Hivi ni kwanini Tanzania tunaleta chokochoko kwa Rwanda? Ushauri alioutoa Rais Kikwete kwa Rais Kagame ulikataliwa kwa kuwa haukuwa na mashiko. Sasa kwa nini mnalazimisha mtu akubaliane na "ushauri"?? Mjiulize silaha wanazotumia FDLR zinatoka wapi na kupitia bandari gani? Hivi mnataka Kagame akae anawachekea tu wakati mko pamoja na waasi wanaotaka kuipindua serikali halali ya Rwanda? Je, ni kweli ama si kweli kuwa Twagiramungu and other genocidaires walikuwa hosted na serikali ya Tanzania? Hapa tuache hisia, tujadili masuala kama wasomi. Patriotism does not mean you blindly defend the indefensible.
Mtu akihoji huu ushirika na wahutu wenye mrengo mkali, mnamuita M-tutsi hata akiwa mkurya kama mimi. Ukweli utabaki pale pale kuwa Rais Kagame ana kila haki ya kutetea na kuilinda nchi yake dhidi ya wauaji ambao mpaka leo wanaona mauaji waliyoyatekeleza yalikuwa halali na bado wangali na mpango wa kuwamaliza watutsi wote na wahutu waliostaarabika. Tanzania has no business propping up the DRC and their FDLR genocidaire surrogates. Nauliza mandate ya MONUSCO kushambulia waasi wa FDLR itatekelezwa lini? Mlikuwa wepesi kushambulia majeshi disciplined ya M23 ambayo yalikuwa yakilinda raia na minorities in Eastern DRC against pillaging, rapes, looting and murders in the hands of the ragtag FARDC. Kuna makundi zaidi ya 17 Eastern DRC ila mkaona ni M23 tu wa kushambulia. Mbona hao wengine hasa hasa FDLR hamuwashambulii? Acheni unafiki, nia yenu ni kumpindua Rais Kagame ili muwaweke wauaji wa FDLR madarakani.