January: Sitorudi nyuma kuhusu urais 2015

January: Sitorudi nyuma kuhusu urais 2015

Hata January wa Makamba! Kweli JK amefanya ikulu iwe rahisi kwa kila mtu kukaa pale kama mkuu Wa nchi.
 
Mi naona makamba yupo kwenye category ya hao marais wazuri coz kwa uthubutu wake wa kutangaza hadharani kuwa anahitaji kuwatumikia watanzania kama rais na kutupa sisi fursa ya kumpima kwa kina ni jambo ambalo linaonyesha uzalendo, uadilifu, na nia ya dhati ya kuwatumikia watanzania

Mimi naona yuko ktk orodha ya 'wenye uthubutu', lakini kuhusu kwamba ni 'rais mzuri' nadhani bado tumpe muda zaidi, tumsikilize mwenyewe binafsi akijieleza ili tuweze kumpima ktk mizani.

Urais ni suala la kitaifa na si dogo kama linavyopigiwa debe hapa. Kama ana nia ya dhati kabisa na cheo hiki basi na atarajie changamoto nyingi mbele, anazozijua na asizozijua; gari bado iko silence haijaondoka na pia haijajaa abiria.
 
Hivi mlitaka awafanyie nini? hivi wewe umeifanyia Tanzania?

Mtu ana nia ya kugombea Urais ili awatumikie Watanzania, wewe unauliza "umewafanyia nini watanzania".

Kwani kumpa mtu Urais ni fadhila kwa alichowafanyia? au ndiyo fikra za kirushwa-rushwa, hutoi kura mpaka ufanyiwe?

Hivi uko sawa?

Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?
 
Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?

Wewe ni agent Wa udini?
 
Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?

Umasikini wa Fikra katika hiki kizazi
 
Baba yake muislam mama yake Mkatoliki. Yeye muislam lakini kaoa Mluteri. Kwa changamoto za migawanyiko ya kidini zinazoanza kujitokeza nchini, huyu historia yake pekee ni onyesho na ishara kwamba Watanzania wa dini mbali mbali tunaweza kuishi pamoja Kwa Amani na upendo.Kwa sasa Makamba ndiye pekee atakayeweza kutuunganisha.
 
Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?


Jana maaskofu wametoa tamko la kumtakia Makamba safari yenye mafanikio huku wakisema 2015 ni mwaka Wa kizazi kipya.
 
Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?

Mkuu, hizo ni propaganda tu; hatuwezi kusimamia hoja hiyo kwa masuala makubwa kama haya ya kumpata rais.

Rais atakayechaguliwa ataongoza watu wa dini zote, na katiba ya nchi pia haitoi mashiko kwa hoja ya udini. Naona kwa mambo nyeti kama haya tusimamie misingi ya umoja na kitaifa zaidi badala ya kugawanyika kwa tofauti kama hizo za kidini.

Tutalumbana na kufarakana sana, lakini hatima ya yote rais atakayechaguliwa hatauliza dini zetu; kama itakuwa kheri ni kwa wote, na kama ni shari ni kwa wote pia. Kwa maana hiyo faraka hizi tunazozijenga hazitakuwa na manufaa kwa yeyote, awe Mkristo, Muislamu au mwingine yeyote.

Vita ya panzi furaha kwa kunguru. Tunapolumbana, wachache wanajiandaa na namna ya kunufaika na mgogoro wetu!
 
Ni wazo nzuri na Mh; January anakiu na tanzania lakini ukweli nikwamba muda wake bado, ajafanya kitu cha kuweza kutushawishi vijan wenzake tumuunge mkono bado aridhike na unaibu waziri pia ashukur kwa kubebwa hadi alipofikia ajitumi tena na tena na mda ukifika hatosema anataka urais bali ni watanzania ss wenyewe tutamuomba agombee urais ila kwa sasa akitulize tu...!
 
Wewe ni agent Wa udini?

Maajenti wa Udini na Ukabila walitembea sana Misikitini kwenye kampeni ya Urais 2010 matokeo yake Mapadre na Wachungaji wanauwawa na wakristu wanalazimishwa kuchinjiwa wanyama wao na Waislamu.Hili jambo linasababisha wakristo wawe wapweke katika Nchi yao.Lazima hali hii irekebishwe ili twende sawa.
 
