Jamaa hawajui tenses!!!, wanachanganya badala ya past continuous tense yeye anasema past tense, hata speaker shida! Wa chadema amejitahidi anaonekana anajua tenses
Agreed. That wasn't an English class you people. Mimi niliona kipindi hicho live na kuridhika jinsi wengi wao walivyojieleza hasa kwa vile Kiingereza siyo Lugha yetu. Hali kama hiyo ingejitokeza pia endapo ungewataka Wajeremani, Wafaransa, Wachina au Watu wa Scandinavia wazungumze kingereza Bungeni mwao. Tatizo letu Watanzania tunapenda sana kuchunguza grammer kwenye spoken English kama vile tuko kwenye Mtihani wa Literature. Mtu akikosea kidogo basi tutacheka kama mazuzu. Ni rahisi kukosoa kuliko kutenda. Wengi wetu tungepewa nafasi ile ya kujieleza jana, hali ingekuwa mbaya kuliko tulivyoiona. Hata aliyeanzisha mada/post hii anajua Kihaya zaidi kuliko Kiswahili au Kingereza. Ni majigambo na ujinga tu ndiyo vinatusumbua.
Ningelikuwa mimi ningelijali zaidi knowledge ndogo waliyo nayo wabunge wetu juu ya hiyo SADC wanayotaka kwenda kutuwakilisha kuliko level ya kiingereza chao.
Kiingereza ni lugha ya wengine na kama hutumii kila siku na ghafla ukaambiwa ujieleze kwenye hiyo lugha utatababaika tu.
Ingelikuwa vizuri laiti wangelikuwa wazuri sana wa Kiingereza lakini sio the most important factor. Angalia wawakilishi mbalimbali hapa duniani, pamoja na lugha zao kutokuwa nzurri, hawajashindwa kufanya kazi zao. Hata katibu mkuu ya UN anaongoza baraza kwa kiingereza chake kisicho timamu na hujasikia wajumbe wakimcheka.
Watanzania tuna ujinga mwingi ambao tunaufumbia macho na kuweka nguvu zote kwenye nani anaweza kuongea Kiingereza bila makosa. Ukiangalia hata kiswahili tunaongea kwa makosa japo tuna confidence nacho na ambayo inaficha makosa kibao ya waziwazi.
Wabunge wajitahidi kusoma ili kuongeza uwezo wao wa kujua mambo ya dunia na challenges mbalimbali ambazo zinaikabili dunia kwasasa na namna ya kupambana nazo. Tupunguze hii ya nyama choma kila jioni na badala yake kuwe na muda wa japo kujisomea vitabu.
Eee bwana weee wacheni kukandia hao wabunge wetu kwa issue ya lugha.
Mimi huwa nahudhuria mikutano mikubwa ya kimataifa yanayohusiana na field yangu. Utakuta Professa limebobea kwenye taaluma yake lakini kwa vile amebadilisha lugha (labda from Spanish or French to English) basi na yeye huwa 'zis is zat is'. Lakini huwa anapewa heshima zote.
Muhimu ni mchango wake katika hilo bunge.
Mkuu mi mwenyewe nimecheka mnooo jinsi mdau alivyo m-quote speaker eti Senkiuu,enye q!
Ila kusema kua Africa tuna janga la lugha sidhani kama ni wote!nchi za west africa karibia zote wako poa kwa ngeli,east africa ni Tz tu yenye challenge coz KY,UG etc wote wanatema mbaya,south africa countries ndo usiseme!
Kuna haja watu wakaelewa kua hii luga ilikuja na MELI ila ni ya muhimu kinoma!
Wakati sisi tunahangaika na Ngeli wazungu wanahangaika na kujifunza kichina coz ndo itakayo lipa baadae!
Yaani speaker ndo kabisaaaaa hoi!
NB:Kingereza ni luga iliyokuja na meli!!!!kaaziii kweli kweli!ha ha haaaaaaaa
Ai Nooo!
Spikingi Inglishi izi noti izi iveni fo graduetsi.
Bati iti izi okee
ifu yuhevu pointi jasti go thea endi spiki yua brkeni ingilshi, ze mosti impotanti singi izi tu deliva ze messeji.
iveni Kenyani,hu wi sinki hevu guudi inglishi du spiki brokeni ingilishi tuu.
Ifi wani keni noti spiki inglishi theti izi noti a problemueti olu spiki awa bilavudi Kiswahili endi leti azazi heso tu transileti.
Hii hiii:becky::becky: