JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Mwanaume mkeo au mwenza wako akipokea simu iliyoseviwa Dady hakikisha anaongea mbele yako huenda kuna mengi huyajui

Hapa ndio mtaani kwetu Usiku wa manane, hapa unawakuta akina win-one na pacha wake ShesRise_1 , mshamba_hachekwi Selikavu ,dosho12 ,Fake P na wakitaa wengine kibao tu kama wote .

Kuna jamaa mmoja ana mke wake mwenyewe,wana kama miaka minne ya ndoa,jamaa kafanya mambo mengi sana kwa mkewe,ikiwemo kukopa kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya kughamia mazishi ya dada yake na mkewe,kuanzia kulipa Bill ya hospital mpaka mazishi,na kupelekea hata gari kuchukuliwa na bank

Guess what? Kumbe mke alikuwa anatoka na rafiki wa mume wake ambaye ni mfanyakazi mwenzake pale Bank . Bidada bila aibu akiwa na mtoto wa mwaka mmoja anachepuka na saa nyingine anachelewa kurudi home kumbe yupo kwa mchepuko wake bwana Charles

Sasa mchepuko kaseviwa Dady,so mume wake akiona dady anapiga basi hagusi simu hata kama mkewe yupo bafuni,akija mkewe anachukua simu na kuenda faragha kuongea na dady. Mume anasema kwakuwa anamuheshimu baba mkwe hivyo humuacha mke awe na faragha aongee na dady yake,kumbe ni mchepuko wake

Guys kiukweli kabisa ukijua mambo ya wanawake unaweza kubadilisha mtazamo wako juu ya hawa viumbe,kuna show moja hapo Kenya inaitwa Comrades flavour ipo YouTube, nakushauri mwanaume ifuatilie hii channel ndio utajua hujui kuhusu wanawake

Heshima kwake Britanicca katika uzi wake mkoja wa hivi karibuni pamoja na mambo mengine aliintroduce hii kitu,aisee nimeangalia kama video 4 au 5 ni moto wa kuotea mbali,kuna mengi ya kujifunza kwenye maisha,na muhudumie mkeo,mwenza wako kadri unavyoweza lakini haupo peke yako,naweza sema asilimia 99.9 wanaume wote tunachapiwa,narudia tena tunachapiwa period


View: https://youtu.be/oKdkDfEmziA?si=9r-sHT1N2wG5mEbk

Sasa wakati huyu mume anahojiwa na mtangazaji ni kwa kiasi gani unamuamini mkeo,akasema namuamini sana,akaulizwa je ikitokea habari tofauti,akasema sidhani kama mwanamke wake yupo hivyo

Anachofanya jamaa anachukua simu ya mume na mke au ya wenza halafu,hata sijui ana utaalamu gani wa kusearch mambo humo,aisee anafuma meseji humo,kama ni simu ya mkeo akishagundua sinto fahamu anamuita mume pembeni na kuzisoma zile texts,kisha wanaenda wote kwa mwanamke,hapo mwanamke anaonyeshwa uchafu wake,anabaki kulialia na kuomba asamehewe.

Basi bwana,jamaa akaonyeshwa meseji za mkewe,hakuamini,kumbe mfanyakazi mwenzake ndio kaseviwa dady, kumbe siku zote hizo,jamaa anamuacha mkewe aongee faragha na dady yake kumbe ni mume mwenzake

Hakikisha mwanaume unaangalia hiyo show,kama huna bando,ukifika ofisini kama mna wifi just download hizo show YouTube kisha utazicheki baadae,ni noma sana aisee

Alamsik!

Me naamini katika kutomlazimisha mtu kufanya kitu fulani...

Nikijua namwambia tu ukwel uende kwa Aman ya Bwana ukapate hitaji lako kwa Aman😃
 
Back
Top Bottom