Mkuu, hizo ni propaganda tu; hatuwezi kusimamia hoja hiyo kwa masuala makubwa kama haya ya kumpata rais.

Rais atakayechaguliwa ataongoza watu wa dini zote, na katiba ya nchi pia haitoi mashiko kwa hoja ya udini. Naona kwa mambo nyeti kama haya tusimamie misingi ya umoja na kitaifa zaidi badala ya kugawanyika kwa tofauti kama hizo za kidini.

Tutalumbana na kufarakana sana, lakini hatima ya yote rais atakayechaguliwa hatauliza dini zetu; kama itakuwa kheri ni kwa wote, na kama ni shari ni kwa wote pia. Kwa maana hiyo faraka hizi tunazozijenga hazitakuwa na manufaa kwa yeyote, awe Mkristo, Muislamu au mwingine yeyote.

Vita ya panzi furaha kwa kunguru. Tunapolumbana, wachache wanajiandaa na namna ya kunufaika na mgogoro wetu!

Mawazo yako ni Mazuri sana na ndivyo tulivyolelewa Watanzania.Tatizo lilianza kwenye Uchaguzi wa 2010 wakati kampeni za udini zilipopigwa waziwazi Misikitini.Profesa Lipumba ni Shahidi kwa hili.Hivi sasa Viongozi waandamizi wanatukana Viongozi wa Kikristo hadharani,Makanisa yanachomwa Moto mchana na hakuna anayepatikana na hatia ilhali Wachaga na watu wa Kaskazini wanatukanwa kwa sababu ya kabila lao.Katika hali kama hii ni Lazima wakristo na wachaga wachukue hatua za haraka ili kujinusuru.
 
Ni wazo nzuri na Mh; January anakiu na tanzania lakini ukweli nikwamba muda wake bado, ajafanya kitu cha kuweza kutushawishi vijan wenzake tumuunge mkono bado aridhike na unaibu waziri pia ashukur kwa kubebwa hadi alipofikia ajitumi tena na tena na mda ukifika hatosema anataka urais bali ni watanzania ss wenyewe tutamuomba agombee urais ila kwa sasa akitulize tu...!

Hao wazee wametufanyia nini zaidi ya kutuibia?kama umefuatilia post hii vizuri utajua ni zipi jitihada za Makamba katika wizara Na jumbo lake.
 
Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba amesema hatakatishwa tamaa na hatorudi nyuma katika harakati zake anazoziita za fikra mpya na mawazo mapya za kushika dola na kwamba wazee wakae kando.

Hata hivyo, Makamba ambaye pia ni mbunge wa Bumbuli (CCM) amewashukuru watu wanaozungumzia nia yake ya kuwania urais mwaka 2015 na kutengeneza mjadala unaoendelea nchini, jambo ambalo alisema linaashiria kuwa dhamira yake imeeleweka.

Akiwa London nchini Uingereza mapema mwezi huu, Makamba alitangaza nia hiyo na kusema amefikia uamuzi huo kwa asilimia 90 lakini bado asilimia 10 katika baadhi ya mambo anayoendelea kuyatafakari, yakiwamo ya kuzungumza na makundi mbalimbali ya wazee, viongozi wa dini na viongozi waliopita ili apate ushauri wao kuhusu namna ya kufanya jambo hilo.

Julai 9, mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete, ambaye anamzidi januari kwa miaka 24, alisema kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Soni, Bumbuli mkoani Tanga kuwa Makamba anataka mambo makubwa, lakini hajamshirikisha.

Rais Kikwete alimtaka Makamba “asilazimishe” kwa kuwa wakati ukifika atapata kile anachokitaka. “Mie hajaniambia na mie nasikia,” alisema Kikwete.

Akizungumzia na gazeti hili jana kuhusu kauli ya Rais Kikwete, Makamba alisema: “Ni kweli sijamwambia. Siku itakapofika yeye ni mwamuzi na mwenyekiti wa chama hivyo nitamweleza. Sitaki kumkwaza kwani na yeye ni wale waliopo katika kundi la asilimia kumi,” alisema.

“Zama za kizazi kipya za kutatua changamoto kwa kipindi cha miaka 30 hadi 50 ijayo zimewadia. Nitahakikisha mabadiliko ya haraka katika ardhi ya Tanzania kwani inawezekana rasilimali za kutosha zipo kilichobaki ni kuweka nidhamu katika nyanja zote.”

