Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Pasco tafadhali tudadavulie kidogo hapa.
Uhaini ulipangwa 1982, home kwetu ni Drive-in Estate, nyumba yetu na nyumba ya Banyikwa ziliuwa zimeungana tukitenganishwa na ukuta. Hapo ndipo ilipokuwa ikifanyika mikutano ya kupanga mambo!. PW No. 1 ni Hope Banyikwa, ambaye ndie binti mkubwa wa familia ya Banyikwa, hawa walikuwa ni Wahangaza, hao mabinti!, usipime!.

Kesi ilivyoanza, ilikuwa na washtakiwa 46. Wote walishikiliwa Ukonga Maximum Prison, Kiongozi mkuu wa mpango huo ni komandoo wa JWTZ aliyeasi, Martin Tamimu aliyeelezewa kuwa ni mtu hatari sana na hashikiki kirahisi, hivyo wakati wa arrest vijana walipewa special instructions, hivyo askari 8 na magari 4 yalimzingira nyumba aliyokuwepo kwa kimada wake Kinondoni Mkwajuni, walipojiririsha yuko ndani ya "game", waliivamia nyumba!, alichomoka bila shati na kuchumpa darini!, jamaa kuingia ndani hayupo!. Huyo demu akawaelekeza askari kwa ishara, wakaizunguka nyumba, ile wanaanza tuu kumpandia, alitobokea kwenye siling board ya bafu la nje na kuruka ukuta hadi upande wa pili, kumbe nako kuna gari la "jamaa", wakamkimbiza, akarukia pick up iliyokuwa inakwenda race,"jamaa" wakaifuata ile pick -up ay very close range, wakamiminia za kutosha na kumaliza kazi!.

Baada ya sterling kuuwawa, Thomas Lugangira "Father Tom" au "Uncle Tom" ndiye alikuwa mshatakiwa wa kwanza Hatibu Macghee wa pili na wenzao 19.

Nitaendelea.

Pasco.
 
ww ndio umetoka nje ya Mada kabisa
Nani kasema Hans Pope ana biashara ya Malori?
Yeye ni Kiongozi wa Chama cha wenye malori Katibu wake akiwa Mtoto wa Lukumay
Huyo Lukumay na Lowassa unajua wana nasaba gani
Zacharia hawezi kuwa na idadi ya MaTank km Kobil, Premus, OilCom na hata yale ya Ridhiwan
Huyo Jamaa yako ni chambo tu hana biashara huko ni M/kiti tu

Sawa nakubali, Zakaria yupo katika hiyo picha lakini haina maana kuwa anafanya biashara na hao Mafisadi [RIdhwani etc.] isipokuwa kwa vile wote ni wasafirishaji wa mafuta bila shaka wana ushirikiano kupitia chama chao ambamo yeye Zakaria ni kiongozi mkuu!!! Nasisitiza kuwa Zakaria Hans Pope hana ubia wa biashara na wakina Lowassa.
 
Mbona umemtaja hans pop tu wengine huwajui eeh??? Ngoja nikutajie wengine sasa. KAPTEN EUGEN MAGANGA, KADEGO, MAGII, NA KUNA MMOJA ALIKIMBILIA UINGEREZA jina lake limenitoka kidogo. Kapten eugene maganga tumemzika mwaka juzi kijijini ITAGA MKOA WA TABORA alikua anasumbuliwa na kisukari aliacha watoto wawili ote wa kiume mmoja anaitwa MICKEY EUGEN MAGANGA na RAYMOND EUGEN MAGANGA ndio mimi nilieandika maneno haya. R.I.P EUGEN MAGANGA
 
msukuma unayemsema alikuwa anaitwa suleiman matusela kamando..alisamehewa na ameshafariki...aliyetorokea kenya na Uk ni Lugangira..ameshafariki....alitokoroka na ex -pilot/comandoo akitwa Hatii maghee-alishikwa na kurudishwa keko.wengine pia walisamehewa na wameshafariki....pope alikuwa kikosi cha mizinga na kaka yake alikuwa Rubani Airwing.....issue ilitisha sana na kesi yake pia ikiwapa umaarufu wanasheria na ma lawyers...mageuzi ya meanza siku nyingi....
 
Jamani mimi bado narudia OMBI langu hivi kweli hakuna waandishi wa Kitanzania wanaoweza kuandika huu mkasa wa akina Hans Poppe ili kuweka KWANZA kumbukumbu na PILI ili vizazi vijavyo viweze kujifunza kutokana na tukio hili.

Tunataka mzungu aje kutoka ULAYA atuandikie hii party ya history ya nchi yetu apate PhD yake. Halafu "makanjanja" (SIC!) wetu waishie kutafasiri kazi hiyo ya mzungu kwa lugha ya kiswahili!?.

