Kwa suala ka Twagiramungu Dar walishalisema nadhani unakumbuka taarifa ya ikulu ila kwa mimi navyohisi hata kama walikuja hapa ni swali la Kigali kuuliza Tz kupitia ubalozi wao iliopo hapa Dar.
Tanzania nahisi siku zote wanapenda mazungumzo kwanza ndo maana hata Kagame alivyokuwa muasi Tz ilikuwa mediator wakati huo na tulofanya vivyo hvyo kwa wenzetu wa Bujumbura.
M23 kulikuwepo na mazungumzo nadhani yalikuwa chini ya Rais Museveni ,yaliposhindikana UN ikaamua watumike vikosi vyake na vikosi vyake vimetoka kwa wanachama SADC ambapo DRC ni mwanachama pia.
Kiongozi Robert nakubaliana na wewe kuwa kutoa ushauri wa mazungumzo kwenye conflict resolution ni njia moja ya kuleta mapatano. Lakini ushauri lazima uwe genuine. Usinipe ushauri wa kuongea na adui yangu wakati unampa support ya hali na mali huyo huyo adui yangu. Nikilijua hili ni lazima nikasirishwe kwa kuwa ushauri utakuwa wa kinafiki. Pili, waasi wa FDLR hawana nia ya kuzungumza, wao wanataka revenge na continuation of the genocide. Sioni hatia juu ya Rais Kagame kwenye hili. Nadhani yeye si mjinga kwa kuwa anawajua vema maadui zake hawa.