Aliwashangaa wanaombeza akisema kuwa hawamkatishi tamaa kwa hilo.


Chanzo;Mwananchi
Ndugu yangu JM wazo lako zuri sana, lakini omba kwanza ushauri jipime Mara Saba then amua.kuna wengi wametoa comments zao. Zipitie tena na tena. Ukiona kama kweli una fit kuwa Rais endelea lakini kama ni mihemuko ya ujana endelea kujiandaa. Wakati ukifika utaona tu wewe mwenyewe unaombwa au unaarifiwa kufanya hivyo. JM sio kama ulivyojieleza kwenye utangulizi wako ikionesha uzoefu wako Ikulu na ziara mbalimbali duniani. Watu uliokutana nao nk. Jipime tena na tena then go head
 
Makamba pekee ndio wakutuunganisha watanzania coz kazaliwa kwenye familia ya baba muislamu Na mama mkristo Na make wake ni mkristo.Ni rais sana mtu huyu kuyaunganisha makundi yote
 
kila mtu kwa nafasi yake amuunge mkono kijana na kama tulivyoshauriwa na maaskofu jana kuwa kijana yeyote mwenye uwezo ni wakati wake sasa.2015 Ni mwaka wa kizazi kipya.

Hii sifa mpya ya ujana pekee inatia mashaka sana, nyie makuwadi wake ilitakiwa muongelee sifa zake za zinazotosha kuwa rais na hiyo ya ujana iwe chagizo tu maana vijana Tanzania tuko milioni kibao huku milioni kibao10 hawana ajira rasmi
 
Kuna uzi unasema 2015 ni Zamu ya Wakristo kwa sababu wamechoka kulazimishwa kuchinjiwa kuku wao kwa Ibada za Kiislamu ambazo kwa Wakristo ni sawa na kuabudu Miungu.Je Makamba ni Mkristo?

Aliyezowea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi.
 
Mawazo yako ni Mazuri sana na ndivyo tulivyolelewa Watanzania.Tatizo lilianza kwenye Uchaguzi wa 2010 wakati kampeni za udini zilipopigwa waziwazi Misikitini.Profesa Lipumba ni Shahidi kwa hili.Hivi sasa Viongozi waandamizi wanatukana Viongozi wa Kikristo hadharani,Makanisa yanachomwa Moto mchana na hakuna anayepatikana na hatia ilhali Wachaga na watu wa Kaskazini wanatukanwa kwa sababu ya kabila lao.Katika hali kama hii ni Lazima wakristo na wachaga wachukue hatua za haraka ili kujinusuru.

Mkuu, hapa ndipo tunapotakiwa kuwa pamoja na makini ili tumchague mtu atakayeepukana na hayo mapungufu. Haitakuwa busara kumchagua mtu kwa sababu tu ni kijana, Muislamu au Mkristo. Kutokana na majeraha makubwa tuliyo nayo inatakiwa tuende mbali zaidi na tupanue wigo wa sifa za mgombea kuliko ilivyo sasa.

Sisi tuko dini mchanganyiko, na hatuwezi kuiepuka hii hali. Vyovyote iwavyo, iwe kwa njia halali au haramu Rais ni lazima apatikane na pia atakuwa wa dini fulani. Hakuna mtu atakayetibiwa au kusomeshwa bure kwa vile Rais ni wa dini yake. Matokeo ya uongozi huo yataathiri watu wote.

Kwa mantiki hii basi, tusiwe wa dini fulani bali tuwe Watanzania tulioathirika kwa ujumla wake na mfumo wa utawala na uongozi ambao kwa njia moja au nyingine haututendei haki. Mathalani, tunapojadiliana hapa, hujui dini yangu nami sijui dini yako. Tunaunganishwa na moyo wa uzalendo, na huo ndio Utanzania. Dini ya mtu itamsaidia vipi kama tutaanza kugawana mitaa na kupigana mapanga?

Tuangalie kwa wenzetu, tusome alama za nyakati, bado hatujachelewa. Mchelea mwana kulia hulia mwenyewe, na sikio la kufa halisikii dawa!
 
kila harusi ina wasindikizaji wake,huyu kipara naye msindikizaji tu.
 
Huyu Jamaa namfananisha na shabiki wa yanga Steve....what he's record instead writing nonsense jk speech.
 
Back
Top Bottom