Jamani hii kitu ni ndege ama nini

Jamani hii kitu ni ndege ama nini

Binafsi sijawahi kuona hii hali Tz, ila ughaibuni. Si ndege ya abiria au mizigo, nahisi kama sio chombo cha kijeshi, basi pengine ni cha utafiti. Baba yako anaweza kuwa sahihi kuwa ni rocket.
Tz huwajawai kuona ndege ikipita hivyo? Kwenu ni wapi?
 
Hii nadhani kwa Tanzania kila mtu ameshawahi kuona ikipita angani hasa pasipo kuwa na mawingu. Wakati mdogo, mzee aliniambiaga inaitwa roketi ni jamii ya ndege lakini Africa hamna uwanja wa kutua alafu ikitua humwaga mafuta Kwanza lakini niki-Google sioni story yake kwa anaejua nisaidie.

Mkuu hiyo ni ndege sema imepita mbali sana sana international flight at international sky
 
Ni kweli urusi ndio ilikuwa ya kwanza kutengeneza rockets za kwenda anga za juu na ndege kubwa kama antonnov,corncord,nk kipindi hiko marekani anasubiri kwenye rockets anga za juu
Concord sio mfaransa mkuu?
 
Kwa uelewa wangu huu mdogo, ila wanaojua zaidi watasema hii ni Ndege Kasi aina ya Concorde ambayo kwa Afrika inatua tu Cairo na Cape Town.
Sasa hizi habari za cairo na cape town ndio habari tulizoambiwa utotoni
 
Ngoja ngoja twende taratibu jibu na hili inakuwaje hapa duniani tunapata joto kali na huko juu kuwe na baridi kali wakati joto tunalolipata huku ndo linatoka huko..??????
Yes mkuu.. nishati ya jua inagawanyika katika makundi mara ifikapo kwenye uso wa dunia
Kuna ile ya kuvukisha maji (Latent Heat), nyingine ya kupasha joto hewa na vitu vyote vilivyo juu ya uso wa ardhi kama mimea, majengo etc na ile inayofyonzwa na ardhi

Pia nishati inayoingia katika uso wa dunia inakuwa na frequency kubwa na nguvu kubwa (shortwave). Ikishafika katika uso wa dunia na kuanza kugawanyika, nishati hii hubadilika kuwa na nguvu kidogo na frequency ndogo (long wave). Tabia za longwave radiation huwa ni kutengeneza joto.

Kwa kujibu swali lako ni hivi:
Nishati ya jua katika anga la juu huwa ni short wave hivyo haina joto lakini juwa likifika katika uso wa dunia hubadilika na kuwa longwave radiation ambayo hutokeza joto. Ndio sababu ya tofauti ya joto kati ya anga la juu na uso wa dunia..
 
Back
Top Bottom