Mbona Wamarekani wameandika vitabu vingi tu kuhusu assassination Kennedy, sembuse hii a failed coup! Waandishi wa Tanzania amkeni jamani.

kama kuna mwana JF yeyote anayefahamu wapi naweza kupata hiki kisa cha akina Hans Poppe naomba anifahamishe. Niko interested kujua ALPHA and OMEGA ya hilo jaribio la mapinduzi. Kisa kizima na wahusika wake.
 
Uhaini ulipangwa 1982, home kwetu ni Drive-in Estate, nyumba yetu na nyumba ya Banyikwa ziliuwa zimeungana tukitenganishwa na ukuta. Hapo ndipo ilipokuwa ikifanyika mikutano ya kupanga mambo!

Habari hizo zilivuja mapema na zilivujishwa na Vijana waliokuwa wakilima michicha na kumwagilia michicha pale mbele ya Flat za Drive INN na Mzee mmoja aliyekuwa akichoma mahindi karibu na nyumbani kwa walikokuwa wakikaa Akina Hans Pope maeneo ya karibu na Highlands Cinema Iringa waliripoti juu ya pilikapilika fulani zisizoeleweka wakachoma utambi!Wanaume wakaanza kujipanga

Na nadhani kuna vitu hawakuvijua vizuri kuhusu hizo flat za Drive Inn!!!

Fungakazi ilikuwa lile eneo la Msasani bonde la Mpunga karibu na mradi wa chumvi ulipokuwepo ambako wafanya mapinduzi walitaka kuangalia na kuweka vifaa vyao vya kumtandika nyerere katikati ya magugu maji ili wamrarue akienda nyumbani au akienda ofisini.Hawakujua kuwa lile pori la magugu maji wamakonde walikuwa wakitumia kucheza watoto wao wa kike na KUlikuwa na wanaume wa kimakonde waliOkuwa wakikaa juu ya magorofa yasiyoisha kuangalia eneo lile na kufukuza watu wasisogee eneo la mambo yao.Walipowaona wanaangalia karavati na kuzunguka zunguka eneo lile wakawaripoti kuhusu pilika zisizo za kawaida mitego ikaanza kuwekwa taratibu.
 
Magazeti ya Rai enzi zile walikuwa na makala kibao kuhusu haya mapinduzi.Yalishaandikwa sana sema labda ni bwamdogo flani.

Jamani mimi bado narudia OMBI langu hivi kweli hakuna waandishi wa Kitanzania wanaoweza kuandika huu mkasa wa akina Hans Poppe ili kuweka KWANZA kumbukumbu na PILI ili vizazi vijavyo viweze kujifunza kutokana na tukio hili.

Tunataka mzungu aje kutoka ULAYA atuandikie hii party ya history ya nchi yetu apate PhD yake. Halafu "makanjanja" (SIC!) wetu waishie kutafasiri kazi hiyo ya mzungu kwa lugha ya kiswahili!?.

Mbona Wamarekani wameandika vitabu vingi tu kuhusu assassination Kennedy, sembuse hii a failed coup! Waandishi wa Tanzania amkeni jamani.

kama kuna mwana JF yeyote anayefahamu wapi naweza kupata hiki kisa cha akina Hans Poppe naomba anifahamishe. Niko interested kujua ALPHA and OMEGA ya hilo jaribio la mapinduzi. Kisa kizima na wahusika wake.
 
msukuma unayemsema alikuwa anaitwa suleiman matusela kamando..alisamehewa na ameshafariki...aliyetorokea kenya na Uk ni Lugangira..ameshafariki....alitokoroka na ex -pilot/comandoo akitwa Hatii maghee-alishikwa na kurudishwa keko.wengine pia walisamehewa na wameshafariki....pope alikuwa kikosi cha mizinga na kaka yake alikuwa Rubani Airwing.....issue ilitisha sana na kesi yake pia ikiwapa umaarufu wanasheria na ma lawyers...mageuzi ya meanza siku nyingi....

Nyerere huwa sielewi kwa nini alikuwa mtu wa kusamehe sana waliokuwa wakitaka kumpindua! yaani nasikia kuna askari moja alisema Kambona lazima niende uingereza nikamwue utake usitake wakati ule Nyerere anasumbuliwa na mpaka wa Malawi na Kambona Mnyasa koko anaendelea na harakati za kutaka kumpindua nYerere Uingereza.

Alichofanya Nyerere alimwambia nimekwambia nimemsamehe usimwue Kambona. Alipoona kapania Akamtoa jeshini akampeleka uraiani kushika vyeo vya kisiasa na akampiga marufuku ya kusafiri nje ya nchi!

Kuna wakati huwa nadhani Nyerere alikuwa mkatoliki mno angekuwa mwingine au angeua hadi basi!
Nyerere uwezo wa kusamehe unashinda hata wa Mandela.
 
