JAMANI KWANI LAZIMA?-29
ILIPOISHIA
Baada ya Stela kuzima taa ya chumbani tu, mume wa Paulina hakuona kama kuna sababu ya kusubiri kuanza kwa ligi mzunguko wa pili ambapo alianza kwa kumbusu Stela, akamtekenya, akamuomba denda na kufuatiwa na kumvua nguo zote na kuzitupa chini.
JIACHIE SASA…
"Jamani," alisema Stela akirukaruka kitandani…
"Nini tena?"
"Unanitekenya."
"Unaumia?"
"Siumii wala."
"Sasa?"
"Najisikia vibaya."
"Na tumbo au?"
Stela alicheka kidogo akamlalia bosi wake kifuani…
"Baby, hivi nini hatima ya maisha yangu na hiki kitoto chako tumboni?" aliuliza Stela…
"Mimi ndiye baba wa mtoto, tulia uzae, tulee mtoto wetu."
"Ni kweli mkeo ataondoka?"
"Lazima aondoke."
"Lini?"
"Nitakwambia, wala usiwe na wasiwasi."
"Naishi kwa tabu sana, mkeo mkali sana, ana majibu mabaya kwangu, ananichukia. Najua anaamini mimba hii ni ya kwako."
"Kwa kigezo gani?"
"Si ninavyomkatalia kumtaja mhusika."
"Itafika wakati hata akijua mimi sitakuwa na shida yoyote ile. Unajua kuwa bado naumia sana kuhusu baba Riziki kudai ile mimba ni ya kwake. Hivi alipata wapi ujasiri wa kufanya vile? Na kama ni kweli, baba Riziki alipata wapi ujasiri wa kutembea na mke wangu na hata mke wangu alipata wapi ujasiri wa kutembea na baba Riziki?"
"Najua unaumia sana baby, lakini jipe moyo kwa sababu siku zote Mungu ndiye anayepanga mipango," alisema Stela huku akimpapasapapasa kifuani baba mwenye nyumba huyo.
Ilifika hatua mwanaume huyo alianza kulia kwa mbali huku Stela akishangaa…
"Baby, usilie."
"Lazima nilie baby, mke wangu ameniaibisha sana. Ngoja kukuche utaona nitakachokifanya," alisema mwanaume huyo na kunyamaza huku Stela akimfuta machozi kwa shuka.
Stela aliamua kupotezea mazungumzo ya bosi wake ambayo yalionesha kumsumbua kichwani na kuanza kumfanyia utani mbalimbali huku akimtekenya ili kumpa moto wa mahaba…
"Ooo! Baby, naona unanipatia sana…ohoooo," alilalamika kimahaba mume wa Paulina…
"Hata wewe baby unanipatia sana jamani mpaka umenipa mimba."
"Mimba ni haki yako wewe kama mwanamke."
"Asante baby," alishukuru Stela huku akiendelea kumpapasa kifua baba wa mtoto wake mtarajiwa.
Hali hiyo walikwenda nayo hadi ikafika wakati wakajikuta wanazama kwenye mahaba. Stela pamoja na tumbo lake alijitutumua kwa staili mbalimbali huku kitanda kikilalamikia kuhenyeshwa na kutoa mlio wa kuumizwa…"Kwacha…kwacha…kwacha…" kitanda kililia hivyo.
***
Paulina alishtuka kutoka kwenye usingizi wa mang'amng'amu, akajiuliza kuhusu Stela…
"Hivi ni kweli ile mimba Stela hataki kuniambia ni ya nani?"
"Mimi naamini ni ya mume wangu na ndiyo maana anamtetea sana."
"Lakini mfano nikimshikia kisu na kutishia kumchoma nacho bado hataniambia ni mimba ya nani?" alijiuliza Paulina, akashuka kitandani akiwa amekasirika. Akiwa ndani ya gauni la kulalia, akatembea hadi mlangoni, akafungua na kutoka hadi jikoni ambako alichukua kisu.
Alipofika mlangoni kwa Stela alisimama ili kugonga mlango. Alishtuka kusikia mlio wa kitanda…
"Kwachu…kwachu…kwachu…"
"Mh!" aliguna Stela…
"Ina maana kuna mwanaume?"
"Atakuwa nani?"Mlio wa kitanda ulishika kasi bila kusikika sauti ya mihemo au mtu kulalamika kimahaba…
"Ni Stela kweli peke yake? Haiwezekani. Kama ni peke yake kwa nini kitanda kinalia hivi, ina maana anacheza kitandani mwenyewe?"
"Kwachakwachakwachakwacha," sasa mlio wa kitanda ulichanganya kwa vile mume wa Stela alikuwa anafika kwenye malengo yake ya kimahaba, lakini bahati nzuri hakutoa sauti ya juu, alimjulisha Stela kwa sauti ya chini kwamba anavunja dafu akakubaliwa kulivunja.
"Stela," aliita Paulina.
"Mungu wangu, mama huyo," Stela alisema kwa sauti ya chini sana.
"Tulia, usipaniki," mume wa Paulina alimwambia Stela`.
"Stela," abee mama."
"Fungua."
Mume wa Paulina kwa vile alitambua lengo la mkewe ni kuingia ndani ya chumba na yumo na hakukuwa na sehemu sahihi ya kujificha, alisimama juu ya kitanda na kuchomoa balbu."
"Kafungue mlango," alisema huku yeye akizama chini ya kitanda.
Stela alifungua mlango, akazama ndani…
"Washa taa."
"Taa ilipasuka mama."
Stela hakuamini, alipeleka mkono ukutani na kuwasha lakini hakukuwa na mwanga wowote.
"Upo na nani humu chumbani?"
"Mama bwana! Sasa unadhani mimi nitakuwa na nani?"
"Kwani huwezi kuingiza mwanaume?"
"Mama giza limeingia tuko wote, tena wewe ndiye uliyefunga mlango mkubwa, huyo mwanaume kaingiaje?"
Paulina alikwenda kitandani na kupapasa sehemu yote akiamini anaweza kushika mtu…
"Sasa mbona kitanda kilikuwa kinalia kwachu kwachu, ilikuwa ni nini?"
"Labda nilipokuwa nageuka mama maana kuna joto sana, jasho mwili mzima na hii mimba ndiyo kabisa."
"Stela."
"Abee mama."
"Nimeshika nini mkononi?"
"Mi sioni sawasawa."
"Huoni sawasawa? Hebu shika hapa."
Stela alipeleka mkono na kushika kisu."
"Umeshika kisu mama."
"Kisu?"
"Ndiyo mama."
"Sasa naomba nikwambie kitu. Kama leo, usiku huu, humu chumbani mwako hutaniambia mwenye mimba hiyo ni nani, nakuua kwa kukuchoma na hiki kisu, niambie nani amekupa mimba?"