Jamani, kwani lazima?

Daudi1

JF-Expert Member
Dec 14, 2013
8,799
8,705

Mtoto utapata ila lazima ufuate masharti yangu."
"Babu siamini kama kweli nitapata mtoto maana huu ni mwaka wa saba sasa niko kwenye ndoa lakini sijapata mtoto, niko tayari kwa masharti yako babu, okoa ndoa yangu, ndugu wa mume wangu wananisema sana."

"Je, unaweza kumjua mwanaume atakayekupa hiyo mimba?"
"Simjui babu.""Basi safari hii utampata tu."

"Kwanza lazima awe mume wa mtu halafu siku ya kukutana avae shati jekundu, sawa?"
"Sawa! Shati jekundu je suruali, au hata akivaa ya jinzi?"
"Suruali hakuna neno. Nazungumzia shati tu."

"Sawa," alijibu Paulina huku akianza kumfikiria kila mwanaume anayemjua ni mume wa mtu.
"Kuna baba Anna, baba Riziki, baba Sarah, baba Kibibi, wapo wengi tu."

Hao wanaume wote aliowawaza ni majirani mtaani, mmoja baba Kibibi ni rafiki mkubwa wa familia, yaani familia ya baba na mama Kibibi iko kilozidi na familia ya Paulina na mume wake, Madale.

"Enhee! Kwa hiyo wewe mimba yako itatungwa kwa kukutana kimwili na mwanaume wa aina hiyo. Lakini hilo ni sharti la kwanza, la pili ni lazima awe mwanaume mweusi, anayependa kufuga ndevu."

Hilo pia kwa Paulina halikuwa sharti kubwa sana kwake kwani wanaume wote walioingia kichwani mwake, ni mumewe tu ndiyo mweupe.

Alipomalizana na mganga, aliondoka na shoga yake Hawa ambaye ndiye aliyempeleka kwa mganga huyo anayejulikana kwa jina la mzee Kavarando…
"Sasa shoga, mbona mganga amekupa masharti magumu sana?" Hawa alimuuliza Paulina.
"Kama lipi?"

"Mimba kupewa na mume wa mtu, sasa si anamaanisha lazima usaliti?"
"Ah! Sasa Hawa unadhani nitafanyaje?""Haya, halafu anasema lazima awe mwanaume mweusi na awe na ndevu nyingi, sasa wewe utamtafutia wapi mwanaume wa hivyo?"

"Namwomba Mungu anisaidie kwa kweli," alijibu Paulina kwa sauti iliyoashiria kwamba hakuwa anapenda maswali ya shoga yake huyo maana moyoni alisema…"Wewe si umeshanileta sasa maswali yote ya nini?"

"Ni kweli umwombe Mungu sana," alisema Hawa huku moyoni akimshukuru Mungu hana mume maana alianza kuona usaliti wa waume za watu kutoka kwa Paulina ili apate mtoto.
***
Usiku wa siku hiyo, Paulina alilala huku akiwa mwenye mawazo kibao. Alimfikiria mwanaume mmojammoja ambaye aliamini anaweza kufanya naye tendo la ndoa ili apate mtoto kama alivyoambiwa na mganga.


Heri ya mwaka mpya, ni mwaka mwingine tena tunakumbushana juu ya uaminifu katika mahusiano yetu, udhaifu wowote alionao mwenzi wako isiwe sababu ya kutoka nje ya mahusiano ni heri ukaachana naye kila mtu ana mapungufu yake sisi ni binadamu, kama unatafuta basi tafuta mwanamke/mwanaume wa vigezo vyako ili usiwe na sababu ya kutoka nje ya ndoa, mambo mengine ni majaaliwa ya Mungu mwenyewe.

Kwa hisani ya GLOBAL PUBLISHER tupate mafunzo kupitia hadithi

Tuwemooo.
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-2

ILIPOISHIA
Usiku wa siku hiyo, Paulina alilala huku akiwa mwenye mawazo kibao. Alimfikiria mwanaume mmojamoja ambao aliamini anaweza kufanya nao tendo la ndoa ili apate mtoto kama alivyoambiwa na mganga. Endelea nayo
"Mh! Baba Kibibi ndiye rahisi sana kumpata lakini wale wengine ni shida! Kwanza nitaanzia wapi!
"Ila baba Kibibi na zile ndevu zake nadhani mganga alinipatia sana kunipa masharti mepesi kama yale," alisema moyoni Paulina.

***
Kulipokucha Paulina alitoka kitandani akiwa na utayari wa moyoni kwamba akikutana na mmoja wa wanaume wenye sifa alizoambiwa lazima ajigonge kwa makusudi ili kunasa.
Alitoka kwenda dukani, njiani akawa anaangaza macho huku na kule akiamini atamuona mwanaume mwenye sifa anazozitaka.

Paulina alishtuka sana kugundua kwamba kumbe hata muuza duka alilokwenda anaitwa Masawe ni mweusi, ana midevu mpaka basi…
"Masawe nipe sukari kilo moja, mkate wa leoleo na sabuni ya kuogea.
"Halafu hivi Masawe una mke wewe?" aliuliza Paulina…
"We umekuja kununua vitu au umekuja kujua kama nina mke au sina?"
"Vyotevyote Masawe."

"Basi fuata moja ijulikane."
"Kweli Masawe mi nataka kujua tu, niambie ukweli, una mke?"

"We nanihii, mimi sitaki maswali yako ya mitegomitego," alisema Masawe kwa Kiswahili chenye lafudhi ya kuleee! Moshi!
Licha ya kuhudumiwa, Paulina hakuondoka akazidi kumtaka Masawe aseme ukweli wake…
"Kwani nikiwa nimeoa au sijaoa unataka nini? Unataka kunitafutia mke wewe au?"
"Ndiyo."

Masawe alicheka sana, akaja mteja mwingine ndipo Paulina aliondoka. Lakini kabla hajafika nyumbani kwake, alikutana na mama Mage. Baada ya salamu tu, Paulina akamuuliza…
"Hivi mama Mage, yule Masawe wa lile duka la kona ana mke?"
"Mh! Mimi unadhani nachunguzaga mambo ya watu basi, kwani vipi?"
"Nilitaka tu kujua!"

"Kujua nini sasa, wewe si una mume?"
"Sina maana mbaya lakini."
"Haiwezekani ukawa na maana nzuri, wewe mumeo akisikia unatafuta kujua uhusiano wa mwanaume mwingine si mtagombana sana?"
"Hawezi kujua."

