ahukumiwe kama yeye si ccm nzima. Kama Mbowe aligaidi kama wanavyosema waliomshitaki, hii isiunganishwe na chadema maana hata ikiwa ni kweli, siamini atakuwa ametumwa na chama.

Kwa kuhitimisha tunatakiwa kusema adui wa nchi hii ni baadhi ya Viongozi wa CCM na si kusema adui ni CCM.
 
Hivi si kuna kiasi fulani cha pesa ukipewa kama zawadi unatakiwa kuijulisha serikali, nayo inachukua kodi yake. Si kuna utaratibu huo?

Sasa wote wale waliogawiwa mabilioni itakuwaje?
 
Hao sio majizi, karma imeisha washughulikia karibu wahusika wakuu wote na waliobakia, itamalizana nao!.
Escrow haukuwa wizi.
P
 
Magufuli alikuwa mwana wa Tanzania,dhamira yake ilikuwa njema sana,ipo siku yule Fatma Karume atapigwa risasi hadharani
Mnahubiri Upuuzi Kama huu!!awe na Dhamira njema apige watu Risasi !!!! Awe na dhamira njema aibe pesa afiche Seychelse au awe na dhamira njema aweke wanyarwanda 245 kwenye system? Kisa ni damu inayogusana na yake ? Awe na dhamira njema amuue Ben saa nane Kwa kummezesha Chatu? Tuwe wakweli bwana
 
Huijui serikal wewe...yaan katoka kwa kudra halaf aje aishitak wakat wamemwonya kabisa..tunakutoa lakin marufuk kuisema vbaya serikal ama kufungua kesi ya madai...weee acha kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…