Nilishajibu
Ndege inamwaga mafuta wakati wa kutua kwa emergency tu. Na ndege zinazomwaga mafuta ni zile ambazo zilikuwa zifanye safari ya masafa marefu (long haul) lakini muda mfupi baada ya kuruka ikapata emergency inayomlazimu pilot atue wakati bado ana mafuta mengi, na uzito wa mafuta, mizigo na abiria ni mkubwa akitua bila kupunguza uzito ataharibu landing gear. Pia wanaweza kumwaga mafuta kama emergncy landing ina hatari ya moto, kwa mfano, kama landing gear imekataa kutoka na hivyo inabidi atue kwa tumbo. Atamwaga mafuta kupunguza uwezekano wa moto mkubwa. Na pia uzito mkubwa wa ndege maana yake umbali mrefu wa ku brake, kwa kuwa momentum inakuwa kubwa.
Ndege ya kwenda Mbeya kutoka Dar ikipata emergency hata eneo la Kibaha tu inaweza kurudi na kutua bila kumwaga mafuta kwa kuwa ndege huwa hawajazi mafuta kwa kusema weka full tank. Hata ndege ya kwenda South Africa inaweza kurudi na kutua bila kumwaga mafuta, kwa kuwa mafuta atakayokuwa amechukua sio mengi kiasi hicho kwa safari ya masaa matatu ya kwenda Johannesburg
Hakuna pilot atamwaga mafuta baada ya kufika destination eti aliweka mafuta mengi au alipatwa na mgandamizo mkubwa njiani. Hizo n stori za vijiweni.