Eugene Maganga alitoa simulizi hiyo katika gazeti la Rai, bila shaka ilikuwa miaka ya Tisini au mwanzoni mwa miaka ya 2000. Binafsi nimeshajaribu sana kuitafuta softcopy ya simulizi ile ila sijafanikiwa. Eugene Maganga alikuwa na mpango wa kutoa kitabu cha stori hiyo ila mauti yalimkuta akiwa bado hajatimiza nia yake. Labda akina Jenerali Ulimwengu wanaweza kuipata hiyo stori kwenye archive zao!

Nilisoma makala hio miaka ya 2000 mwanzoni nadhani kama sio mwishoni mwa miaka ya tisini....mwaka jana nilienda habari coorperation kuulizia kama naweza kupata makala hizo, cha kushangaza wakaniambia niende maktaba ya taifa huwa wanaweka kumbukumbu za magazeti....sikuwa na muda so sikufuatilia zaidi.
 
This is a smart chap and hard working person. He has got big influential power that is why he survives in the business and thrives as well. Probably he is still connected to the system he tried to turn against during Nyerere's time. Who knows?
 
Unadhani aliamka tu asubuhi akaorganise wenzake wakampindue Rais bila kuwa na back-up ya wanasiasa na wafanyabiashara nyuma yake? Ana bahati lile jaribio walilifanya kwa Nyerere, ungekua utawala wa nchi nyingine hizi za kiafrika hata mahakamani kesi zao zisingeenda!

Zacharia Hans Poppe, ambaye alizaliwa mwaka 1956 mjini Dar es Salaam na kukulia mkoani Iringa.

Baada ya kumaliza elimu ya sekondari, Zacharia alijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ambako alifikia cheo cha Kapteni, kabla ya kuachishwa kazi na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela, kwa tuhuma za uhaini, dhidi ya serikali ya awamu ya kwanza, ya hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwaka 1983.

Lakini mwaka 1995, Zacharia aliachiwa huru kwa msamaha wa rais wa awamu ya pili, Alhaj Ally Hassan Mwinyi, mwezi mmoja kabla hajamuachia Ikulu ya Tanzania, Benjamin William Mkapa, rais wa awamu ya tatu.

Kama zinavyosema sheria za nchi, mtu aliyehukumiwa kifungo, hana haki ya kugombea wadhifa wowote au kuajiriwa tena, Zacharia naye hakuweza kurejea kazini, badala yake akaamua kujiajiri, kwa kuanzisha miradi yake mwenyewe, ambayo leo ikiwa ni miaka 17 baadaye, miradi hiyo imesimama imara.

Kwangu mimi namuona shujaa si kwasababu ya kutaka kumpindua nyerere bali pamoja na kupotezewa muda mwingi akiwa gerezani lakini ameibuka na kuwa mmoja wa matajiri na mfanya biashara mkubwa nchini,ikumbukwe baba yake mzazi aliuwa na iddi amini kipindi kile cha vita ya kagera
.
 
Baadhi wanaojua vzr hii stori wanakuja kubeep then wanakimbia!
cc;Pasco,The East africa Eagle,
 
Zakaria Hans pope alikuwa kwenye mizinga yeye alipangwa kupiga mizinga msasani kwa mwalimu endapo mapinduzi yangefanikiwa!
 
Habari hizo zilivuja mapema na zilivujishwa na Vijana waliokuwa wakilima michicha na kumwagilia michicha pale mbele ya Flat za Drive INN na Mzee mmoja aliyekuwa akichoma mahindi karibu na nyumbani kwa walikokuwa wakikaa Akina Hans Pope maeneo ya karibu na Highlands Cinema Iringa waliripoti juu ya pilikapilika fulani zisizoeleweka wakachoma utambi!Wanaume wakaanza kujipanga

Na nadhani kuna vitu hawakuvijua vizuri kuhusu hizo flat za Drive Inn!!!

Fungakazi ilikuwa lile eneo la Msasani bonde la Mpunga karibu na mradi wa chumvi ulipokuwepo ambako wafanya mapinduzi walitaka kuangalia na kuweka vifaa vyao vya kumtandika nyerere katikati ya magugu maji ili wamrarue akienda nyumbani au akienda ofisini.Hawakujua kuwa lile pori la magugu maji wamakonde walikuwa wakitumia kucheza watoto wao wa kike na KUlikuwa na wanaume wa kimakonde waliOkuwa wakikaa juu ya magorofa yasiyoisha kuangalia eneo lile na kufukuza watu wasisogee eneo la mambo yao.Walipowaona wanaangalia karavati na kuzunguka zunguka eneo lile wakawaripoti kuhusu pilika zisizo za kawaida mitego ikaanza kuwekwa taratibu.

Kweli Kabisa kwa sie wazamani pale msasani bonde la mpunga walipojenga May Fair plazza walikuwa wanavuna chumvi pale miaka ya 70's.
 
Kama kuna mwandishi atataka kuandika Kuhusu kadhia hii amtafute Balozi Augstin Mahiga wakati ule alikuwa mkurugenzi wa Usalama wa Taifa anaijua movie yote mwanzo mpaka mwisho.
 
Back
Top Bottom