"Haya, lakini mimi sijui."
Waliachana, Paulina akiwa anakaribia kufika kwake, alikutana na baba Riziki akiwa anakwenda kazini kwake…

"Za leo shemeji?"
"Nzuri shemeji, mmeamkaje?"
"Hatujambo, naona unakwenda kazini sasa?"
"Ndiyo shemeji, kumekucha."

"Haya, kazi njema shemeji, sisi tupo bwana, kumekucha sasa kwa hiyo tunaangalia maisha yanakwendaje!" Paulina aliongea sana kiasi kwamba, siku hiyo baba Riziki akashangaa imekuaje, maana licha ya kumfahamu lakini si kawaida yake…
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-3

ILIPOISHIA
"Haya, kazi njema shemeji, sisi tupo bwana, kumekucha sasa kwa hiyo tunaangalia maisha yanakwendaje!" Paulina aliongea sana kiasi kwamba, siku hiyo baba Riziki akashangaa imekuaje, maana licha ya kumfahamu lakini si kawaida yake…
SEREREKA NAYO MWENYEWE…

Hapo walikuwa bado wamesimama wakiendelea kuzungumza…
"Sawa shemeji yangu, nisalimie familia, mzee na watoto pia," alisema baba Riziki licha ya kwamba alijua kuwa, Paulina hana mtoto hata mmoja achilia mbali watoto.
Paulina akaanza tena…

"Aah! Shemeji yangu wee, watoto wapatikane wapi? Ndiyo nahangaika sasa kutafuta, sijui Mungu atanisaidiaje? Lakini pia nategemea zaidi na misaada yenu nyie mashemeji zangu."
"Shemeji we mwombe Mungu tu, atakusaidia. Lakini shemeji kuna daktari mmoja ni mtaalam sana kwa wanawake wenye hali kama yako," alisema baba Riziki.

"Yupi huyo shemeji? Anaishi wapi? Anapatikanaje?" aliuliza maswali mengi Paulina.
"Mmmh! Anaishi Mikocheni, anaitwa Dokta Paul."
"Labda shemeji ungenipa namba yake na yako pia."

"Oke," baba Riziki alianza kwa kuzitaja namba zake kisha akamalizia na za Dokta Paul.
Wakaagana na kuondoka, baba Riziki alitembea kwa hatua kadhaa, akageuka nyuma kumwangalia Paulina lakini huku akiwa na tahadhari kubwa kwamba asije naye akageuka wakakutana macho…

"Lakini ana hoja!" alisema moyoni baba Riziki akiwa anatembea huku bado anamwangalia mwanamke huyo. Ghafla, Paulina naye akageuka kumwangalia baba Riziki, wakakutana macho, baba Riziki akakimbiza kichwa mbele, Paulina akachekea moyoni…

"Da! Kumbe na yeye alikuwa ananiangalia, baba Riziki bwana. lakini leo ni mara ya kwanza mimi na baba Riziki kuzungumza tukiwa tumesimama, mara nyingi inakuwa juujuu tu," alisema moyoni Paulina.

***
Baada ya kumaliza kazi zake za ndani siku hiyo, Paulina alikaa na kuanza kuwasiliana na Dokta Paul…
"Yeye Paul mimi Paulina," alisema moyoni akiwa anaseti namba, akampigia. Simu yake ilipokelewa upande wa pili na Dokta Paul mwenyewe ambapo alijitambulisha kisha akasimulia tatizo lake la msingi…
"Oke….oke oke…pole sana…sasa kwa tatizo hilo inabidi tuonane hospitalini kwangu siku ya Alhamisi saa kumi jioni ndiyo huwa nahudumia akina mama," alisema Dokta Paul…
"Sawa dokta, nitakuja."

Baada ya kukata simu, Paulina alisema moyoni…
"Ungejua nimeshakutana na madaktari kibao mpaka wale wakware lakini hamna kitu. Ninachotaka mimi ni mwanaume mweusi, ana midevu kama Osama na awe amavaa shati jekundu basi, labda uwe na wewe una sifa hiyo ya mganga wangu."

Aliiseti tena simu yake na kumtwangia baba Riziki sasa ambaye ndiyo chanzo cha msingi kwake…
"Haloo," baba Riziki alipokea kwa sauti nzito, ya kiume bila kumjua mpigaji maana namba ya Paulina hakuichukua muda ule…
"Shem, Paulina hapa…"

"Ooo! Shemeji, vipi ulimpigia Dokta Paul?"
"Ndiyo shemeji, ndiyo nimetoka kuwasiliana naye muda huuhuu…"
"Amesemaje?"

"Amesema niende Alhamisi jioni ya saa kumi ndiyo huwa anahudumiaga watu wenye hali kama yangu."
"Oke oke, si utakwenda shemeji?"
"Nitakwenda shemeji, mimi tena!"
"Basi sawa shemeji."

"Sawa shemeji, nilisema tu nikupe taarifa."
"Sawa shemeji."
"Lakini shemeji jambo moja please, huu mkakati wangu naufanya kuwa siri, mume wangu hajui. Kwa hiyo naomba usimwambie kitu shemeji!"
"Oke! Lakini si mista anatakiwa kujua?"

"Noo! Atajua mambo yakianza kuwa mazuri."
"Sawa, tufanye nimekuelewa shemeji."
"Nashukuru sana."

Baada ya kukata simu, baba Riziki akabaki na maswali kibao…
"Sasa mwanamke anatafuta ujauzito lakini hataki mume ajue! Mh! Huo ujauzito anamtafutia nani?" alijihoji baba Riziki…
"Wanawake wengine bwana," aliishia kusema hivyo.

***
Kwa upande wake, Paulina baada ya kukata simu alijisifu kwamba anakaribia kushinda masharti ya mganga wa kienyeji…

"Ina maana…Da! Mimi kiboko! Ina maana nakaribia kumnasa baba nanihii! Sasa siku ikifika akiwa amevaa shati jeusi itakuaje? Masharti mengine bwana, ni shiiida!"
Mchana wa siku hiyo, Paulina akamtumia meseji baba Riziki…
"Yaani shemeji nikifanikiwa sijui nikupe zawadi gani! Teh! Teh! Teh!"
Aliisubiria meseji yake kujibiwa kwa dakika tano, ikaingia ya baba Riziki…

"Mh! Shemeji we unataka kunipa zawadi gani kwani?" baba Riziki naye sasa alijitosa, akaanza kuhisi kama kuna ubwete kwa mwanamke huyo mwenye figa ya namba nane na sura ya kitoto achilia mbali miguu ya haja na midomo iliyoviringishwa vizuri kama pindo la kanga…
"Shemeji bwana! Yoyote ile utakayoipenda wewe."

