Japo Uchaguzi wa 2020 ni Uchaguzi halali, Ushindi wa Kishindo wa CCM ni halali? Wapinzani ni Wameshindwa Kihalali au Wamedhulumiwa kwa Figisu?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,
Kwa maslahi ya taifa, leo naomba kuendesha somo kuhusu kitu kinachoitwa ubatili na haramu.

Ubatili ni kitu ama kilichofanyika kinyume cha sheria, taratibu na kanuni hivyo jambo likifanyika kwa ubatili jambo hilo linakuwa ni batili.

Haramu ni jambo ambalo limefanyika kinyume cha imani na sio lazima iwe ni kinyume cha sheria.

Huu ubatili na uharamu unafanyika katika nyanja nyingi za maisha yetu, kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Sasa ili batili iwe ni batili kweli, lazima batili hiyo ibatilishwe, batili isipobatilishwa inakuwa ni halali!. Vivyo hivyo kwa haramu, ili jambo fulani kuwa ni haramu, lazima haramu hiyo iharimishwe, haramu isipoharimishwa inakuwa ni halali.

Mada kuu ya bandiko hili ni maswali kuhusu uchaguzi mkuu uliopita wa 2020, kuna watu mpaka leo zaidi ya miaka miwili imepita, bado hawataki kukunali matokeo, bado wanaamini uchaguzi ule haukua huru na wa haki hivyo kwao matokeo ya uchaguzi huo sio halali na wengine hata kuuita ulikuwa sio uchaguzi bali ni uchafuzi na matokeo yake ni haramu, hivyo kuendelea kususa hadi leo, hawayatambui matokeo, hawamtambui rais, hawalitambui Bunge hadi kususia nafasi za viti maalum!, hivyo nina viswali kidogo kwako, kuwa japo uchaguzi wa 2020 ni Uchaguzi halali, kwa kanuni ya "the end justifys the means", aliyetangazwa mshindi ndie mshindi halali, jee ushindi wa kishindo wa CCM wa kukomba kila kitu ni ushindi halali au batili na haramu?. Wapinzani ni wameshindwa kihalali kwa kukataliwa na wananchi au ni wameshindwa kwa kudhulumiwa na kufanyiwa Figisu hivyo kushindwa kwao sio halali ni wameshindishwa kwa ubatili na haramu?.

Naomba kukiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili baada ya kusoma hoja hii ya mwana jf huyu
Pascal ana shida sana kuhalalisha haramu kuwa halali.
Mkuu WALOLA VUNZYA kwanza naomba kukiri post yako hii imenimotivate kupandisha bandiko linalojitemea, thanks for motivation.

Ili jambo lolote haramu liwe ni haramu kweli ni lazima liharimishwe, ukifanya jambo la haramu, lisipo harimishwa linakuwa ni halali, yaani kitendo cha kutoiharimisha haramu yoyote, kunakuwa ni kuihalalisha hiyo haramu inakuwa halali mpaka pale yule YEYE anapoingilia kati kwa karma ama kuibatilisha haramu hiyo ama kuiacha na hivyo kuibariki.

Kwa vile issues zs uhalali na uharamu ni issues ngumu kueleweka kirahisi, naomba nifungie darasa kabisa niwapige shule kwa kutoa mifano ila pia kwa vile humu tuna simple readers na deep readers, simple readers hawataki vitu virefu, wanataka vitu short, simple and clear, hawa wanaweza kuishia hapa na ku jump kwenye conclusion, wale ma deep readers, tuendelee.
Mfano wa Nyama Halal na Haramu
Ndugu zetu Waislamu wanapaswa kula nyama halal ambayo mnyama amechinjwa kwa Kiislam kwa kutazamishwa kibla, ukila nyama ambayo haikuchinjwa Kiislamu ni haramu. Nchi nyingi za Afrika Tanzania tukiwemo hili tunaliheshimu, hivyo wachinjaji katika machinjio zote ni Waislamu na nyama zote za public inchini Tanzania ni halal. Mtu ukiwa na sherehe yako, ukajochinjia utakavyo, Waislamu wakala, wanakuwa wamekula haramu!, lakini kwasababu hakuna mtu yoyote aliyeuliza kama hiyo nyama ni halal, hao Waislamu wote waliokula haramu hiyo, bila kujua ni haramu, wanakuwa wamekula halal!.

