Jamani kumbe wabunge wetu umombo...Mmmmm

Jamani kumbe wabunge wetu umombo...Mmmmm

Speaker: "CAN YOU EXPLAIN YOURSELVES" kisha kamalizia " THANK YOU FOR YOUR REPRESENTATION!" wanamrepresent nani hapo mbele? OMG!
 
At least leo umeweza kuwa objective kwenye issue inaiyohusu chadema

Hata ninyi mnaonekana wengine humu 'kiingrereza' kinawapiga chenga, jamaa wa chadema amejitahidi kuzungumza 'grammatical english' CCM na CUF hawajui has been, have been na had been zinatumikaje, lakini pia wa CCM amejitahidi sana kutumia vocabulary nzuri
 
Kweli aibu kubwa sana imeonyeshwa pale bungeni tukianza na speaker.

Watu sio wadadisi na hawajiandai kwa interview.

Na jamani haya mambo ya wabunge kupitisha issue kwa kutamka jumla naona ni uhuni tu jamani.
Inabidi tuende kisayansi.Hii imetoka wapi?
 
Speaker: "CAN YOU EXPLAIN YOURSELVES" kisha kamalizia " THANK YOU FOR YOUR REPRESENTATION!" wanamrepresent nani hapo mbele? OMG!
 
lugha ni tatizo, lakini tatizo kubwa zaidi ni mtindo wa kupitisha bila kupingwa, hata pale ambapo kanuni zilipaswa kutoa muongozo.
 
Ha aha aha aha aha aha aha aha aha aha ahii kali
nami nimeinyaka!!!!!!!!!!!!!!
"i am an economist holding a masters degree in community development which i took it from______"ilibidi nibonyeze mute!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
MASWALI MADOGO MADOGO HAWAJUI:
kirefu cha SADC= JibU South Development Community
SADC ilianzishwa lini?= Jibu sijui
Eleza utawakilisha vipi Watanzania= eti nina Degree nimesoma ulaya, nimehudhuria semina na mabunge mengi Africa na duniani

Kasoro Mchungaji Msigwa kajibu vizuri na hata language barrier hana.
Wengine puuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

CUF ndio kabisaaaaaaaaaaa, eti yakhe mie takailisha urojo na gahawa, pia watwakilisha tende na halua , hovyoooooooooooooooooooo

Spika naye: SENKI YU, ENE KWESHENI TO HIM? HIM AU HON?

KANUMBA UNG'ENG'E UNG'ENG'E

WAKAJIFUNZE KWANZA.
Nashauri hizo nafasi bora zibaki wazi kuliko kupeleka aibu hii kwa Taifa letu.

Au bora wakazungumze kiswahili si ni ligha kubwa tu Africa na wakalimani wapo jamani, tuthamini chetu.

Spika: ENE KWESHENI?
wABUNGE : kIMYAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA, SIYO KWAMBA HAWANA MASWALI

iLA BABA Umombo, kutema yai, kazi kweli kweli.
 
Speaker: "CAN YOU EXPLAIN YOURSELVES" kisha kamalizia " THANK YOU FOR YOUR REPRESENTATION!" wanamrepresent nani hapo mbele? OMG!

Mimi Maimiuna! Itabidi aambatane na consultant akienda vikao vya Commonweath. Mikataba feki huanzia hapa
 
MASWALI MADOGO MADOGO HAWAJUI:
kirefu cha SADC= JibU South Development Community
SADC ilianzishwa lini?= Jibu sijui
Eleza utawakilisha vipi Watanzania= eti nina Degree nimesoma ulaya, nimehudhuria semina na mabunge mengi Africa na duniani

Kasoro Mchungaji Msigwa kajibu vizuri na hata language barrier hana.
Wengine puuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

CUF ndio kabisaaaaaaaaaaa, eti yakhe mie takailisha urojo na gahawa, pia watwakilisha tende na halua , hovyoooooooooooooooooooo

Spika naye: SENKI YU, ENE KWESHENI TO HIM? HIM AU HON?

KANUMBA UNG'ENG'E UNG'ENG'E

WAKAJIFUNZE KWANZA.
Nashauri hizo nafasi bora zibaki wazi kuliko kupeleka aibu hii kwa Taifa letu.

Au bora wakazungumze kiswahili si ni ligha kubwa tu Africa na wakalimani wapo jamani, tuthamini chetu.

Spika: ENE KWESHENI?
wABUNGE : kIMYAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA, SIYO KWAMBA HAWANA MASWALI

iLA BABA Umombo, kutema yai, kazi kweli kweli.