"Aaa! Shemeji we si ndiyo utanipa zawadi umesema, mimi siwezi kusema, wewe ndiyo mwamuzi…"
"Hamna shemeji, zawadi za siku hizi anayepokea pia ana uhuru wa kusema anayoitaka. Naweza kusema nikupe zawadi ya Big G kumbe unapenda biskuti mwaya!"
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-4

ILIPOISHIA
"Aaa! Shemeji we si ndiyo utanipa zawadi umesema, mimi siwezi kusema, wewe ndiyo mwamuzi…"
"Hamna shemeji, zawadi za siku hizi anayepokea pia ana uhuru wa kusema anayoitaka. Naweza kusema nikupe zawadi ya Big G kumbe unapenda biskuti mwaya!"CHOMOKA NAYO MWENYEWE SASA
…Mmmh! Basi nataka zawadi ya kitambaa cha kujifutia jasho," aliandika baba Riziki kama kumchekesha mwanamke huyo…

"Aaa! Vitambaa unavyo jamani shemeji, kila siku namwona mama Riziki anavifua pale uani kwake."
"Haya! Basi, mkanda wa suruali shemeji."
"Hata hiyo unayo mingi! We chagua kitu ambacho wewe huna ila mimi ndiyo ninacho."
"Kama nini shemeji, labda magauni."
"Magauni si hata wewe unaweza kushona tu shemeji. Kuna kitu mimi ninacho lakini wewe huna hata ufanyeje huwezi kuwa nacho."

"Mh! Shemeji huo kwangu ni mtihani mkubwa, maana sijui ni kitu gani wewe unacho mimi sina. Labda nido."
"Ha! Ha! Ha! Shemeji bwana, kweli ni mtihani mkubwa huo kwako?" aliuliza Paulina huku moyoni akiamini kwamba, baba Riziki hajajua tageti yake ndiyo maana ameshindwa kujiongeza.
"Kweli ni mtihani shemeji, kama ni darasani napata sifuri kwa mia."
Paulina alicheka sana kule aliko, lakini hakuwa tayari kuacha kuchati na baba Riziki, akaendelea…

"Labda tukikutana nitakujuza kwa mdomo nini unatakiwa kukiombea zawadi."
"Mmh! Unataka ugomvi shemeji," alijibu baba Riziki.
"Ugomvi gani tena shem?"

"Ukutane na mimi, wapi kwanza? Unataka yule mgogo wako aniue siyo?"
Mgogo wake alimaanisha mume wa Paulina.
"Wala hakuui! Kwani utamwambia unakwenda kukutana na mimi?"

Baba Riziki alijikuta mwili ukizidi kusisimka kwa meseji za Paulina. Hakuzitegemea wala kufikiria. Amekuwa akimwona mwanamke huyo jirani yake kama aliyetulia na asiyeweza kuchepuka lakini akashangaa meseji zake zote ziliashiria kutaka mchepuko na yeye.
Ilifika mahali alianza kuamini kwamba huenda ametegewa fumanizi ili aingie mkenge. Lakini wazo hilo alilipuuza kwani hakuwa na ukaribu na Paulina hadi kumfanya mumewe amtilie shaka na kumwandalia mtego.

"Siwezi kumwambia, akijua je?"
"Atajuaje? Kama wa kumfanya ajue ni wewe au mimi mwenyewe."
"Haya shemeji, kazi kwako."

"Kazi kwangu kwako shemeji. Mimi si nimesema tukutane ili nikuelekeze zawadi unayotakiwa kuniomba jamani! Sasa mwenye kazi hapo nani kama si wewe."
"Unatakaje kwani?"

"Nataka tukutane shemeji nikuelekeze zawadi unayotakiwa kuniomba."
"Haya, leo au?"
"Hata muda huu shemeji, mimi mbona nipo tu. Nina likizo ya siku ishirini na nane na nimeanza juzi tu."
"Oke, lakini mzee jioni si anakuwepo nyumbani, utatokaje?"
"Ni kweli lakini pia siamini kama tunaweza kukutana usiku, kwani saa kumi na mbili si muda mzuri pia shemeji."

Baba Riziki aliwaza kwa muda, akajishika paji la uso na kuanza kulisuguasugua huku akimwingiza kichwani mkewe mama Riziki kwa jinsi anavyotaka kumsaliti.
"Lakini ndiyo maisha yenyewe haya, nitafanyaje sasa?" alijiuliza baba Riziki huku akiwa hana la kuamua kuhusu muda.
Baada ya dakika tano, Paulina akamtumia meseji akisema…
"Shemeji!"

Baba Riziki akajua meseji ile ilimaanisha kuuliza kwamba, mbona kimya!?
Naye akaandika…
"Yes shemeji!"

"Mbona kimya tena au nikuache uendelee na kazi?"
"Noo! Mimi natoka kazini saa kumi na nusu shemeji, nikitoka basi nitakwambia tukutane wapi!"
"Mh!" Paulina aliguna kwenye meseji...
"Vipi tena, mbona umeguna shemeji?"

"Ah! Sasa tunakutana wapi, baa au? Maana baa nako macho ya watu…"
"We unataka wapi shemeji?"
"Popote lakini si baa."
"Kichakani je?"

"Aaah! Shemeji bwana! Kichakani kwani sisi ni mbwa mwitu!"
"Sasa wapi jamani shemeji?" aliuliza kwa mbwembwe baba Riziki…
"Pawe na utulivu halafu tuwe sisi wawili tu."
"Gesti au hotelini?"
"Mmm! Poa, hapo sawa."

***

Saa kumi na dakika arobaini na tano, baba Riziki mwili wote ukiwa kwenye chaji ya mahaba akimfikiria Paulina, meseji iliingia kwenye simu yake, akaifungua haraka akijua ni Paulina tu…
"Shem!"
Baba Riziki kwa kuwa alishatoka kazini na alikuwa akielekea kwenye taksi ili alifuate gari lake gereji, alimpigia Paulina…

"Haloo," alipokea Paulina…
"Halo shem, mambo?"
"Mambo poa. Vipi kazi?"
"Kazi poa. Nimetoka, nafuata gari baada ya hapo wewe njoo pale Sun City Hotel. Kama baada ya nusu saa tu njoo."

"Poa shem."
Paulina aliingia bafuni kuoga harakaharaka kisha akajipara vilivyo siku hiyo. Breki ya kwanza alipitia dukani, akanunua shati la rangi nyekundu…

Kazi imeanza! Je, baba Riziki atauingia mtego wa Paulina?
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-5

ILIPOISHIA
"Kazi poa. Nimetoka, nafuata gari baada ya hapo wewe njoo pale Sun City Hotel. Kama baada ya nusu saa tu njoo."
"Poa shem."
Paulina aliingia bafuni kuoga harakaharaka kisha akajipara vilivyo siku hiyo. Breki ya kwanza alipitia dukani, akanunua shati la rangi nyekundu…
NENDA NAYO SASA…

"Nikifika tu namvalisha hili shati," alisema moyoni Paulina huku akiingia ndani ya duka moja linalouza nguo za watu wazima.
"Nipe lile shati jekundu," aliamuru Paulina bila kujali ukubwa au muundo…
"Saizi gani dada?" aliuliza muuzaji kabla ya kumpa shati hilo.
"Saizi ya mtu mzima."
"Itakuwa XL."

