Mzee Mzima
Senior Member
- Mar 31, 2008
- 159
- 47
Naomba msaada kujua Kweli Salute ni nani anapigiwa kwani hapa naona anatoa salute wakati wa kumuaga Kanumba, I think this is not right, wanaojua please enlight me.View attachment 51467
Hapigi saluti hapo.Naomba msaada kujua Kweli Salute ni nani anapigiwa kwani hapa naona anatoa salute wakati wa kumuaga Kanumba, I think this is not right, wanaojua please enlight me.View attachment 51467
Wewe ndi hujui protocol za kijeshi...kijeshi maiti yeyote inapigiwa salute...sasa wewe raia haya mambo huyajui bora ukae kimya...
Za maadui je?Sasa mkiwa vitani utapiga saluti ngapi kwa wote watakaokufa?
Sugu ni kamanda.Mkuu mbona hata sugu kampigia salute SCK....
eti kuna mtu anauliza kuwa sugu ni kamanda?
nenda mbeya kaulize sugu ni nani?
baada ya jeshi kushindwa ukamada chadema imeamua kusimamia mambo yote yanayohusu ukamanda.
Ukweli ni kwamba Kova alikuwa sahihi kabisa kwa kitendo alichofanya na kwa ufafanuzi alioutoa na nimemkubali kwa elimu aliyoitoa kwani kisheria Saluti ni alama ya heshima kwa mkuu au mtu mwenye mamlaka juu yako. Kimsingi nyuma ya Majeshi yote duniani yana raia kama wawezeshaji wakuu wa uwepo wao. Katika mila na desturi za kijeshi Raia wa kawaida hapigiwi saluti isipokuwa kama yafuatayo yatajiri:" Saluti ya Kova kwa Kanumba yazua balaa"MSIBA wa msanii maarufu wa filamu nchini Steven Kanumba umezidi kuibua mambo, safari hii Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Suleiman Kova, amejikuta kwenye mjadala mzito, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Sambamba na hilo, kamati ya mazishi ya msanii huyo imesema kuwa imetumia sh milioni 70 kwa ajili ya gharama za kuuaga hadi kuuzika mwili wa Kanumba, huku mama mzazi wa msanii huyo, akiambulia sh milioni 4 za rambirambi.
Tukirejea kwenye sakata la Kova, kamanda huyo ameingia kwenye mjadala wa kifo cha Kanumba kutokana na hatua yake ya kuamua kutoa salamu za mwisho kwa kupiga saluti mbele ya jeneza la Kanumba.
Tukio hilo limeibua hisia mbalimbali miongoni mwa askari na wananchi kwa ujumla, huku kila mmoja akisema lake.
Baadhi ya askari na wananchi waliohudhuria hafla ya kuagwa kwa msanii huyo, walionyesha kushangazwa na kuhoji hatua ya Kova, kupiga saluti wakati wa kumuaga marehemu Kanumba.
Mmoja wa maofisa wa juu wa Jeshi la Polisi, ambaye hakupenda kutajwa jina lake, alibainisha kuwa Kova alichanganyikiwa kuipigia saluti maiti ya Kanumba kwani ni kinyume cha kanuni na taratibu za kijeshi.
Askari ukiwa umevaa sare katika misiba ya kijeshi ni sawa kuaga maiti kwa kutoa salamu ya kijeshi (saluti), lakini napo inazingatia na cheo husika kwa kweli kama siku hiyo Kova alikuwa amekusudia kumpigia saluti aliyekuwa mgeni rasmi, (Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Ghalib Bilal), ila katika kuaga mwili wa Kanumba, alikuwa amekosea, alibainisha ofisa huyo.
Baadhi ya wanaomjadili Kova wanahoji uhalali wa afisa huyo wa juu ya Jeshi la Polisi kutumia saluti katika kutoa heshima wakati salamu za aina hiyo hutolewa kwa polisi waliozidi vyeo.
Kwa upande wake, Kamanda Kova ametoa ufafanuzi wa saluti aliyoitoa wakati akitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa Kanumba.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Kova alisema anawashangaa askari wanaomshangaa kwani salamu hiyo ni ya kawaida tu katika nidhamu ya kijeshi.
Alisema kwa majeshi yote nchini, saluti ni salamu au heshima na alifanya hivyo kwa Kanumba kuonyesha heshima na jinsi alivyothamini kazi na mchango wake kwa taifa.
Alisema askari yeyote aliyevalia sale ya polisi kama anataka kusalimia au kutoa salamu kwenye shughuli kama ile ya Kumuaga Kanumba, lazima apige saluti.
Katika hali ya kawaida askari mdogo anapaswa kupiga saluti kwa askari mkubwa, lakini askari anaweza kupiga saluti kwenye tukio la kutoa heshima za mwisho kama nilivyofanya kwa mtu yeyote na sio lazima kwa askari kwa hiyo nilikuwa sahihi, alifafanua Kova.
Kwa mujibu wa Kova ni kosa kwa askari kutompigia saluti mkubwa wake, lakini sio kosa kwa askari yeyote kutoa heshima kwa marehemu hata kama aliyefariki ni mtu wa kawaida kama Kanumba.
Alisema siku ya kuuaga mwili wa Kanumba kulikuwa na watu mbalimbali na kila mtu alitoa heshima kuendana na utamaduni au imani yake, lakini kwake ilikuwa lazima apige saluti.
Nimesoma gazeti la Tanzania Daima leo habari hii na imenishangaza sana
Ukweli ni kwamba Kova alikuwa sahihi kabisa kwa kitendo alichofanya na kwa ufafanuzi alioutoa na nimemkubali kwa elimu aliyoitoa kwani kisheria Saluti ni alama ya heshima kwa mkuu au mtu mwenye mamlaka juu yako. Kimsingi nyuma ya Majeshi yote duniani yana raia kama wawezeshaji wakuu wa uwepo wao. Katika mila na desturi za kijeshi Raia wa kawaida hapigiwi saluti isipokuwa kama yafuatayo yatajiri:
i. Akiwa na cheo cha kisiasa ambacho moja kwa moja anamwakilisha Rais , Mfalme, Malkia au Mkuu wa nchi.
ii. Akiwa amefariki ambapo askari au Afisa bila ya kujali cheo chake hata kama ni CDF (Chief of Defence Forces) IGP
au Kamishna anapaswa kusimama kwa heshima na kuupigia saluti mwili kutoa salamu na heshima kwa Raia yule
ambaye kimsingi ndiye aliyekuwa mwajiri wake. Saluti kwa mwili haijalishi umri, jinsia, wala cheo cha marehemu
alipokuwa mzima wala rika la marehemu kulinganisha na anayeitoa saluti hiyo. Kwa maana hiyo askari aliyeiva
sawasawa kama Kamanda Kova na anayejua wajibu wake ataupigia saluti hata mwili wa mtoto mdogo ukiwa
umeandaliwa kwa mazishi au ukiwa safarini kuelekea huko.
iii. Katika nchi za kifalme Malkia na familia ya kifalme hupigiwa saluti.
NB: Ninayeandika haya ni Afisa Mwandamizi Mstaafu aliyehudumia JWTZwa zaidi ya miaka 40 hadi kustaafu miaka kadhaa iliyopita na aliyefanya mafunzo (Na kufundisha) ndani na nje ya nchi hii.
Changamoto: Maafisa na maaskari wa leo ambao awali hamkuwa mkijua hili kama huyo Afisa aliyenukuliwa na gazeti hilo mjifunze kutokana na somo alilolitoa Kova. Bravo Commander Kova.