KERO Janga la uhaba wa maji ni kubwa kwa wakazi wa MailiMoja – Kibaha (Pwani), shida ni kubwa mno

KERO Janga la uhaba wa maji ni kubwa kwa wakazi wa MailiMoja – Kibaha (Pwani), shida ni kubwa mno

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
654
Reaction score
1,598
Ni takribani mwezi mmoja sasa maeneo mengi ya Kibaha MailiMoja kuna changamoto kubwa ya maji na majibu ya Mamlaka ya Maji yamekuwa ya kuungaunga.

Awali walitoa taarifa kuwa maji yatakoseka kwa siku chache takribani tatu hadi nne kutokana na maboresho ya mitambo yam aji, lakini ilipita wiki mbili bila maji.

Baada ya hapo baadhi ya maeneo yakaanza kupata maji mdogomdogo, wale waliokosa walipouliza wakajibiwa kuwa yatatoka ndani ya saa 24 kwa kuwa bado hayana nguvu ndio maana yanatoka kwa uchache katika baadhi ya maeneo.

Hali hiyo imeendelea hadi sasa na mwisho wake tuna wiki moja hakuna maji kabisa n ahata zile sehemu ambazo yalikuwa yanatoka mdogomdogo kwa sasa hayatoki kabisa.

Hali ni mbaya, wakazi wa MailiMoja hasa mitaa ya Mpiji, Muheza, Tankini kwa Mbonde na kwingineko tuna hali mbaya, kwani tunalazimika kutumia fedha nyingi kununua maji n ahata hayo tunayoyapata napo kazi ni kubwa.
 
Polen sana na changamoto.
Je ? Uliwafuata kuwauliza wakuambie shida ni nin?.
Bado maboresho hayajakamilika? Au kuna Lingine.

Sehem ambayo ina miundo mbinu ya maji atleast maji yatoke mara 1 au 2 kwa wiki.
Sasa kwa wiki 4 hayajatoka.
Mmmmh ni hatar hiyo.
 
Polen sana na changamoto.
Je ? Uliwafuata kuwauliza wakuambie shida ni nin?.
Bado maboresho hayajakamilika? Au kuna Lingine.

Sehem ambayo ina miundo mbinu ya maji atleast maji yatoke mara 1 au 2 kwa wiki.
Sasa kwa wiki 4 hayajatoka.
Mmmmh ni hatar hiyo.
Juma anasemaje kuhusu hilo?
 
Kweli vyombo vya habari bongo vimepigwa pin, ujue ukiona jinsi wanavyopongozana na uhalisia wa maisha tofauti kabisa.
 
Kweli vyombo vya habari bongo vimepigwa pin, ujue ukiona jinsi wanavyopongozana na uhalisia wa maisha tofauti kabisa.

Kuna namna mm Nawapongeza Tanesco.
Hii kuanzisha group za whatsapp ili kutoa taarifa na kupokea malalamiko imefanya Shirika liwe na ufanisi kwa upande wa kuwahudumia wateja.

Mashirika mengne yanayotoa huduma kwa jamii yaige huu mfano.
 
Ila hii nchi alieturoga sijui ni nani, tunajisifia sijui SGR, Interchanges na upuuzi mwingi ila masuala muhimu ya maji safi kwa umma yanatushinda. Nini kibaha uko mbali hapo tu Mabibo na Kimara kuna shida mbaya ya maji. Eti Dar ni New York. Nyanoko bhebhe.
 
Back
Top Bottom