JAMANI KWANI LAZIMA?-24
ILIPOISHIA
Utamuuliza mkiwa wenyewe. Tena mimi naondoka zangu, yangu yalikuwa hayo tu, alisema mama Jumanne na kuondoka zake. Ye alishalisanua basi, roho yake ilikuwa kwatuu!
Stela, aliita Paulina kwa sauti ya ukali
Abee mama.
Njoo haraka sana.
JIACHIE SASA
tela alifika sebuleni na kuukuta uso wa bosi wake huyo ukiwa umebadilika rangi kwa hasira
Ulikuwa na nani?
Wapi mama?
Ulikotoka.
Si na wenye mimba wenzangu.
Stela, aliita Paulina.
Abee mama.
Unataka kunidanganya mimi, wewe hukuwa gesti?!
Stela alishtuka kusikia hivyo, akainamia chini
Nani amekwambia mama?
Hukuwepo, ulikuwepo? aliuliza Paulina kwa sauti iliyojaa ukali zaidi
Nilikuwepo, alijibu Stela bila kumwangalia bosi wake huyo
Na nani?
Wakati Paulina anauliza na nani, kichwa kilianza kumvurugika akihisi jibu la Stela litakuwa ni na baba.
Moyoni aliomba jibu hilo lisiwepo katu kwani aliamini angeweza kupiga mwereka na kupoteza fahamu.
Na mtu mmoja.
Nani? Nani? Hana jina?
Huwezi kumjua mama.
Mimi nisimjue mtu wa hapa mtaani? Anaitwa nani?
Hakunitajia jina.
We ulivyoondoka hukuongozana na mume wangu?
Akha! Mimi nilimwona kwa mbele tu, alijibu Stela na kutoa wasiwasi zaidi kwa Paulina kwani alikumbuka kwamba, Stela ndiye aliyetangulia kutoka, akafuatia mumewe
Ilikuwaje umuone kwa mbele wakati yeye aliondoka baada ya wewe kuondoka?
Mimi sijui sasa ila nilimwona kwa mbele halafu sikumwona tena.
***
Jioni mume wa Paulina alirejea, alimkuta Paulina amekaa sebuleni kwa mawazo
Za saa hizi? alisalimia mumewe na kupitiliza chumbani.
Paulina alimfuata mumewe chumbani
Samahani, nimeletewa siri za msichana wa kazi, alisema Paulina.
Kwamba?
Ameonekana akitoka gesti leo asubuhi wakati aliaga anakwenda kliniki.
Sasa siri iko wapi hapo?
Ha! Si amejulikana tabia yake!
Mi nilidhani tabia yake ilishajulikana baada ya kupata mimba.
Paulina alichoka kwa jina la mumewe, akajikuta hana la kusema
Sasa mtu tayari ana mimba, akionekana anaingia au anatoka gesti ajabu yake ni nini?
***
Mimba ya Stela ilizidi kukua, sasa ilifikisha miezi saba. Siku hiyo, Paulina akaamua kumfuata muuza genge ambaye Stela alimtaja kuwa ndiye mwenye ujauzito huo
Hujambo kijana?
Sijambo, shikamoo anti.
Marhaba. Nataka kujua una mpango gani na ile mimba ya msichana wangu wa kazi? Paulina alisema kwa ukali kidogo
Khaa! Anti unavyoniuliza hivyo una maana gani?
Nina maana gani? Yaani sisi ndiyo tukulelee mimba ile we unakula bata tu.
Ah! Mnilelee mimba kwani mimi ndiye niliyebeba?
Kwani wewe si ndiyo umesababisha!
Kivipi, mbona sikuelewi?
Ile mimba ni ya nani?
Anayejua ni nani si yeye mwenyewe.
Hajakwambia kwamba ana mimba yako?
Mimba yangu? Anti mbona sikuelewi.
Kwani hujui kama ana mimba?
Sasa mimi nahusika na nini na mimba yake?
Alisema ya kwako!
Mimi? Mbona sijawahi hata kumtongoza! Hiyo mimba nilimpajempaje?
Paulina alionekana kushtuka sana kwa maneno ya muuza genge hilo
Ina maana wewe na Stela si wapenzi?
Wala! Mimi sijawahi kuzungumza neno lolote linalohusu mapenzi na msichana wako wa kazi.
Wakati muuza genge huyo anamaliza kusema, Stela alitokea akiwa amekwenda kununua mahitaji mbalimbali
We Stela unasema mimi nimekupa mimba, lini?
Kwanza Stela mwenyewe alishtuka sana kumwona bosi wake pale gengeni. Alipoongezewa na hilo la mimba ndiyo kabisa. Alionekana akitetemeka waziwazi
We si unaulizwa wewe? Paulina alidakia.
Ndiyo naulizwa mimi.
Sasa mbona hutoi majibu?
Stela alibaki kushangaa tu! Aliilaani miguu yake kwa kukanyaga hadi pale gengeni bila kujua kuwa bosi wake alijaa tele
Hebu sema ukweli hapahapa gengeni! Muuza genge ni huyu, ulisema ndiye mwenye hiyo mimba lakini mwenyewe anasema hajawahi kukutongoza hata siku moja Stela. Je, hiyo mimba ni ya nani?
Dada nisamehe sana.
Nikusamehe kwa lipi?
Nilifundishwa kwamba kama nikiulizwa mimba ni ya nani nimtaje huyu kijana anayeuza genge.
Ulifundishwa na nani?