"Haya nipe, shilingi ngapi?"
"Elfu kumi na tano."
"Nifungie."
Paulina alitoka na shati hilo kwenye mfuko huku akiwa amekaza macho kwenye simu yake akiamini muda wowote atapigiwa na baba Riziki. Alipoona kimya sana aliamua kumpigia yeye…
"Shem," alisema baba Riziki…

"Ee vipi shem?"
"Poa, nimetoka kazini, nikafuata gari mahali, sasa naingia hapa nilipokuelekeza, we uko wapi?"
"Nipo njiani kuja hapo. Kwani upo kazini shem? Maana kama ulisema uko likizo!"
"Kuna kazi muhimu sana nilikwenda kuifanya kwa leo na nimelipwa."
"Oke. Basi nakuja."

Baba Riziki alichukua chumba, akazama ndani na kukijaribu kwa kukaa kwenye godoro huku akinesanesa…
"Haiwezekani nikae naye humu ndani halafu nisibanjuke naye," alisema moyoni baba Rikizi.
Baada ya dakika tano tu, akapigiwa simu…
"Uko chumba gani shem, nimefika."
"Niko namba 111."
"Oke."

Paulina alikatiza kuingia ndani akitumia mwendo wa kuiba kwani aliamini lolote linaweza kutokea. Yaani anaweza kuonwa na mtu anayemfahamu yeye tu au anayemfahamu yeye na mumewe ikawa balaa.
Aligonga mlango namba 111 na kuzama ndani. Aliamua kujitoa ufahamu kwa kumvamia baba Riziki na kuanguka naye kitandani huku akimpiga mabusu mfululizo…
"Mmmwa….aaaaaa…aaa."

"Asante shemeji, lakini mbona umenihamasisha shemeji?" aliuliza baba Riziki.
"Kivipi shemeji?"
"Ulivyonilalia na kunibusu, mmh!"
"Umejisikiaje shemeji?" Paulina alimuuliza baba Riziki akiwa naye kwa ukaribu zaidi. Hapa na hapa!
"Mh! Shemeji umeona ee?"
"Aaah! Shemeji."

"Mmh! Shemeji bwana."
"Nini shemeji?"
"Aah! Shemeji."
Shemeji zilizidi mpaka ikafika mahali wote wakaangua kicheko cha chini kwa chini huku wakiendelea kutazamana kwa macho yaliyojaa mahaba mazito.
"Shemeji," aliita Paulina.

"Niambie."
"Nimekuletea zawadi."
"Ipi shemeji? Ninavyojua mimi ulisema tukutane ili unifundishe kuomba zawadi ambayo wewe unayo lakini mimi sina."
"Ndiyo hiyo niliyokuletea shemeji."
"Ipi shemeji?"

Paulina aliufuata mfuko wake na kutoa shati jekundu zuri sana…
"Nimekununulia zawadi ya shati shemeji," alisema.
"Daa! Shemeji bwana, kweli? Yaani umeamua kabisa kuninunulia shati shemeji yangu! Huu ni upendo wa ajabu sana shemeji," alisema baba Riziki akiwa analikaguakagua shati hilo.
"Ndiyo shemeji, nimeamua kukupenda wewe na roho yako na mwili wako."
Walicheka tena, safari hii wakajikuta wanasogezeana midomo na katika hali ya kutaka kupigana denda.

Kweli, hakuna aliyejizuia walijikuta wanazama ndani ya denda bila kuulizana wafanye hivyo au la! Walizama kwa dakika kama tano huku wakihema kwa kasi…
"Shemeji," aliita Paulina.
"Naam shem."
"Simama."

Baba Riziki alisimama, akasubiri maelekezo. Paulina alianza kumvua nguo moja baada ya nyingine huku baba Riziki akiamini hakuna bahati amewahi kuipata katika maisha yake kama hiyo.
Baada ya kumaliza kumvua nguo zote, Paulina alichukua shati alilolinunua na kumvalisha baba Riziki. Kwa hiyo baba Riziki akawa amevaa shati bila nguo nyingine yoyote, wakapanda kitandani.
Ilikuwa mchezo bila kuchelewa, waliingia uwanjani na kuanza mechi ya nguvu huku kila mmoja akijituma ili asionekane kuwa hawezi kitu.

Paulina alisema maneno mengi sana ya mahaba yaliyomfanya baba Riziki kuchanganyikiwa kwa penzi tamu hadi akatangaza muda huohuo kwamba anavunja dafu!
"Yes baby," alianza kuita Paulina baada ya baba Riziki kumtangazia na yeye akatangaza, wote wakavunja!

***
Asubuhi ya siku iliyofuata, Paulina alirudi kwa mganga wake kwa lengo la kumsimulia kilichotokea kwa baba Riziki.
"Nimefanikiwa babu," alisema Paulina kwa uso wa tabasamu pana.
"Ulifanyaje?"

"Nilimtongoza mwanaume mmoja, siku ya kukutana nilimnunulia shati jekundu halafu tukazini."
"Aaaa! Umekosea binti yangu."
"Kivipi tena babu?"
"Shati alitakiwa awe amenunua mwenyewe mwanaume, si wewe. Umekosea masharti.
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-6

ILIPOISHIA
"Nilimtongoza mwanaume mmoja, siku ya kukutana nilimnunulia shati jekundu halafu tukazini."
"Aaaa! Umekosea binti yangu."
"Kivipi tena babu?"
"Shati alitakiwa awe amenunua mwenyewe mwanaume, si wewe. Umekosea masharti."
IKAWAJE SASA?
Sasa babu, itakuwaje wakati nimeshampa penzi langu? Mbaya zaidi mwanaume mwenyewe ni mume wa mtu na mimi namuita shemeji."
"Binti umeshakosea masharti. Hata mimi wakati nakwambia sikumaanisha shati ununue wewe, hilo linakuwa halina dawa yangu."

Paulina aliganda kwa muda akiwaza ujinga alioufanya. Hakujua nini cha kufanya kwa wakati ule zaidi ya kutulia tuli akitafakari. Akili yake ilipokaa sawa aliamini kwamba alichokifanya siyo.
"Kwa hiyo sasa itabidi niwe nawasiliana naye kila siku namuuliza leo umevaa nini baby ili siku akiniambia amevaa shati jekundu ndiyo nikalale naye?"

