January: Sitorudi nyuma kuhusu urais 2015

January: Sitorudi nyuma kuhusu urais 2015

Unajua nani kachangia mawazo mpaka leo hii nchi yetu inavuna kodi ya international calls kiasi cha zaidi ya billioni moja kila mwezi baada ya kufunga mtambo wa kubill ni nani?, unajua mgogoro wa Aritel na TTCL mpaka hivi karibuni tunatarajia ubia umaalizike ili kampuni mama limilikiwe na serikali 100% na lianze kukopesheka na hatimaye tutumie simu za kampuni mama kimawasiliano nani anaratibu kumaliza huo mgogoro ? unajua mawasiliano vijijini ufungaji wa minara inayotumia sora ili kupeleka mawasiliano vijijini na mipakani kote ambako network ilikuwa haipatikani nani ameongoza kampeni hizo na sasa baadhi ya vijiji wanawasiliana bila matatizo ni nani kachangia kufanikisha?....... najua haya ulikuwa huyajui ila kwa taarifa yako kijana January baada ya kufika pale wizarani mapinduzi makubwa ya mawasiliano yametokea na kwa taarifa yako sasa hivi inafungwa device ambayo itamonitor mawasiliano yote hapa nchini na kugundua kila mtu atayepiga simu au kutumia mitandao kwa nia ovu yuko wapi na device hiyo kama ni simu au computer kuna uwezekano wa kudestroy remotery na isifanye kazi daima kwa hiyo tutakomesha uchochezi..... kwa hayo machache wewe unasemaje!

Asante kwa kuwapa fact.
 
january njia nyeupe ikulu 2015.m/mungu akupe afya njema na akulinde na maasidi wa nchi hii.
 
Muda wa Tanzania kuongozwa hata na vichaa unakuja.
Katangaza nia na akigombea atashinda mtachoka.

Hakuna Makamba mtu makini Na atashinda tu,Ni Kijana aliyeishi katika mazingira halisi ya kitanzania.
 
Tunahitaji kuchagua watu kwa facts zilizopo mezani na sio mere beliefs.Tunahitaji tuletewe majina yenye historia iliyojaa minofu ili tumhukumu mtu.Huyu bwana ana historia changa mno kiasi kwamba tutamhukumu by chance,na kama tutaamua kumpitisha mtu wa aina hii basi ni kuiweka nchi rehani.Napendekeza rais wa nchi awe ni 45+ na wabunge,mawaziri,wakuu wa mikoa na wilaya,wakuu wa majeshi na maafisa wa ngazi za juu jeshini,wakurugenzi wa wizara,makatibu wakuu na vyeo vya level hizo wawe 40+.vijana tupewe muda wa kuingia majaribuni na kupimwa kama hatubadiliki kama akina Z..Aaah,nimesahau,.napendekeza pia umri wa walimu wa shule za vidudu uwe 40+,primary na o level uwe 35+,A level na kuendelea 30+.Walio chini ya hapo tuwatafutie mfumo wa kuwagroom kwanza.Vijana oyee!
 
Unataka tuwape wazee we ye uzoefu Wa kuibia taifa hili kama lowasa?

Umeweza kumhukumu mzee Lowasa kwa sababu tayari ana historia iliyojaa minofu,hivyo unatazama ni mizuri au mibaya kwako.January utamtathmini kwa kipi?jamani ikulu sio bilicanas jamani,hapahitaji fasheni wala "usawa" pale.Tusiwe emotional kwenye mambo ya msingi namna hii.
 
Kwa hiyo kuongoza wizara ndani ya kipindi kisichozidi 10 years na kuleta mabadiliko inatosha kumpa urais mtu?wana jf mna utani mbaya,kwii kwi kwi kwi,kwii kwii kwii kwi kwii,Dogo kuingia wizarani tu jamaa kumuogopa wakafunga device,ile kuingia tu,airtel na ttcl wakaacha kugombana,ni mafanikio makubwa,anafaa urais jamaaani kwiiii kwiiiiii,kwii,uh,uh,uh,aah,auwii,uh,uh!
 
sasa wewe mambo haya ya mitandao unayaleta kama ushahidi huna tofauti na waliopiga picha kaburi la barali na kudai eti alifariki kweli, utajisikiaje siku nikisajili akaunti mchunguzi@yahoo.com alafu nikaandika upuuzi maana yake ni wewe au ni ndugu yako? Amagezi nkekikere chwekao.

Tuondolee uchafu wako hiyo hata mi naweza kutengeneza.

