WABALLA Inc
JF-Expert Member
- Sep 2, 2014
- 2,711
- 1,018
Code:
Daudi1
Code:
Furahi day
Daudi1
Furahi day
Duh! inamaana Daudi1 unatu taste patience amma?
Tupiamo ka hadihi bhana!
Dah! mkuu sorry sijaweka toka ijumaa network ya tigo ilikuwa mbovu hivyo nikashindwa ila nimeweka zote mbili endele kupata uhondo
Nimeweka zote mbili mkuu ziko hapo juu ya ijumaa na leo
Karibuuu
JAMANI KWANI LAZIMA?-36
ILIPOISHIA
akakasirika sana. Alitoka kitandani kwa lengo la kwenda kumbeba Mozie na kumwingiza chumbani kwake japokuwa nguvu hizo hakuwa nazo...
Yaani huyu ameanza tabia gani ya kulala sebuleni? Alisema Stela akifungua mlango wa chumbani kwake na kwenda sebuleni...
ENDELEA KIVYAKO...
Khaa! Yuko wapi sasa? Au amekwenda kulala kwa Paulina? Si alisema atakuja kwangu? Ndiyo nini sasa? Alijiuliza Stela na kuamua kwenda moja kwa moja chumbani kwa Paulina ili kujua kama Mozie alikuwa kule au la!
Ngo...ngo...ngo, Stela aligonga mlango kwa nguvu...
Atakuwa nani huyo? Aliuliza Paulina...
Ndani ya nyumba hii tupo wawili, unadhani atakuwa nani kama siyo Stela? Alijibu mumewe...
Ngo...ngo...ngo, Stela aliendelea kugonga mlango.
Mozie alitoka kitandani, akiwa ndani ya bukta akafungua mlango...
Mume wangu kwani umeamua kuanza zamu kwa mwenzangu au amekulazimisha? Alihoji Stela...
Stela, aliita Mozie...
Abee.
Unajua kwa siku mbili tu nimekugundua wewe ni bogasi kabisa. Sasa sikia, sitaki niwe mume wako wala shemeji. Kama ni mtoto utazaa, nitamhudumia lakini mapenzi mimi na wewe mwisho leo.
Paulina alitoka kitandani haraka sana baada ya kusikia kauli ya Mozie, hakuamini...
Baby, mbona unamjibu vibaya Stela? Aliuliza Paulina akijifanya yeye ni mwema.
Namshangaa mke mwenzangu, hivi anaweza kunijibu mimi maneno machafu kama hayo. Eti mimi bogasi, bogasi mwenyewe bwana.
Hasira zilizidi kumpanda Mozie akamrushia kofi lakini Paulina aliliwahi kulizuia...
Paulina niache nimshughulikie huyu. Kwanza nimegundua nimedili na mtu asiye na akili timamu. Hivi we uliona alivyokuwa akizungumza mambo ya kijinga kuhusu wewe pale sebuleni? Anasema una ahadi na baba Riziki. Mara anasema sijui utumbo gani, mpaka nikamsema.
Sasa wewe unakerwa na nini niliposema Paulina anakwenda kwa baba Riziki, si alikuwa anakwenda kweli. Kwani uongo? Sema una lako jambo, umeshanipa mimba sasa unajiandaa kunitelekeza, alisema kwa hasira Stela.
Stela sikia, nenda kalale, mimi nazungumza kama dada yako sasa. Kalale asubuhi sana tutazungumza.
Stela aliondoka, akaenda kulala. Asubuhi kulipokucha, Mozie aliweka kikao kizito cha watu watatu, akaweka msimamo wake kwamba, yeye na Stela ibaki kuwa historia.
Na nataka nikwambia ukweli kwamba, wewe kaa hapa mpaka ujifungue. Kila kitu utapata...
Na hata ukishajifungua utaendelea kukaa hapahapa mpaka mtoto akue, alidakia Paulina. Stela alikuwa mpole baada ya kugundua kuwa, Mozie alikuwa siriasi na uamuzi wake.
Aliamini kitendo chochote kile cha kutaka kuweka ukorofi angeweza kukosa bara na pwani...
Sawa, alijibu kwa upole Stela.
Na sitapenda kusikia unamjibu vibaya Paulina, ni bosi wako kama zamani. Hii chukulia ni agizo na msimamo wangu kwako, sawa?
Sawa.
Saa kumi jioni ya siku hiyo, Stela alishikwa na uchungu akakimbizwa hospitali na Paulina kwenda kujifungua. Paulina alikaa nje baada ya Stela kupokelewa.
Baada ya kama saa tano kupita, nesi mmoja alitoka nje kwa Paulina...
Dada mgonjwa wako ameshajifungua, alisema yule nesi akimwambia Paulina...
Kweli, mtoto gani?
Wa kiume. Kwani baba wa mtoto ni Mwarabu?
Mwarabu?! Hapana, kwani vipi? Aliuliza kwa mshtuko Paulina...
Mtoto ni Mwarabu kwa asilimia mia moja. Una maana baba yake ni mswahili? Nesi aliuliza...
Si mswahili tu, ni mweusi japo si sana lakini ni mweusi wala si maji ya kunde, alisema Paulina huku moyoni akiombea uarabu wa mtoto huyo usipinduke hata marra moja.
Hii kwangu poa sana, Mwarabu? Ina maana Stela alikuwa anatembea na Mwarabu. Lakini ni Mwarabu gani atakuwa?
Paulina aliingiza wodini ambako Stela alihamishiwa baada ya kujifungua...
Hongera sana Stela, alisema Paulina.
Asante sana.
Hebu mfunue nimwone kidogo.
Stela aligoma kumfungua sura mtoto huyo...
Sitaki.
Khaa! Kisa nini?
Nimesema sitaki umbeya wako.
Baadhi ya wazazi waliokuwa hapo kwa ajili ya uzazi nao walishangaa sana, akiwemo nesi aliyemwita Paulina...
We dada mbona sikuelewi. Huyu si ndiye amekuleta? Alihoji nesi...
Hata kama, alijibu Stela kwa sauti yenye dalili ya kiburi.
Paulina palepale aliondoka, aliamua kurudi nyumbani...
Vipi za huko? Mozie alimuuliza...
Mwenzangu mbaya.
Ubaya wake nini?
Stela amejifungua mtoto wa kiume, lakini nilipoingia wodini amenigomea kumwona mtoto.
Kwa nini kagoma?
Mtoto Mwarabu.
Mtoto Mwarabu?
Mwarabu ndiyo.
We Paulina mwongo. Ulijuaje ni Mwarabu kama alikukatalia usimwone?
Aliniambia nesi.
***
Kesho yake saa tano asibuhi, Stela aliingia nyumbani hapo akiwa na mtoto wake huku akiangua kilio.
ITAENDELEA IJUMAAA...................