"Sasa si atavaa lilelile ulilomnunulia wewe."
"Kwani hana jingine?" aliuliza Paulina.
"Hilo ulitakiwa kujua wewe, si mimi."
"Da! Inamaana nimtafute mwanaume mwingine tena?"
"Itakuwa bora kama kweli shida yako ni mtoto."

"Ndiyo! Shida yangu ni mtoto tu babu hakuna kingine ninachokitaka kwake."
"Sawa fanya kama nilivyokuambia."
Paulina aliaga kwa vile hakuwa na kitu kipya cha kukipata kwa mganga huyo, kama ni masharti alishayatoa ila aliyakosea taiming'.

Njiani aliamua kumwingiza akilini jirani mwingine, anaitwa baba Nyundo ambaye awali hakuwa kwenye mawazo yake. Alikumbuka mwanaume huyo ana mashati mekundu kama matatu kwani ana uhakika alishayaona katika mtazamo tofauti akiwa ameyavaa lakini pia baba Martha ana sifa za mganga, ndevu na rangi nyeusi zilitosha kumpa taswira.

"Lakini yule sidhani kama tutawezana naye, mbona namwonaga ni mkali sana! Nitamuweza kweli mimi?" alisema moyoni Paulina huku akimtafakari baba Nyundo.
"Kiukweli mara nyingi namuonaga kama mkali sana.

"Liwalo na liwe tu, hata kama ni mkali kwani ndiyo nini? Kwanza kwenye mapenzi ukali hakuna, siku zote watu wakali ndiyo wanaoangukia kwenye mapenzi motomoto…
"Na kama akijifanya mkali kwangu atakuwa amefika, nitahakikisha namuwekea mtego mkubwa hadi mwenyewe atashangaa na nafsi yake," aliwaza na kuwazua Paulina.

***

Siku hiyo alipofika nyumbani tu, meseji ya baba Riziki ikaingia kwenye simu yake, harakaharaka aliifungua na kuisoma…

"Vipi mpenzi, mbona upo kimya mwenzangu?" iliuliza.
Paulina aliipuuza kwa vile aliumia sana kuona amezini bure, lakini baada ya kukaa kwa muda akiiangalia ile meseji aliamua kumfungia kazi kwa kumjibu…

"Wewe jua ulipata ngekewa basi, angalia yako, siyo kunifuatafuata tena mimi, sitakiiii."
Meseji hiyo ilimuumiza sanasana baba Riziki, alianza kufikiria ni kwa namna gani alikutana na Paulina katika mapenzi makubwa halafu ghafla amebadilika na kumjibu vile, kila alichokuwa akikiwaza hakikumuingia akilini kabisa…

"Au ana Ukimwi nini, alidendadenda anipate ili aniambukize halafu aniachie gonjwa? Lakini ninavyokumbuka si tulitumia kinga? Au amechukia kwa sababu mimi ndiyo nilimlazimisha na kutaka matumizi ya kutumia kinga?" aliwaza sana baba Riziki pasipo kupata jibu.
Huku akijua fika kwamba ana mume wake, baba Riziki na yeye akamtumia meseji ya kumshambulia…
"Kwa hiyo umeona umalaya wako kwangu haunifai ndiyo umenitumia meseji ya kijinga kama hii siyo? Hata ufanyaje haina maana kwangu ni pumba tu."

Meseji hiyo ilimkera sana Paulina, akaanza kuhisi baba Rikizi ana lake jambo na hamjui vizuri, akamjibu…
"Unanitafuta siyo? Unajua kwa kiasi gani najuta kukutana na wewe kimapenzi? Unatambua kilichonitokea?"
Baba Riziki naye alipoisoma hiyo meseji, akamjibu…
"Najua unajuta kwa vile sikukutosheleza siyo?"
"Ndiyo."

"Kwa hiyo unatafuta mwingine wa kukutosheleza siyo?"
"Ndiyo."

"Kwa hiyo hata mumeo hakutoshelezi ndiyo maana ukanitafuta mimi nikutosheleze siyo?"
Meseji hiyo haikujibiwa na Paulina kwani ilimchoma sana moyoni mwake. Alihisi huenda baba Riziki anajua kila kitu na ndiyo maana anatoa majibu yale ya kumuumiza.

"Mbona kimya sasa, si unataka kutupiana maneno na mimi, si unajifanya kijike siyo, tuendelee. Na bahati nzuri hata meseji zako za mwanzo kabisa za kuniomba tukutane ili unifundishe zawadi ya kuomba ninazo, tuendelee sasa, ala! Mwanamke mzima ovyooo!"

Paulina alianza kujilaumu kwamba, ni kwa nini alimtumia meseji mbaya kiasi kile wakati anajua ukweli yeye ndiye aliyeanza kumtongoza baba Riziki, akaanza kujutia uamuzi wa kumjibu meseji vibaya…
"Kwani kama ningeamua kumjibu vizuri nini kingetokea?" alijiuliza mwenyewe na kujihukumu. Aliwaza sana na kuwazua hadi akapata ujanja wa kumjibu…

"Kwani wewe nani mwenzangu? Maana tunajibishana tu. Simu yangu ilipotea jana leo nimekwenda kununua nyingine na hii namba ni mpya kwa laini ileile ya zamani."

"Mh! Acha hizo? Kwani ulikuwa unamjibu ovyo nani vile kama ulikuwa hujui mimi ni nani? Unanijua sana hiyo janja yako tu."
"Please niambie basi."
"Baba Riziki."

"Ooo! Baby, sorry, hivi hapa nilikuwa nataka kufanya juu chini nipate namba yako maana jana usiku nimepoteza simu asubuhi nikadamkia kununua nyingine. Kisha nikafuata kununua laini nyingine hapa nilipo kila anayepiga namuuliza, kifupi nimeanza kusevu namba upya kabisa."
"Oke! Pole sana mpenzi wangu, sikujua."

"Pole na wewe kwa majibu yangu."
"Nimepoa. Sasa leo vipi tutaonana mpenzi? Maana penzi lako limeshanipa ulevi mkubwa sana hapa nilipo sijielewi kabisa juu yako."
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-7

ILIPOISHIA
"Oke, pole sana mpenzi wangu, sikujua."
"Pole na wewe kwa majibu yangu."
"Nimepoa. Sasa leo vipi tutaonana mpenzi? Maana penzi lako limeshanipa ulevi mkubwa sana."
JIRUSHE NAYO MWENYEWE…

"Muda gani baby wangu?"
"Jioni, maana mimi nipo tu mtaani."
"Poa, basi utanishtua," alijibu baba Riziki.
"Sawa baby wangu."