Documenti hii wakati ikijadiliwa hapa, wote mulikuwa hamujazaliwa hapa jf. Nyamazeni wakubwa zenu waongee. Historia yenu hapa ni ya 2014. Tena mwingine ni wiki jana tu, 10 july. Umepata ajira? Hongera lakini naona muko chini ya kiwango.
 
Mwadilifu,uzalendo,mwenye umakini wa hali ya juu.Uzalendo wake hauna shaka

Hivi umeishia darasa la ngapi?? Au niulize umepata divisheni gani? Unaweza ukatoa sifa zisizopimika?
Hebu ulizia wizi wa mitihani pale galanosi ilikuwaje. Akikujibu ndo uheme kumutetea.
 
Urais wa Tanzania umeshapoteza uelekeo baada ya Ben kuondoka!!
 
uwezo wa kuongoza nchi unaoujua wewe ni wa sifa za kuiba wake za watu kama babu yako mstaafu slaa!!

Tatizo la watu msio na akili hajui kitu cha kujadili!! Mmeleta thread kuwa January anafaa, tunahoji uwezo wake mnaanza kujadili Silaa. Wapi nimesema Silaa ndiye chaguo langu!!? Tutataka mtuambie uwezo wa January kama kiongozi!!
 
Tatizo la watu msio na akili hajui kitu cha kujadili!! Mmeleta thread kuwa January anafaa, tunahoji uwezo wake mnaanza kujadili Silaa. Wapi nimesema Silaa ndiye chaguo langu!!? Tutataka mtuambie uwezo wa January kama kiongozi!!

Mkuu, tatizo la wachangiaji wengi ni kushindwa kujadili mada inayowekwa jamvini na badala yake huingiza hisia nyingi binafsi pamoja na chuki.

Kwa mfano, kama mdau alitaka Slaa ajadiliwe basi angeanzisha uzi rasmi. Tatizo hili ni kubwa sana hapa JF kiasi kwamba inataka fikra ya pili ili kuamini kama ni kweli jukwaa ni la 'Great Thinkers'


lnatakiwa ifike mahali jukwaa hili lifikie matarajio yake. Wako wachangiaji humu wenye maarifa mengi na uoni mpana na wasio na choyo ya elimu kiasi kwamba tunanufaika sana na weledi wao wa mambo.

Natoa rai kwa wadau wenzangu, tuache chuki binafsi na kejeli ili tunufaike na jukwaa hili. Mada inapowekwa mezani isiwe ndio mahali pa kutolea chuki, hasira na kukashifiana. Wote kwa ujumla wetu tunazo tofauti zetu; tuvumiliane na kuheshimiana ktk tofauti zetu hizo. Haya ni maoni yangu tu, kwa kadiri ya uoni wangu.
 
january makamba ni somo tosha kwa wabunge wetu
ambao
hufikiri kujinufaisha wenyewe pasipo kuweka maslahi ya
waliowachagua mbele.
January alinifanya nitafakari kwa kina, kumbe inawezekana
kwa wabunge wetu hata kama wanaishi mijini (Arusha na
Dar es Salaam) lakini hukohuko walipo wakafanya kitu kwa
ajili ya wananchi majimboni mwao. Ni kweli kuwa wasomi
wengi kama si wote wapo mijini lakini swali ni je, wabunge
wetu wamefanya jitihada gani kuwaunganisha huko walipo
na kubuni miradi ya maendeleo huku nyumbani? Nadhani
ni wakati muafaka kujifunza kutoka kwa January ambaye
anawakilisha vijana wapenda mabadiliko katika jamii.
 
Wengi wanasema kizazi kipya, wengne wanasema Makamba, nine wanasema kijana, wengine wanatumia neno mabadiliko.

Mimi nasema yote hayo ni upuuzi tu! UPUUIZI! Ni sawa na kusema rais awe mrefu, awe mwanamke, mwanaume au mfupi. Then what for? Kijana for what? mzee for what? Tunataka mtu mwenye uwezo, FINITO. Munaosema awe Makamba, anazo sifa? If not, RUBBISH!

Hebu someni mawasilian hayo yaliyowahi kuletwa hapa JF. Mtu aliyeombewa nafasi kwa ufisadi wa aina hizi, hat Ngono!

Ni afadhali mtufumbue macho maana wengi wetu ni vipofu. Tunaposema hafai ni hafai kweli! Hata zito kutokana na mishemishe zake kwenye madini na JK mwenyewe kajikusanyia pesa wee akaona sasa ana sifa za uenyekiti CDM na urais wa nchi!

Tatizo nchi imevurugika kiasi kwamba hata mchakato wa Katiba haueleweki kwa hiyo tunaweza kuja kumpata rais ataketuangamiza kabisa.
 
Back
Top Bottom