Mtoto mzuri atembea na wanaume watatu,apata mimba na hajui yupi ni baba wa mtoto, zigo lasukumwa kwa mtoto wa kishua
Watoto wa kishua mpo? Habar ndio hiyo,msichana huwa ana kawaida ya kuangalia wapi kwenye mbolea ambapo mtoto atapata matunzo mazuri,kwahiyo nyakati nyingine sio kwamba mnapendwa ila mnachaguliwa kwakuwa mna uwezo wa kuprovide
Show imerekodiwa 14,February,2026 siku ya wapendanao.
Chalii mmoja yupo na mtoto mzuri rangi ya Mtume,portable flani hivi unaweza hata kumuweka begani na kusepa nae nyakati za hatar
Story.mbili tatu hapa na pale, wakaambiwa kuna safari ya Zanzibar kwa wepandanao ambao hawana mpango wa kando/hawana hawara
Mchongo uko hivi,kama wote mkikaguliwa simu zenu na mkaonekana mpo fresh hakuna mpango wa kando,basi mnalipiwa trip kwenda kizimkazi Zanzibar kwa 2 nights
Kabla ya kusonga mbele,hawa ni wanandoa ambao wapo kwa ndoa kwa miaka 3 sasa na wamejaliwa kababy girl ka ten months
Okay tuendelee......
Wakaulizwa kwanza, kama mke ukijua mwanaume wako anachit utafanyeje, mtoto mzuri akasema " sidhani,ila kama akinichiti ninamuacha"
Homeboy akaulizwa kama mkeo ukikuta amechiti niaje,akasema kwanza sidhani kama yupo hivyo,hali tuliyofikia hatuwezi kufanya mambo hayo,nipo optimistic kwamba kila kitu kipo poa
Homeboy akaulizwa ebu mwambie maneno ya mwisho mkeo kabla hatuja kagua simu na mambo kuharibika, chalii akasema " nimeandaa hotel nzuri ya kufikia na mke wangu kama kwa wiki moja hivi
Wife nae akaulizwa una maneno gani ya kumwambia mume wako kwenye Valentine hii, akasema "nampenda sana mume wangu amesacrifice mambo mengi kwa ajili yangu na mtoto,kuna mambo ameyaacha kwa ajili ya kuangalia familia yetu
Wakati ukawadia wa simu kufanyiwa operesheni maalumu kabisa, simu ya homeboy ikachekiwa inside out,mtoto wa mshua mwenye hela zake yupo clean, wanaume kwakweli hawatuangushi,ni yule chalii mmoja tu chapisho la siku kadhaa nyuma aliye wachapa mama na binti ndio alituharibia Cv
Mtoto mzuri akatoa nywila/password kumpa mtaalamu simu ifanyiwe operesheni maalumu,mwamba hana baya kaingiza code zake mzigo huu hapa
Demu anachati na dada yake,anamwambia nimepima mara tatu nina mimba,na sijui baba wa mtoto ni yupi kwasababu nimekuwa nikipush na wanaume watatu
Akaendelea kufungua code,naogopa kumwambia mama sababu anaeweza kumwambia baba
Dada yake akamuuliza " je kuna.mtu mwingine anajua hili?" Mdogo mtu akasema "ni wewe tu ndio unajua"
Akaulizwa je, ni yupi unampenda? Mtoto mzuri akajibu fulani nampenda lakini bado anastruggle,ila kuna mmoja ni zero love,akimaanisha hampendi ila kwao kuna doo/ kuna pesa
Dada yake alimshauri asiwe kama yeye yupo na jamaa yake wapo kwenye slum/uswahilini
So mchongo ukawa hivi atest Zarii kumwambia huyo Homeboy kuwa ana mimba yake,ebu tuweke pozi kwa nza hapa nataka kuongea kitu,kumbe sometime unajaribiwa kuambiwa ni mimba yako,sasa ukitekenyeka kirahisi imekula kwako,boys mna la kujifunza hapa
Let's go...kweli bwana mtoto wa kishua alivyoambiwa demu ana mimba akajaa kwenye mfumo,si unajua tena ukiwa na mtoto mzuri halafu akakwambie ana mimba yako,basi unajiona kama vile wewe ndio kidume,kumbe fala tu!
So chalii ambaye sasa tumuite boya,chap kamchukua mrembo mpaka home,tambulisha kwa mshua,mama na ndugu zake,unaambiwa mtoto kakubalika sana,huenda ana nyota ya chips hahaha
Mawifi zake wakamnunulia ndinga,yes ndinga unashangaa nini sasa!!! Kwakuwa wewe huna hela unafikiri wote hawana hela
So maisha yakaendelea vizur mpaka hapo siri ilipofichuka
Mtoto wa mshua akipoonyeshwa hizo meseji hakuamini macho yake,kila akisomewa na kusoma mwenyewe anarudia mara mbili mbili
Akakuta mtoto amefunguka hizo habar kwamba,amekuwa na wanaume watatu,akaona mimba akabidhiwe mtoto wa kishua
Na kibaya zaidi demu alisema huyo baba mkwe wake ni kama gunia tu huenda ndani ya miaka miwili atakufa
Hizo habar za mshua kufananishwa na gunia na kwamba ndani ya miaka miwili mshua atakata kamba zilimuumiza Homeboy
Akafunguka " yani baba yangu ambaye anatulipia nyumba yenye 3 bedrooms ambayo rent yake ni kama 25k unamuita gunia?"
Chalii akaendela kutoa nyongo " huyu baba ambaye ametupa plantation unamuita gunia na kwamba ana miaka miwili ya kuishi,je wewe ni malaika Israel utachukua roho yake"?
Huyu mrembo ambaye sasa tumuite mbwa,akasema "baby hIzo si mambo ya zamani"
Huyu mbwa akaendelea tena kusema "baby hayo ni zile mambo ya zamani,si now tupo pamoja"
Chalii akafungua mafaili zaidi " unamuona huyu dada yake kila siku ananiomba hela kwamba sijui jamii yake hana hela ana maisha magumu,kwahiyo kila wiki namtumia hela,yani hata hapa bro naweza kukuonyesha hizo meseji za hela"
Mwisho Homeboy akampora simu yule mwanamke na kumwambia huu ni ushahidi nampelea baba akaone ambaye wewe unamuita gunia
Demu akamwambia mumewe naomba simu yangu,Homeboy akasema hii simu nimekununulia mimi naichukua,kama haitoshi Homeboy akasema yule mtoto hataki kumuona ndani ya masaa mawili.
Guys, hayo ndio mapenzi bwana,narudia tena usijigambe kwamba mkeo au mumeo au boy wako au girl wako yupo special kwamba she/he is innocent,we shukuru tu mpoa pamoja mengine mwachie mwenyewe
View: https://youtu.be/TQpvyPfzyQQ?si=r-gQB5s4J3ucJTXg
Kwa mastory kama haya ya kuelimishana na ambayo ni true events/matukio ya kweli just tembelea uzi mkubwa hapa jamii forums nao sio mwingine ni "Usiku wa Manane" daily am your host Ertugrul bey
Alamsiki!