Jamani mbona vitu vimepanda ghafla

Hahaa aisee....basi ngoja tukanunue ugali mboga itakua madege hayo kwenye bakuli
Jamaa yangu wewe ni mpiga dili ulizoea dili, mshahara unatosha sana haina haja kuongeza na wengine tunawapunguzia..

Wewe huoni midege inatua Chato pale, SGR, stiggler, shule bureee, ATCL imetua SA, uchumi unakua kwa 7% na umasikini umepungua, awamu ya tano inapiga kazi balaaa
 
Yaani in balaa apa iringa nyanya3 kwa 500... Nguo ndo kabsaa hugusi...twafwaaaa
 
Kuna ukweli hapa

Plain Papers 3 ilikua Tsh. 100 ila sasa kuanzia j3 Plain Papers 2 ndo hiyo Tsh. 100

Kutoka Jalalani Stationeries
 
Hahaa aisee....basi ngoja tukanunue ugali mboga itakua madege hayo kwenye bakuli

Acha uvivu wewe, huo ugali ulionunua uliwezaje kuununua ushindwe kununua mboga, lakini sio lazima pia ule ugali na hapa ndipo inaonyesha namna ulivyoshindwa kuwa na kipaumbele.. Kuwa vegetarian tu mkuu achana na ugali huo nunua mchicha uchemche na maji ya bomba utafune shushia na ndizi mbili mbivu maji glasi mbili hapo poa kabisa tena diet ya uhakika kabisa hiyo.
 
Mwanamme hakimbii matatizo bali hupambana nayo labda vinginevyo utakuwa wakike....
Kweli ndio mana wanaake wengi wanaenda ulaya na uropa kutafuta maisha sisi wanaume tupambane tu hapahapa.
 
Watanzania mtembee vifua mbele we a on the LAIT TLAK. Ilani ya chama inaenda vizuri.
😳😳😳😳😳

Wakuu habari zenu poleni na majukum ya kitaifa

Kuna jambo limenishangaza sana mbona maisha yanazidi kupanda sana toka tarehe moja nimeenda dukani kununua sukari kilo moja kwetu huku ilikuwa tsh 2600 sasa hivi imefika 2800

Bati pia hivyo hivyo bando moja hizi za rangi nimekuta bei imepanda toka 370000 mpk 390000

Hizi za kawaida simbadum zimepanda toka laki mbili themanini mpaka laki tatu na arobaini.

Cement nayo imepanda hatari jamani tunaelekea wapi sasa mbona hatari hii kwa wafanyakazi kipato bado kile kile pia wafanyabiashara hali ya biashara ngumu

Hii hali hii mbona umri unaenda hatufanyi lolote la maana kwa ajiri ya watoto wetu zaidi ya kujibana kula na kuvaa napo kwa shida.
 
Tunyooshe babaa maguu,watu walizoea sana kuichezea serikali na wengine kujiita mapedejeee,kanyaga hapohapo baba magu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom