Hili ni moja kati ya matatizo yetu makubwa Wabongo.
Kila kitu tunafanya kwa kuangalia jamii.
Ukitaka kumpendeza kila mtu maana yake hutampendeza kila mtu.
Hata huyo mzuri hajulikani yukoje, utakayemyona wewe mzuri, mwingine atamkosoa.
Mwingine anaona kimbaumbau ndio mzuri, mwingine anaona tipwatipwa ndio mzuri, mwingine anaona shorty ndio mzuri, mwingine anaona super tall ndiye mzuri.
Sasa katika.mazingira kama hayo ambayo hayana jibu moja la "mzuri", suala la uzuri aa hiwe muoaji, kwani yeye ndiye atakayeamka kila asubuhi akimuangalia mke wake.
Nyie wengine ni wapiga domo tu.
Mwanamme wa shoka hawezi ku criticize uzuri wa mke wa mwanamme mwingine.
Labda vivulana visivyojua siri za ndoa wala kwenda jando hata la kiakili tu.