Muislamu Kula Kitimoto Bila Kujua, Sio Haramu!
Nyama ya mkuu wa meza, kitimoto ni haramu tena sio kwa Waislamu tuu, hata kwa Wakristo, kitimoto ni haramu na kwenye Biblia imeharimishwa!. Ukifanya sherehe ukaweka kitimoto bila kusema ni kitimoto, Waislamu wakala bila kujua wamekula kitimoto, then wanakuwa wamekula haramu, ila kwa vile hawakujua ile ni haramu, wanajihesabu wamekula halali!, kitendo cha kutokujua kuwa nyama hiyo ni haranu, kunaihalalisha haramu ile kuwa halali!.

Kubakwa na Kunyamaza ni Kuridhia Ubakwaji!.
Kubaka ni kosa kubwa la jinai na adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela. Mwanamke akibakwa, asiposema kuwa amebakwa, kile kitendo cha kunyamazia kubakwa ni kuuhalalisha ubakaji ule na kuufanya kuonekana ni consensus hivyo ni tendo halali.

Mfano wa Ndoa Halalu, Ndoa Batili na Ndoa Batilifu.
Ndoa ni mahusiano ya mume na mke. Uhalali wa ndoa sio ile shahada ya ndoa au cheti cha ndoa, ni lile tendo la ndoa, liitwalo consumation, ambapo uhalali huo hupatikana by perfomance ya lile tendo!.

Wanandoa baada ya kufunga ndoa ya kidini Kanisani, au Msikitini, ndoa ya kiserikali kwa DC au ndoa ya kimila kwa Mwenyekiti wa Kijiji, na kukabidhiwa cheti chenu cha ndoa au shahada ya ndoa, uhalali wa ndoa hiyo hupatikana kwa consumation.

Ukitokea wanandoa hao wameshindwa kufanya lile tendo kwa sababu yoyote, then, ndoa hiyo inakuwa ni ndoa batilifu, na itakiwa ndoa halali baada ya perfomance kufanyika.

Ikitokea tendo limeshindikana kabisa kufanyika, then ndoa hiyo inakuwa ni ndia batili ila vile vyeti vya ndoa ni vyeti halali na ndoa hiyo itahesabika ni ndoa halili hadi mwandoa mmoja atakapo toa siri kuwa hakuna performance, na kuiomba mahakama kuibatilisha. Hivyo ndoa batili isipobatilishwa itaendelea kuwa ni ndoa halali!.

Mfano wa Mkataba na makubaliano Halali, Batili na Batilifu.
Mikataba na makubaliano, yaani contracts na agreements iko kama ndoa, kuna mikataba halali, batili na batilifu, void contracts na voidable

Kwanza sio kila makubaliano ni mkataba, ila kila mkataba ni makubaliano!. Yaani not every agreement is contract, but every contract is agreement.

Tofauti ya contact na agreement, contract no kisheria zaidi na agreements ni makubaliano tuu ambayo sio lazima yawe ya kisheria.

Mfano mzuri ni makubaliano ya muungano, artcles of union, zina kipengele cha muungano kuridhiwa pande zote. Tulipoungana ile April 26 1964 muungano ule ulipaswa uridhiwe na ma Bunge ya pande zote, kwa a process inayoitwa ratification. Kwenye muungano wetu ni Bunge tuu la Tanganyika ndilo liliridhia na kutunga sheria ya muungano, lakini kwa Zanzibar ratification haikufanyika, bali Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliwaita mabalozi na kuwaeleza Zanzibar imeridhia!. Hivyo makubaliano ya muungano yalikuwa ni voidable, na yalihalalishwa by perfomance ya utekelezaji wa vifungu vya mkataba. Kwasababu hakuna yeyote aliyelalamika rasmi popote, Muungano wetu ni halali licha ya Zanzibar kutoridhia kwa ratification.

Mfano wa Kufuta Uchaguzi Zanzibar ile 2015 ni Haramu ila Uchaguzi wa Marudio ni Halali
Kitendo cha Mwenyekiti wa ZEC kufuta matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar ile 2015, kitendo kile ni haramu na kufuta kule no batili kwasababu Jecha hakuwa na mamkaka ya yeye kujigeuza ZEC!. Ili haramu iwe ni harami, haramu hiyo lazima iharimishwe na batili hiyo ni lazima ibatilishwe!. Kwa vile hakuna yeyote aliyepinga rasmi haramu ile na kuibadilisha batili ile, then iligeuka halali hivyo uchaguzi wa marudio ilikuwa halali!. Haramu isipiharimishwa, na Batili isipo batilishwa, hugeuka halali Zanzibar Issue: Kwanini watu wanapiga kelele tu bila kuchukua hatua zozote na Kuna haja ya kuhofia kurudiwa Uchaguzi Zanzibar?
.
Conclusion
Vivyo hivyo kwa haramu ya demokrasia na ubakwaji wa demokrasia, ili haramu iwe ni haramu kweli lazima haramu hiyo iharimishwe, haramu isipoharimishwa, na batili isipo batilishwa inageuka halal!.

