hapo sijakuelewa, kwani mwanzoni kabla hajalipa mahari hukuziona hizo tabia, alafu hapa inakuwa ngumu mana hatujui vigezo ulivyoweka wewe kuwa hakufai ni vipi, ni malaya, mchafu au ..........? angalia mapungufu na mazuri yapi yamezidi, usije ukamuacha alafu ukaingia kubaya zaidi, shetani umjuaye ni bora kuliko malaika usiemjua, swali lingine, je ulimshirikisha Mungu wakati unatafuta mchumba? kwa imani yeyote uliyonayo muombe Mungu akusaidie kwa akili za binadamu ni ngumu lakini kwa Mungu yote ya yanawezekana, kumbuka mke/mume mwema anatoka kwa Mungu.