Mkuu hapa nilipo kuna baridi kali sana (winter hapa Ulaya sasa) lakini comments zako nimenifanya nicheke na kijasho kikatoka.

Umombo kama breaks za mbuzi kwa watanzania wengi, mbuzi haiendi kabisa. Kila mtu kimyaaa kabisa
 
Ivi ata zamani kulikuwa na ST Kayumba?
Alafu UKO SADC si waongee kiswahili alafu watatafsii maana mambo ya kujiuma unakosa confidence na point zinapotea
 
Kiingereza ni tatizo letu wa-TZ kwa ujumla hata wasomi hasa sisi wa zamani kidogo. Tatizo hilo linakuzwa na mazingira yetu ya kusisitiza kiswahili pekee katika shughuli za umma na pia mkanganyiko wa mtazamo. Wapo wanaosisitiza kutumia kiswahili tu katika elimu na hivyo kufanya kiingereza kuwa lugha ya watu wa matawi ya juu (elite/high class). Katika dunia ya leo, tunatakiwa kuzimanya vizuri lugha muhimu za kimataifa kiingereza kikiwa juu kikifuatiwa na kifaransa n.k. Haifurahishi kuona wawakilishi wetu wakiongozwa na Spika mwenyewe kuchukulia uwezo wa kutumia kiingereza kama vile ni mtihani mkubwa hasa na kuonekana wakipata taabu kujieleza kwa lugha hiyo. Hii inaonyesha huenda wakawa hata hawasomi au kusikiliza media za kimataifa.
 
Bunge letu kama litaamua kutumia kiingereza tutasevu pesa nyingi sana za wabunge kukaa muda mrefu kujadili mada moja kwa muda mrefu. Maana mswahili ukimpa nafasi kuongea kiswahili mpaka agongewe kengele na anazidi kubwabwaya akitaka aongezewe muda zaidi.

Leo nimeona wabunge wanaogombea nafasi za SADCC wakiona dakika tatu walizopewa ni sawa na saa nzima.

Mara baada ya kuuliza wabunge km wanamaswali na hakuna mbunge aliyejitokeza kuwauliza maswali mazito mazito, afadhali hata wabunge wa Chadema kina Tundu Lissu waliuliza japo maswali madogo ambayo pia yaliwashinda wagombea kuyajibu.

Spika alipowaruhusu warudi kuketi ktk viti vyao walishukuru mungu kwa kumwinamia spika kwa utii wa kijogoo.

kweli ni kichekesho km ungeona live ungtamani uzime tv.

yaani km yule zero wa katoon za kwenye magazeti, unaulizwa hiki unajibu kile km madenge vile.
 
Bintimkongwe sio suala la Lugha tu....Hivi inakuwaje mtu anagombea Ubunge wa SADC na anaulizwa kirefu cha SADC pia anashindwa?anaulizwa umoja huo una Nchi ngapi pia hajui?Je angeulizwa kwanini sasa ni SADC na ilipoanzishwa (1980) ilikuwa SADCC si angeona wanamtusi? Huyu mtu anataka kwenda huko kufanya nini?Inapaswa tuchague wapi walio serious,vinginevyo ni aibu ya Nchi.Wale wote Wabunge wageni Bungeni wanapaswa wawe watundu kujifunza mambo yanayohusu kazi zao.Tanzania ya leo sio ile ya Mwalimu....masuala ya kubebana lazima yaondoke na tuchague watu kwa merit.

Nakuunga mkono kwenye hoja..ila nadhani ni matokeo ya mchakato mzima wa kuwapata wabunge.Kigezo kikuu ni kujua kusoma na kuandika na siyo lugha ya kigeni wala taaluma. Kama hiki ndio kigezo tunategemea nini?
All in all nadhani mle Bungeni kuna watu wenye uwezo mkubwa tu tena na uelewa mpana wa maswala. Sasa kama hawakujitokeza nani wa kumlaumu? Lakini kama tunataka kuwa objective nadhani ni kitu kizuri kwa hawa wageni kupewa nafasi watajifunza mbele kwa mbele maana pia siyo kama hawana uwezo kiviiile kama watu wanavyosema hapa.
 