Swali la kujiuliza kuhusu uchaguzi wa 2020 jee kuna mgombea yoyote aliyelalamika rasmi popote kuhusu uchaguzi huo?. Jibu ni hakuna!. Hivyo kwasababu hakuna mtu yoyote aliyelalamika popote, then kumehalalisha kila kilichofanyika kwa kuitumia ile kanuni ya "the end justifies the means" kwa hoja hizo, na kwa muktadha huo, Uchaguzi wa 2020 ni uchaguzi halali, na sio uchafuzi kama unavyodaiwa na baadhi ya walioshindwa!, CCM imeshinda ushindi wa kishindo kihalali, na wapinzani wamekataliwa na wananchi na kushindwa kihalali!, the winner takes it all!, the looser standing small.

Paskali
 
Paschall kumbuka kuuliza swali ambalo jibu unalo huo unakua ni zaidi ya ujuha au basi tukuulize na wewe kwakua ulikua sehemu ya uchaguzi (mugombea) mbinu alizotumia mwendazake zilikua halali? Kumbuka hata wewe bila kuponzwa na kile kiswali chako Leo ungekua bungeni kama Gwajima.
 
Sijawahi kushuhudia uchaguzi wa kipuuzi na wa hovyo, kama ule wa 2020! Yaani anashinda Juma, tena kwa kura nyingi tu! Halafu kwenye matokeo anatangazwa John! Aliyeshindwa vibaya.

Polisi na watendaji wa kata, haki ya nani mtaishi maisha magumu sana. Na aliyetoa amri ya kutangaza wagombea wa chama tawala pekee, alaaniwe milele!

Ile haikuwa demokrasia hata kidogo. Ule ulikuwa ni uhuni.
 
Hata uchaguzi wa Marekani wa mwaka 2020 Trumph alidai kufanyiwa rafu, alidi kaibiwa kura na kambi ya Baiden.

Trumph alienda Mahakamani na alibwagwa, lkn hadi leo hajawahi kukubali kushindwa.

Jirani zetu wa kenya Raila alienda mahakamani baada ya kushindwa kwa debe, alibagwa lakini hadi leo hajayakubaali matokeo.

Tatizo la kutokukubali matokeo ya uchaguzi ni tatizo la dunia nzima, iwe imethibitishwa na vyombo vya sheria au la, hata wangeenda Mahakamani bado wasinge kubali.
 
Tukiendelea na katiba hii na Rais kupewa mamlaka za kuteua wasimamizi na waratibu wa uchaguzi watoke kwenye akili na mawazo yake Tanzania kamwe haiwezi kuwa na uchaguzi huru na wahaki. Magufuli alaaniwe huko alipo ametuharibia sana nchi kwa kujaza Wabunge kutoka CCM. 2020 hakukuwa na uchaguzi kulikuwa na uchafuzi. BABU TALE NA MWANA FA eti nao wabunge.
 
Sijawahi kushuhudia uchaguzi wa kipuuzi na wa hovyo, kama ule wa 2020! Yaani anashinda Juma, tena kwa kura nyingi tu! Halafu kwenye matokeo anatangazwa John! Aliyeshindwa vibaya.

Polisi na watendaji wa kata, haki ya nani mtaishi maisha magumu sana. Na aliyetoa amri ya kutangaza wagombea wa chama tawala pekee, alaaniwe milele!

Ile haikuwa demokrasia hata kidogo. Ule ulikuwa ni uhuni.
Bado mnaishia kulalama tu,mngethibitisha uharamu kwa kuchukua hatua, hivyo inabaki kuwa ule ulikuwa uchaguzi halali na ushindi wa kishindo kwa CCM,nimemuelewa sana ndugu" P ".

2025 mtaishia kulalama hivihivi tena bila kuchukua hatua za kisheria kuharamisha. mpaka siku mshinde nyie ndio utakuwa uchaguzi halali.
 
