Kaka situation yako inasikitisha.
Mwanamke akiwa mwenyewe anapata sana vishawishi. Ex-boyfriends, mabosi etc.
Ila mwanamke anaweza kumudu hali hii iwapo TU, anampenda kwa DHATI mpenzi wake. Hii hata iweje piga ua msichana ataendelea kusubiri TU.
Kama sivyo basi kama ana marafiki wa kike wanaweza kumuinfluence na matokeo yake akakutana na njemba zikachukua kimoja.
Social networks zinaongoza kwa kutongozwa wanawake. FACEBOOK!!
Ila pia hata wewe ulipo huko unaweza kushawishika kumuacha solemba mwenzi wako. Group discussion na akina dada usiku hatari sana.
CHA KUFANYA
Sijui mpenzi wako mnaishi vipi kwenye ukweli, uwazi na mawasiliano ila nakushauri yafuatayo:
1. Mpenzi wako asiwe kabisa FACEBOOK
2. Mawasiliano kati ya wewe na mpenzi wako yawe ni ya kila saa/kila baada ya muda/kila siku. Hakuna ubusy kwenye mawasiliano. Mimi hapa nilipo ungejua niko wapi lakini nawasiliana na mke wangu KILA wakati. Kwa siku mara 50+ labda.
3. Mkeep busy awe anawasiliana na ndugu zako, dada, mama, kaka, shangazi, etc. Maana umesema ilikuwa mfunge ndoa so anafahamika
4. Jaribu pia kufahamu muda gani anakuwa free/fahamu ratiba yake(nadhani unafahamu). Mfano kama anafanya kazi unajua kabisa kuanzia labda saa mbili mpaka muda fulani(lunch) atakuwa busy. Unaweza kumtumia message moja mbili ukamuacha aendeleze taifa. Unafahamu anarudi saa ngapi, anarudi na usafiri gani etc. Kama ilikuwa karibu mfunge ndoa vyote hivi unafahamu
5. Punguza wivu utadata. Kuwa na wasiwasi tu iwapo unaona si kawaida kutowasiliana nawe. Jaribu kuwaza labda simu kwenye charge au chochote kingine. Wanawake si rahisi kucheat kama wako IN LOVE
6. Mpe majukumu mengine labda kufuatilia harusi fulani, kiwanja, biashara etc.
7. HAKIKISHA kutokuwepo kwako inakuwa ni PHYSICAL TU ila MENTALLY uko nae. Unajua amekula nini, amevaa nini amefika kazini saa ngapi, amekutana na challenges gani. Pia na wewe share nae unayojifunza.
8. Si vibaya ukijitutumua ukamtumia kinauli akaja kukutembelea au wewe ukarudi likizo. Miaka miwili ni mingi ingawa narudia tena kama ANAKUPENDA ATASUBIRI TU.
Yako mengi sana sana sana ila mimi ninajitahidi kudeal na long distance relationship na honestly namshukuru Mungu naimudu.