Swala la kimombo ni tatizo sehem nyingi dunian lkn hapa kwe2 mfumo mbovu wa elimu uliopo bongo nadhan wabunge wa sisiemu wamezidi hata grammar ya spika inatia huruma.....
Tunahitaji mabadiliko ya dhati na kweli ktk mfumo wa elimu hasa swala la lugha ya ufundishiaji mashuleni na vyuoni NI AIBU SANA KWA TAIFA kiongozi mkubwa kama spika kuongea broken ni bora tuzungumze kiswahili che2 tujue moja kuliko kukomaa na lugha tulizoungaunga shuleni.:nono:
 
Jamani WABONGO mmetizama session ya bunge leo walivyokuwa wanajinadi kugombea unaibu speaker na ubunge wa SADC? mtu unajinadi kuwakilisha nchi yako kwenye SADC lakini hujui hata kirefu cha SADC wala ilianzishwa lini? Mungu wangu!! such simple information which can be found any where! this means these guys take everything very simple. Hivi jamani hata ukiwa unaenda kwenye interview hujiandai hata kidogo? walau kujua a bit about what you are applying for? This is a bad joke!! Another surprise came when one of the MPs suggested that the contestants should express themselves in english. This became an excellent way of limiting their words and also limiting the number of questions to be asked. What a technique to cut long stories short!! Ni wachache wenye kujiamini kama kina tundu lisu ndo walitamba
 
sasa ndugu yangu kandonga hicho kiswahili ndicho tutaenda zungumza hukoo SADC? Nimeshtukia hata hizo safari wanazoenda nje ya nchi wanaenda tu kuwa mabubu. Wanatumalizia resources bure hawa. Lakini tusiseme sana tuwaache walau wavunje hivyo hivyo ndo kujifunza tena. Si unajua enzi za mwalimu kile kibao cha speak english if you don't wanna carry me? Tulikuwa tunabreak mwisho tukajua.
 
Lugha isiwe sababu, kizazi kinacho kua cha hawa Inglishi /akademi/inteneshno na wengine ,Lugha itakua sio tatizo,. tatizo ni mfumo uliowekwa wa elimu ya Tanzania , ulikua wa kukikuza kiswahili zaidi , kwa hizo hata hao SADC wanatakiwa waweke wakalimani na wa lugha ya kiswahili sio laizma kuongea kingereza.
 
Kwa Tanzania hakuna sababu yoyote kwa kiongozi kutojua Kiingereza kwa sababu ni lugha yetu official. Sheria zetu zote huandikwa kwa kiingereza, na hata gazeti la serikali huandikwa kwa kiingereza.
 
Ivi ata zamani kulikuwa na ST Kayumba?
Alafu UKO SADC si waongee kiswahili alafu watatafsii maana mambo ya kujiuma unakosa confidence na point zinapotea

Mkuu huwezi kutumia lugha yako ya nyumbani kama huna nguvu ya kutosha kiuchumi. China wameweza hilo kwenye G 20 sababu ya uchumi imara.

Sisi bado tunauza udongo kwa wenzetu na wao wanatuuzia vyungu baada ya kutumia huo udongo sasa unategemea nini.

Halafu hakuna sababu ya msingi ya kutojua lugha zingine...huko ni kujiendekeza tu. Nilipokuwa Switzerland nilikutana na watanzania wenzangu wanafanya kazi za uhudumu kwenye migahawa na walikuwa wana uwezo wa kuzungumza kijerumani, kiingereza na kifaransa kwa ufasaha kabisa. Hawa ni watu walioenda huko miaka michache iliyopita kutafuta maisha.

Kuna maafisa ubalozi wanakuja kwetu wakiwa na umri wa miaka 50 na zaidi na baada ya kukaa nchini kwa miezi miwili, tayari wanazungumza kiswahili vizuri na kwa ufasaha ikiwa ni lugha ya tano au zaidi. Wanajua kuwa hawawezi kutetea vema maslahi ya nchi zao bila kujua lugha kuu katika mahala husika.

UTATUZI sio kutumia kiswahili na kutafuta wakalimani. Tuache uvivu, tuanze kujifunza kiingereza, kifaransa, kijerumani, kihispanola, kichina n.k. Ni rahisi mno kama tusipojiendekeza.

Ilitakiwa watu wanaogombea ubunge sifa mojawapo iwe uelewa mzuri wa lugha za kigeni.

Ndio maana mawaziri wetu na wataalam wao wanashindwa kusoma mikataba nyeti. Kama English ya kawaida tu ni tatizo je ya kitaalam itakuwaje? Hivi lugha za kisheria, kichumi na kibiashara( Business English) itakuwaje kwa mtu ambaye kujieleza kwake ni

Ze ze honorabo supika, and ze my membazi of of of ze paliamenti of ze Tanzania. I want to vai for ze zis pozisheni of ze riprizentingi ze Tanzania paliamenti in ze Sadeki of ze paliamenti.

So i beg you to vote ze for me.!!!!!!!!

Lamberto!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom