Miss Neddy
JF-Expert Member
- Nov 3, 2013
- 14,684
- 8,760
Jamii zote zilizoendelea zimepata kuendelea kwa kujali faragha na maamuzi ya watu binafsi. Hata wanapokuwa tofauti na jamii.
Hivyo ndivyo watu walivyopata kujua kwamba dunia si bapa bali ni tufe karibu na mduara.
Hivyo ndivyo watu walivyogundua kwamba jua halizunguki dunia, bali dunia inazunguka jua.
Hivyo ndivyo watu walivyogundua kwamba muda si kitu kimoja kwa ulimwengu mzima (I am not talking about time zones, rather Einstein's relativity) na unategemea kasi na sehemu ya mtazamaji.
Kama binadamu angekuwa anaaangalia na kuheshimu taratibu za jamii muda wote, tungekuwa bado tunaishi mapangoni na hata moto hatujagundua mpaka leo.
Kwa sababu hata ugunduzi maana yake ni kuibua kitu kipya na tofauti, ambacho hakijakubalika wala kujulikana na jamii.
Kwa hivyo, kama jamii inataka kuendelea, haina budi kuwakubali qanaoenda tofauti nayo na ku challenge maoni fulani ambayo yanaonekana kuwa kweli kama injili.
Kwa sababu kushikilia maoni ya jamii kwa sababu ni ya jamii tu kungetufanya tuamini dunia ni bapa na inazungukwa na jua mpaka leo.
usikariri kila kitu kinahitaji mabadiliko vingine ni maagizo kutoka kwa muumba mbingu na nnchi huku duniani ni utekelezaji wake tu mfano NDOA ukienda kinyume huendi kinyume na jamii tu bali mungu pia
NB
isipokuwa kwa wasioamini ambao ni 1% kati 99%