Unajua maana ya hamna aliyelala popote? Au hayo maelezo yako umeshindwa kuyaweka vizuri? Unasema unasikia watu wanalalamika halafu unasema hakuna aliyelalamika popote! Endelea kuomba watu waendelee na huu uoga, siku uoga ukiisha utaona waliokuwa wanalalamika popote wakijitokeza.
 
Bado mnaishia kulalama tu,mngethibitisha uharamu kwa kuchukua hatua, hivyo inabaki kuwa ule ulikuwa uchaguzi halali na ushindi wa kishindo kwa CCM,nimemuelewa sana ndugu" P ".

2025 mtaishia kulalama hivihivi bila kuchukua za kisheria kuharamisha,mpaka siku mshinde nyie ndio iwe halali
Ulitaka hatua gani zichukuliwe kama mchakato wote wa uchaguzi ulivurugwa! Kuionesha tu dunia kuhusu uhuni wote uliotokea, bado nayo ilikuwa ni hatua mojawapo.
 
We jamaa unaandika ujinga tu

ccm 2020 waliiba kura sasa hapo usichofahamu Ni Nini!?
Paskal wewe ni mwanasheria pia? Kama ni hivyo basi tafadhali "Consensus" kwenye andiko lako isomeke "consensual". Kupata majibu ya maswali yako inatakiwa urejee kwenye somo la falsafa. Hili somo, ili uweze kulielewa vizuri unatakiwa uelewe mambo ya msingi kwanza, kwa maana ya kuwa usirukie masuala ya Phd kama uelewa wa shahada za awali hujaumudu. Pengine na kigezo kingine, wale unaowaandikia kama unavyofanya humu ndani, unatakiwa, ama uwafikishe kwenye kiwango chako cha uelewa kama wewe unao uelewa au wao pia wawe wamefikia kiwango hicho kwa juhudi zao . Katika historia ya hivi karibuni, suala kama hili hujadiliwa kwenye kiwango cha juu cha somo la "jurisprudence". Kesi nyingi ambazo hutumika kufafanua mkanganyiko wa masuala unayoyasemea utazipata kwenye kesi za rufaa baada ya utawala wa Hitler kutokomezwa Ujerumani. Mahakama huzo za rufaa zilikuwa zinasikiliza rufaa za wahanga ambao walikutwa na hatia wakawa bado wako hai baada ya Vita Kuu ya Pili. Hawa waliokutwa na hatia wakati wa Hitler, mahakimu ama hawakufuata sheria za wakati wa Hitler au walitumia sheria ambazo hazikuwa halali katika kipimo cha misingi ya utu. Baada Mahakama za rufaa kupitia rufaa hizo na kutoa uamuzi wa rufaa ambao waliona ni sahihi, hizo mahakama zilirudi na kuamua kama mahakimu au majaji waliowatia hatiani hao wahanga ambao wameonekana kuwa hawajuwa na hatia hata wakati wa Hitler, je mahakimu na majaji nao wahukumiwe kwa makosa yao? Mahakama za juu nyingi zilikubaliana kuwa vuguvugu, ushabiki na vitisho ambavyo chama cha Hitler na serikali yake wakati huo vilisababisha mahakimu na majaji kutotenda haki kama nafasi na utulivu waliokuwa nao Mahakama za rufaa baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kuisha na Hitler na Chama chake kupigwa marufuku. Mahakama za rufaa zikiona kuwa uwanja, mantiki na haki vilikuwa tofauti kwenye mazingira tofauti. Kwa ushauri wangu, si vema kuwadhakisha watoto wa chekechea majoho ya Phd na kuwaaminisha kuwa wamepata hiyo elimu wakati ndiyo kwanza wanaanza safari ya elimu.
 
Kaka Pascal nimekuelewa,kuwa kila mchezo una kanuni za kuingia na kutoka.Uchaguzi unafanyika kwa mujibu wa sheria na kanuni ambazo zinaeleza kila hatua ambayo mgombea anapaswa kufuata,kuanzia kuchukua fomu, kuirudisha,kuteuliwa,kugombea,kutangazwa mshindi na hatua za kuchukua endapo hujaridhika na matokeo.Sasa kama mgombea alishiriki kwa kujua kanuni na sheria za mchezo alafu anachagua vipengele vya kutekeleza,asaidiweje?
Naunga mkono hoja kuwa uchaguzi ulikuwa halali,na hauwezi kuwa batili kwa kanuni za nje ya mchezo(lawama) bali utakuwa batili kwa kuwa challenged na kanuni za mchezo husika(mchakato wa sheria za uchaguzi).
 
Back
Top Bottom