Paulina alipokata simu tu alisonya, akaiweka simu mezani huku akisema…
"Watu wengine bwana, yeye anajiona amefiiika! Mimi sina mapenzi naye, nilitaka mimba tu, sasa nimegundua nimevunja masharti anataka nini tena, naangalia mbele tu."
Mchana wa siku hiyo, Paulina alitoka kwenda saluni, ghafla akiwa anatembea Bajaj ikasimama pembeni yake…

"Wapi dada nikupeleke nipate japo chochote?"
Paulina alimwangalia dereva huyo kwa macho ya kumtafakari. Alikuwa amevaa shati jekundu, mweusi tii, ana midevu…

"Mh! Mbona ana sifa zote za kunipa mimba kama alivyosema mganga," alisema moyoni Paulina…
"Nakwenda Magomeni," alijibu Paulina ingawa ukweli alikuwa haendi huko. Alimwambia hivyo ili tu aweze kuwa naye kwa muda mrefu na kuangalia uwezekano wa kumpata.

"Kwanza huyu nikimpata hanipi shida, akinipa mimba hawezi kujua kwa hiyo mtoto atakuwa wangu maishani," alisema moyoni Paulina.Njiani, Paulina na vile alikuwa amekaa nyuma, alimwangalia dereva huyo kwa macho ya kumtamani hata kumvamia ili wamalizane kabisa…

"Tena leo nikilala naye tu mimba, maana niko kwenye siku za hatari," aliendelea kusema moyoni Paulina…
"Magomeni gani?" dereva aliuliza.
"Mapipa."

"Mapipa kubwa, wapi?"
"Kuna gesti moja inaitwaaaa….aaa ah! Jina limenitoka."
"Au Savannah Guest?" alisema dereva…
"Hiyohiyo…hiyohiyo, umejuaje kama nakwenda hapo suka?" alisema Paulina licha ya kwamba hakuwa akiijua gesti hiyo wala hakuwa na safari ya huko. Aliamua kutumia ujanja wake ili amnase dereva huyo mwenye sifa za mganga wake.

"Nimejua, ndiyo gesti ya wanawake wajanja wa mjini kama wewe. Una ahadi nini?"
"Nina ahadi ndiyo."
"Da! Watu wanafaidi kwelikweli jamani!"
"Kama nani?"
"Si huyo unayemfuata!"

"Kwa hiyo unataka ufaidi wewe siyo?"
"Mh! Mimi na wewe wapi kwa wapi! Sisi wetu wa uswahilini bwana."
"Ah! Kwani mapenzi yana makundi?" aliuliza Paulina huku akifurahia moyoni kwamba anakaribia kumnasa dereva huyo kijana.

"Yana makundi ndiyo. Sasa dada mzuri kama wewe uwe na mimi mlalahoi si maajabu hayo jamani," alisema suka huku akigeuka kumwangalia Paulina ambaye naye alipoona anaangaliwa, alirembua ili kumtamanisha dereva wake huyo.
"Hamna bwana! Kama huamini basi tushuke wote leo unifaidi wewe."
"Nini?" aliuliza suka huku akipunguza mwendo kama aliyetaka kusimamisha Bajaj.
"Wewe si umesema huwezi kunifaidi mwanamke mzuri kama mimi, sasa tushuke wote ili ukanifaidi."
"Kweli dada?"

"Kweli ee."
"Na huyo jamaa unayemfuata je?"
"Nitamwambia nimepata matatizo ya ghafla."
"Haa! Mwambie nione," alisema suka huku akisimamisha Bajaj pembeni.
"Sasa mbona umesimamisha Bajaj?"
"Ala! Kumbe…"

Bajaj ilianza kutembea tena, Paulina akajifanya anaongea na simu…
"Halo baby, nimepata dharura kidogo, ile ahadi yetu tuifanye kesho, samahani sana lakini…oke oke…nashukuru kwa kunielewa baby."
Baada ya Paulina kujifanya amemaliza kuongea alikaa kimya ili amsikie dereva huyo anasemaje. Ukapita ukimya kama wa dakika mbili nzima na wakati huohuo, suka naye akawa anaegesha Bajaj nje ya gesti.
Alishuka huku akiwa anatetemeka…

"Si hapa sista?"
"Ndiyo," alijibu Paulina huku naye akishuka lakini kwa aibu maana gesti hiyo ipo maeneo ambayo majirani kwenye nyumba zao hukaa nje na kuona kila kitu.
Alitaka kumwambia dereva wake wasiingie wakatafute gesti nyingine lakini sauti f'lani moyoni ilimwambia…

"Hakuna haja ya kuogopa, kwani wewe unataka mtoto au unataka mapenzi?"
Paulina akashuka, akatembea kuingia ndani huku akiangalia chini. Alijipa ujasiri kwa kujua kwamba hakuna aliyemfahamu maeneo hayo.

Walipata chumba, dereva akiwa haamini kabisa kilichokuwa kikiendelea. Yeye alihisi ni bahati ya mtende kuota kwenye jangwa!
"Hivi ni kweli?" alijiuliza mwenyewe.

Walivua nguo, kila mmoja kivyake huku dereva akijisikia aibu maana mh!
"Jamani hii dunia ina wanawake wazuri, hivi naota au ni hali halisi?" Dereva wa Bajaj aliwaza.
"Njoo baby kitandani," alisema Paulina akiinua mikono kumpokea dereva huyo.

Kwa kuwa muda huo dereva damu zilimuenda mbio si kidogo, akajaa mikononi mwa Paulina tii!
Sarakasi zilianza, dereva aliyekuwa mahiri katika sanaa ya mapenzi alimchumu Paulina midomoni na kwenye paji lake. Kufuatia swaga hizo Paulina akatabasamu.

Dereva huyo hakuishia hapo, alimzungusha na kumpiga vibao vya kimahaba maeneo yake ya nyuma, Paulina ambaye ilikuwa mara yake ya kwanza kufanyiwa hivyo alijisikia raha ya aina yake.
"Eh! Kumbe huyu suka anayaweza mambo, nilipanga nikipata mimba sitakuwa na habari naye lakini kwa hivi vimbwanga anavyonifanyia nitampa nafasi ya kudumu," Paulina alijisemea moyoni.

Kama vile dereva wa Bajaj alimsikia, aliongeza vionjo kwani aligusa kila kiungo chenye shoti ya umeme cha Paulina, mtoto wa kike akalegea kama mlenda.
Alipomuona dada huyo akihemea puani, hakuona sababu ya kumchelewesha.
Dereva huyo aliyepania kutoitumia vibaya nafasi aliyoipata ya kuwa na dada wa kishua kama Paulina, alionesha ufundi wake wa kusakata kabumbu.

