Hapo mkuu nimejitaja mimi hasa ambaye sijui lolote kuhusu mambo ya anga, Kumradhi kama umeguswa ila lengo ni mimi hasa
Mmhhh, ndio maana nikasema wale vipanga wa Fizikia watusaidieUliingizwa chaka na mwalimu wako
Ha ha haaaa!Hiyo ndege utakuta fuel pump ina tatizo hivyo kupelekea kutoa moshi mweupe...
Huo ni uongo Mkuu, kama huelewi jambo ni vema ukae kimya kuliko kuleta stori za wajuba wa vijiweni
Ndege inamwaga mafuta wakati wa kutua kwa emergency tu. Na ndege zinazomwaga mafuta ni zile ambazo zilikuwa zifanye safari ya masafa marefu (long haul) lakini muda mfupi baada ya kuruka ikapata emergency inayomlazimu atue wakati bado ana mafuta mengi, na uzito wa mafuta, mizigo na abiria ni mkubwa akitua bila kupunguza uzito ataharibu landing gear. Pia wanaweza kumwaga mafuta kama emergency landing ina hatari ya moto, kwa mfano, kama landing gear imekataa kutoka na hivyo inabidi atue kwa tumbo. Atamwaga mafuta kupunguza uwezekano wa moto mkubwa. Na pia uzito mkubwa wa ndege maana yake umbali mrefu wa ku brake, kwa kuwa momentum inakuwa kubwa.
Ndege ya kwenda Mbeya kutoka Dar ikipata emergency hata eneo la Kibaha tu inaweza kurudi na kutua bila kumwaga mafuta kwa kuwa ndege huwa hawajazi mafuta kwa kusema weka full tank. Hata ndege ya kwenda South Africa inaweza kurudi na kutua bila kumwaga mafuta, kwa kuwa mafuta atakayokuwa amechukua sio mengi kiai hicho kwa safari ya masaa matatu ya kwenda Johannesburg
Hakuna pilot atamwaga mafuta baada ya kufika destination eti aliweka mafuta mengi au alipatwa na mgandamizo mkubwa njiani. Hizo n stori za vijiweni.
Ndege siyo lori mkuuHiyo ndege utakuta fuel pump ina tatizo hivyo kupelekea kutoa moshi mweupe...
Maelezo yako kwa asilimia kadhaa yameshabihiana na uongo tuliodanganywa enzi hizo.Kwa uelewa wangu huu mdogo, ila wanaojua zaidi watasema hii ni Ndege Kasi aina ya Concorde ambayo kwa Afrika inatua tu Cairo na Cape Town.
Ndege siyo lori mkuu
Hata mm sijui mkuu nilishazoea kunyonya mafuta kwenye carburetor kwa mdomo nmemeza Sana petrolHeeeeehhh.....kumbe? Hata unadhani nlikuwa najua basi? Hamna.
Yaani utafikiri mzee wako alikuja kwetu pia,na sisi tukiwa wadogo tuliambiwa na ndege kubwaaaaaaaa,haiwezi kutua hapa kwetuHii nadhani kwa Tanzania kila mtu ameshawahi kuona ikipita angani hasa pasipo kuwa na mawingu. Wakati mdogo, mzee aliniambiaga inaitwa roketi ni jamii ya ndege lakini Africa hamna uwanja wa kutua alafu ikitua humwaga mafuta Kwanza lakini niki-Google sioni story yake kwa anaejua nisaidie.
Ndege yenye Jet engine hutoa hizo Condensation trails, husababishwa na hewa ya moto iliyotoka kwenye engine inapokutana na hewa ya ubaridi, hupoa haraka na kutengeneza hilo kama wingu.
Rocket sio ndege wala haina uwanja wa kutua bali huwa na lauching pad, pia rocket husafiri vertical na sio Horizontal,
Rocket sio ndege bali ni chombo kinachotumika kupeleka vifaa kwenye sayari za mbali.



mweehBoss asante sana ,nimepata maelezo murua,watoto wakijilengesha wakaniliza nawamiminia materialKwa ufupi tu kinachotokea pale ni kwamba,kama umewahi kuishi sehemu zenye baridi kama Iringa au Mbeya kuna muda ukiamka asubuhi ukiongea unatoa moshi/mvuke mdomoni sasa basi hewa inayotoka mdomoni inakua ni ya moto kuliko inayokuzunguka nje. Hivyo inakua inalazimishwa kupoa itokapo mdomoni hapo ndipo unaona ule moshi ukipumua kupitia mdomo na ndivyo hivyo hivyo kwenye ndege zinazopita kwenye anga za kimataifa pale kunakua na baridi kali kwa hiyo hewa ya joto kali inayotoka kwenye jet engine ikikutana na baridi kali inalazimishwa kupoozwa hapo ndipo unapo ona ule moshi/mvuke.
Nadhani utakua umeelewa kwa ufupi mleta uzi
Swali konki sana hiliNgoja ngoja twende taratibu jibu na hili inakuwaje hapa duniani tunapata joto kali na huko juu kuwe na baridi kali wakati joto tunalolipata huku ndo linatoka huko..??????
Asante bossmweeh
Asante mkuuAnga la kimataifa ndo huko juu kabisa zinapopita hizo ndege kubwakubwa.. it means hakuna nchi inamiliki hilo anga isipokuwa Kuna kimo ukipita Kuna anga la kila taifa mfano tz .. sijui umbali exactly wa kwenda juu ndo inakuwa si anga lakimataifa ila nafikiri upo umbali huo.. so ukishuka chini ya huo umbali unakuwa umeingia kwenye anga la nchi fulani itategemea na upo nchi gani so wanahaki ya kukuhoji,kukuzuia usitue endapo wakitia shaka n.k..
Ahsante ya nini?Asante boss