Ah mkuu JMali salama kiongozi? Nilishangaa kutokukuona kwenye mjadala huu. Vema. Unasahau kuweka bayana chanzo cha RPF/RPA kushambulia Rwanda, ama kwa kutokujua ama kwa makusudi (most likely kwa kuwa wewe ni muelewa). Sio siri kuwa serikali ya Habyarimana ilikuwa ina "wahutu" wenye mrengo mkali ambao ndio walikuwa wasimamizi na watekelezaji wakuu wa sera za kibaguzi. Sio siri ya kuwa "watutsi" waliokuwa Rwanda chini ya Habyarimana walikuwa ni raia wa daraja la pili. Kulikuwa na state sanctioned persecution against the "tutsi". They were ostracized from all levels of government and business. Hili halina ubishi. Refugees waliokimbia genocide ya miaka ya sitini na sabini walinyimwa haki yao ya kurudi Rwanda. And so, the gist of what I want to say is the RPF/A's push into Rwanda was a righteous prerogative move for a people denied of their basic right of citizenship in their own fatherland. I liken it to Aaliyah. Suala la watu kufa vitani sio geni but it was not as systematic as the deliberate and selective massacres carried out by the FAR against "tutsis" and moderate "hutus". You must understand that the RPF/A consists of both "hutus" and "tutsis". In fact it has always been RPF/A policy to have both "ethinicities" down the unit level. Unafikiri "hutus" walio RPF/A wangekubali kuona wenzi wao wanauawa bila hatia?
Always tutatofautiana katika malengo ya RPA/RPF, so lets not go there it would be a waste of our time. The FACTS are these.
1. RPA kilikuwa ni kikundi cha waasi ambacho hata malengo yake yangekuwa mazuri namna gani (kama ulivyowatetea), kwa mujibu wa international community walichokuwa wanakifanya hakikukubalika! Ndio maana wenye akili (Tanzania) tukaweka mezani pande zote mbili kwa MAZUNGUMZO.
2. watutsi waliokimbia Rwanda in the 60's hawakukimbizwa na Habyarimana, in fact most of them waliondoka wenyewe. Swali la kujiuliza (naamini unajua jibu) ni kwa nini watutsi hawa wachache walikimbia?
FACT ni kwamba majority ya kabila la watutsi wako RWANDA siku zote. since time immemorial, ukihesabu wanyarwanda watutsi dunia nzima, majority yao wako RWANDA, that
FACT has never changed! So you see haiingii akilini kuwa eti watutsi walifukuzwa au walikimbia genocide, wakati majority yao iko kwenye hio hio nchi.
Ukweli ni huu: mapinduzi yalipindua ufalme wa kitutsi na kuleta uongozi wa kidemokrasia ambao given the demographics lazima hata leo hii uwe na majority wahutu. watutsi waliokimbia walikuwa ni wale vigogo ambao walikuwa kwenye system ya ufalme.
FACT: kagame mwenyewe ni kabila la wafalme ambae ukoo wake ndio unatoa malkia. Hawa vigogo ndio waliokimbilia Uganda na kwingineko kwa kutokubali mabadiliko sio kwa kunyanyaswa. Although in fair-ness kulikuwa na manyanyaso ya kulipa visasi toka kwa wahutu, but they were more likely as a result of sera maalum za ku-redress inequality iliyotengenezwa na ufalme wa kitutsi kwa miaka zaidi ya 400.
Mfano: katika ufalme wa kitutsi, wahutu hawakutakiwa kwenda shule, shule ilikuwa ni kwa ajili ya watutsi tu. Ili kubadilisha hilo serikali ya kihutu ikaweka asilimia kubwa kwa wahutu na ndogo ya watutsi katika nafasi za watoto kuingia shule. Ikatumia vitambulisho ili kuhakikisha wahutu waliokuwa wamenyimwa fursa wanapata nafasi zaidi. Hii haikuwa na lengo la kulipa kisasi bali lengo lilikuwa kuleta usawa tu. btw, mimi nakubaliana na idea, lakini sikubaliani sana na mfumo uliotumika. All in all hii concept iko dunia nzima, aliyeonewa anapewa upendeleo. hata sisi TZ tulitaifisha ili watu wote wamiliki, South Africa walikuwa na BEE policy, hivyo Rwanda ilikuwa na system yake ya kipekee (though not perfect).
Lakini wakina kagame kwa kuwa wao walikuwa wafalme hawakukubali hilo, wakataka usawa wakati wanajua fika kwamba wao ndio wangetawala.
Na kama haitoshi serikali ya Habyarimana ilishakubali kushare nao madaraka pale Arusha. Kama ndege isingetunguliwa maana yake ni kuwa kagame na jeshi lake wangekuwa integrated Rwanda na maisha yangeendelea. kwa kujua kuwa katika mfumo huru wa kidemokrasia watutsi hawawezi tena kuwa wafalme, mambo ndio yakawa kama yalivyotokea. Sasa historia ya vita vya miaka minne inafutwa, badala yake tunalazimishana kuanzia historia ya Rwanda kwenye 'genocide'. kama kagame alistopisha genocide si angeishia hapo halafu akarudi kwenye Arusha accord? NO, badala yake anacriminalize the entire army kwa uhalifu wa genocide, ili majority ya wanyarwanda ambao ni wahutu wasiwe na jeshi, watu pekee wenye bunduki rwanda wawe ni watutsi.
Na hili ndio tatizo lake na FDLR. FDLR ndio lile jeshi la nchi halali ya Rwanda, hawa wakirudi focus itakuwa ni yale mazungumzo ya Arusha, ambayo yatalazimisha uchaguzi wa kidemokrasia na sio udikteta.
Ingawa Tanzania hatuna ukabila mtu yoyote mwenye common sense atapata tabu kuamini eti wanyarwanda ambao zaidi ya asilimia 80 ni wahutu wamchague kagame kwa asilimia 90 given historia ya kagame kuwauwa kwa miaka minne na kusababisha genocide. Ni kama vile udai kuwa endapo M23 wangechukua nchi ya DRC, wangechaguliwa kidemokrasia kwa asilimia 90 katika uchaguzi na wacongomani wale wale waliokuwa wanapigana nao! The only way hilo lingewezekana ni pale tu jeshi halali la congo lingekuwa mafichoni nje ya nchi.
Mimi nakuambia ukweli siku FDLR wakifanikiwa kurudi Rwanda kwa mtutu utashangaa jinsi wanyarwanda wanavyogawanyika kwa ututsi na uhutu. Hii ni kwa sababu Kagame hajawahi kuwaunganisha, the only chance for true unity ilikuwa mazungumzo ya Arusha! Huu unyarwanda wa leo ni woga tu kwa kuwa jeshi zima ni watutsi, hakuna mhutu anayeweza kuongea kwa uhuru.