Alimgaragaza vilivyo na kumfanya Paulina kumshangaa kwani alimuweza kuliko baba Riziki.
Paulina hakuchukua muda kujieleza kwamba anafika kwenye kilele cha mlima waliokuwa wakiupanda ambapo dereva naye akafika sambamba naye.
Paulina alifurahi sanasana, palepale akamuuliza suka…

"Hivi ikitokea umenipa mimba itakuaje? Maana tumeduu bila zana!"
"Aah! Haiwezekani mbona, mimi nina matatizo ya kutoweza kumpa mimba mwanamke!"
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-8

ILIPOISHIA
Paulina alifurahi sanasana, palepale akamuuliza suka…
"Hivi ikitokea umenipa mimba itakuaje? Maana tumeduu bila zana!"
"Aah! Haiwezekani mbona, mimi nina matatizo ya kutoweza kumpa mimba mwanamke!"
JIACHIE SASA…

Haaa!" Alihamaki Paulina, kidogo adondoshe machozi."Ina maana kwa huyu pia nimeingia mkenge?" Alijiuliza moyoni Paulina…

"Mbona umeshtuka sana?" Aliuliza yule dereva wa Bajaj..."Hata! Umenisikitisha uliposema huna uwezo wa kumbebesha mimba mwanamke."

"Ni kweli, nilipata ajali nikapata matatizo hayo. Inaniuma sana ndiyo maana siwazi kuoa maana najua nitamtesa tu mwanamke wa watu."
"Loo! Maskini, kwa hiyo utakufa bila kuwa na mtoto?"
"Ndiyo maana yake."

"Mh! Wewe kama mimi," Paulina alisemea moyoni.
Paulina alitoka kitandani, akaenda bafuni, alipotoka akamwambia suka waondoke…
"Lo! Hatupumziki kidogo mpenzi?" Aliuliza dereva.
Moyoni Paulina akamjibu…

"Tupumzike nini wakati huna uwezo wa kunipa mimba, we mjinga nini?"
"Noo! Nina haraka sana," alisema Paulina akiwa anavaa.
Ilibidi dereva huyo naye aingie bafuni kuoga kisha akavaa, wakaondoka.
"Mi niachie hapo kituoni tu," alisema Paulina kwa sauti isiyotaka utani.

"Mh! Mbona kama amebadilika?" Alijiuliza moyoni dereva baada ya kugundua kuwa, uchangamfu wa awali wa Paulina umepotea ghafla tu.
"Utapanda daladala?"
"Ndiyo."

"Kwani unawahi wapi mpenzi?"
"We tambua nawahi, usitake kujua ni wapi!"
"Oke, samahani sana," alisema suka huyo huku akisimamisha Bajaj kwani tayari alishafika kituoni alipotaka Paulina.

Paulina alishuka bila kusema asante wala baadaye kwa dereva huyo. Ilibidi amtazame kwa muda wakati akiondoka…
"Au sikumpatia sawasawa amenidharau?"
"Lakini si kweli, mbona alivunja dafu vizuri tu. Labda kama ametumiwa meseji imemchanganya. Lakini mbona sijamuona akishika simu? Ah! Atajijua mwenyewe bora ngekewa imeniangukia basi."

***
Ndani ya daladala kila aliyemwona Paulina alimshangaa kwani alikuwa akilia…
"Dada vipi, una matatizo gani?" Mwanaume mmoja aliyekaa naye kwenye siti moja alimuuliza…
"Niko sawa tu," alijibu Paulina…
"Uko sawa wakati unalia. Au wewe kulia ndiyo upo sawa, ukicheka ndiyo una matatizo?"
"Nani kakwambia?" Aliuliza Paulina.
"Si nakuona."

Paulina kabla hajamjibu alimgeukia yule mtu ili kumwangalia, akashtuka kumwona ana midevu, mweusi tii na alivaa shati jekundu na suruali nyeusi…

"Teh! Teh! Teh! Unajua kuongea kweli, yaani mimi nikilia ndiyo nipo kawaida, nikicheka ndiyo nina matatizo? Kuna mtu wa hivyo duniani?" Alichangamka Paulina baada ya kubaini mwanaume huyo ana vigezo vya kumpa mimba.

"Mtu wa hivyo duniani yupo na ndiyo wewe hapo."
Paulina akacheka tena, safari hii huku akijifuta machozi kwa kitambaa cha mkononi.
"Mimi nina mawazo yangu mwenyewe ndiyo maana nilikuwa nalia."
"Mawazo gani mrembo?"

"Ah! Basi tu. Unajua wakati mwingine ndoa ni chungu sana."
"Vipi, umeachika?"
"Sijaachika ila nakaribia."
"He! Mrembo kama wewe uachike, huyo mumeo ana macho kweli? Hajui kama ukisema cha nini, wenzio wanauliza watakipata lini?"
"Sijui mwenyewe."

"Kwani unaishi naye bado?"
"Ndiyo."
"Loo! Maskini. Akikuacha njoo kwangu, nitakuoa mimi."
"Kwani we huna mke?"
"Sina. Mke wangu alifariki kwa ajali mwaka juzi, bado sijaoa. Nadhani Mungu alikuwa na makusudi ya kunikutanisha na wewe mrembo."
"Huna watoto?"

"Watoto ninao, tena damu yangu kali sana, nilimzalisha mke wangu watoto watatu ndani ya miaka mitatu."
"Mh! Huyu ananifaa. Mimi ninachotaka ni mimba tu, si ndoa bwana," alisema moyoni Paulina.
"Labda uchukue namba yangu," alisema yule mwanaume. Paulina akaziandika kwenye simu yake kisha akambipu naye mwanaume akaziandika…

"Sasa mrembo, kama nyumbani hakufai si tungeshuka tukae mahali tuzungumze hata mawili matatu?" Yule mwanaume alimwomba Paulina…
"Poa," Paulina alijibu bila kuweka pingamizi.
Palepale mwanaume akamwomba konda kushusha kituo kinachofuatia. Hapo walishafika Tip Top!

Baadhi ya watu walishangaa kumwona Paulina akishuka na yule mwanaume baada ya mazungumzo ya muda mfupi wakiwa wameinamiana ndani ya daladala lile.
Walitembea kuelekea kwenye hoteli moja. Mwanaume alishaamua moyoni kufanya matumizi yasiyokuwa kwenye ratiba ilimradi ampate Paulina. Ni kweli alimpenda sana kutoka moyoni mwake…

"Hapa panatufaa au unasemaje?" Aliuliza yule mwanaume huku wakikalia viti vya kwenye baa ya hoteli hiyo…
"Bwana, kwa nini tusiingie kukaa kama chumbani hivi, hapa wanaweza kupita watu wanaonijua ikawa balaa kwa mume wangu," alisema Paulina. Lengo lake lilikuwa kwamba, wakiingia chumbani lazima wataduu! Kwa hiyo uwezekano wa kupata mimba kuwa mkubwa.
"Lakini kweli," alisema mwanaume, wakaenda kuomba chumba.
 
JAMANI KWANI LAZIMA?!-9

ILIPOISHIA
"Bwana, kwa nini tusiingie kukaa kama chumbani hivi, hapa wanaweza kupita watu wanaonijua ikawa balaa kwa mume wangu," alisema Paulina. Lengo lake lilikuwa kwamba, wakiingia chumbani lazima wataduu! Kwa hiyo uwezekano wa kupata mimba kuwa mkubwa.
"Lakini kweli," alisema mwanaume, wakaenda kuomba chumba.
JIONGEZE MWENYEWE SASA…
Ndani ya chumba, Paulina alionesha mapenzi ya dhati akiamini ndiyo siku ambayo atasaidiwa tatizo lake. Alimshika mkono mwanaume huyo na kumwambia…
"Nimependa sana rangi yako ya ngozi, inanivutia sana."
"Kweli?"

"Kweli kabisa, mimi mwanaume mweusi halafu awe na ndevu kama hivi yaani sipinduagi."
"Ina maana unazuzuka na weusi siyo?"

"Sana, napenda sanasana," alisema Paulina huku akimshikashika mwanaume huyo hali iliyoibua hisia kwake kwamba alikuwa anataka kuingizwa uwanjani ili mechi ianze.
Naye hakufanya ajizi, akaanza kutambaa naye kwa kumshikashika mwilini, kiunoni, kichwani, wakati mwingine alimwingiza vidole kwenye masikio, Paulina akashtuka sana na kulia kilio cha mahaba.
Mwanaume kuona hivyo akampandisha kitandani na kuanza kutambaa naye kwa kitandani sasa. Muda si mrefu, Paulina mwenyewe akaomba mechi ianze bila refa.

Ilikuwa ni bingiribingiri, mwanaume kwa vile hakuamini kilichotokea hadi kumpata mwanamke mrembo kama Paulina alijikuta akitumia nguvu ya ziada kumwonesha ufundi wake wote…
"Jamani, hivi kama iki…iki…" alitaka kusema Paulina akashindwa.
"Ulitaka kusema nini?"
"Nitasema tu."

"Sema sasa hivi basi."
"Ngoja kidogo lakini nitasema."
"Sema sasa."
"Mfano…mfano…"

Paulina hakumalizia akatangaza kuvunja dafu. Lakini mwanaume huyo ndiyo kwanza akashika kasi kwa kuingiza gia namba kubwa ili gari litembee vizuri. Paulina akamkandakanda mwilini ili kunogesha mechi, mwanaume wa watu akajikuta akitaka kupiga mayowe na kutangaza naye kwamba mambo yamekaribia, mara akafika kweli huku akipokelewa kwa usahihi na umakini wa hali ya juu, akatulia hapo.

Walitulia kwa muda wa kama dakika tatu nzima, kila mmoja alikuwa akihema kwa kasi.
"Mpenzi, ulitaka kuuliza nini muda ule?" aliuliza mwanaume.
"Hivi mfano, ukinipa mimba itakuaje?"
"Si mtoto atakuwa wetu au?"

"Kwani una uwezo wa kumpa mimba mwanamke?"
"Mimi, achana na mimi, nina damu kali sana."
"Nimefurahi sana kusikia hivyo, nitapenda sana uwe baba wa mtoto wangu siku moja," alisema Paulina huku moyoni akijua wazi kwamba kama atanasa mimba atampatia wapi kwani atabadili namba ya simu na akiulizia jina atamtajia la uongo.

"Ina maana unapenda sana mtoto au?"
"Napenda kama inavyokuwa kwa wanawake wengine."
"Basi kwangu umefika mama, hivi unaitwa nani?"
"Mimi?"

"Aaah! Nani mwingine jamani wakati tuko wawili tu?"
"Mimi naitwa Mage."
"Mage nani?"
"Mage Mathayo."
"Oke, mimi naitwa Ibra."
"Ibra nani?"

"Ibra Ibra."
"He! Yaani wewe Ibra, baba'ko naye Ibra?"
"Ndiyo."
"Kwa hiyo wewe ni Junior?"
"Ndiyo."

Walizungumza mengi lakini ndani ya moyo, Paulina hakuwa na mpango wa kuondoka kwenye ndoa yao ila alitaka mtoto. Na kwa nini alitaka mtoto vile, walishapima ikabainika yeye ndiyo tatizo. Lakini daktari alimwambia anaweza kunasa siku moja ndiyo maana akaanza hata kwenda kwa waganga.
"Nikwambie kitu Mage?" alisema Ibra.
"Niambie."
"Unajua mimi ni mweupe sana?"
"Kivipi?"

"Mimi nafanya kazi ya kuwasaka watu flani hivi ambao walifanya maovu miaka ya nyuma, sasa ili niwapate lazima niwe mweusi na madevu kama hivi lakini hii ni siri yako wewe tu," alisema Ibra huku akijishauashaua…

"Bado sijakuelewa Ibra, wewe ni mweupe kivipi sasa?"
"Si kwa rangi. Nimeamua kusema hivi ili kama utaamua kuwa na mimi uendelee kama utaamua kuacha basi uache."
"Kivipi sasa?"

Ibra alijishika sehemu fulani kwenye shingo akavua maski alilovaa na sura yake halisi ikaonekana! Akamwangalia Paulina huku akitabasamu…
"Mungu wangu, nitakuwa malaya mimi," alisema Paulina na kuanza kulia.
Kilio chake kilitokana na ukweli kwamba, alianza kujiona ni mhangaikaji kwani alishatembea na baba Riziki, akakosa sifa ya shati jekundu alilomnunulia yeye, akatembea na dereva wa Bajaj naye akamtangazia kwamba hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke, sasa Ibra naye alikwona mweusi, ana midevu kumbe alivaa maski.

"Sasa unalia nini Mage?"
"Nalia, najua mwenyewe."
"Kwa sababu mimi mweupe pee?"
"Hata, siyo sababu."

"Nini sasa, kwa vile nimekwambia nafanya kazi ya upelelezi?"
"Siyo hivyo, niache kwanza."
 
Back
Top Bottom