Jamani hii kitu ni ndege ama nini

Jamani hii kitu ni ndege ama nini

Huyo ni bwana mshana na kamati zake za jadi wanakuwa wanasafiri na ungo toka anga moja kwenye anga lingine
 
Duuh,Mkuu mababu zetu huwaga wasanii ila wakwako kazidi aisee,ningetamani nimuone,ok kwa kifupi hiyo ni ndege kubwa(jet) yaweza kuwa aina yeyote Airbus,Noon nk,kuhusu suala la kumwaga mafuta wakati wa kutua ni uongo,na pia Kama ukibahatika safiri safari za kimataifa huko Angani utaziona nyingi tu na ni ndege za kawaida,kuhusu u wanja kwa zamani ndege kubwa tulikuwa hatuna Ila Sasa hivi ndege yeyote yaweza tua DIA
Ndege huwa zinamwaga mafuta pindi zinapotaka kutua.
 
Hii nadhani kwa Tanzania kila mtu amesha wai ona ikipita angani hasa pasipo kuwa na mawingu.wakati mdogo mzee aliniambiaga Ina itwa loketi ni jamimi ya ndege laki Africa hamna uwanja wa kutua alafu ikitua humwaga mafuta Kwanza lakini Niki Google sioni story yake kwa anae jua isaidie

Picha na maandishi yajielezaj
 
ndege hiyo inapita internation air space ila kwa kuomba na wanalipia ushuru lakini kama nchi husika mna rada ya kisasa kama ambazo zimefungwa sasa tanzania ,zamani walikuwa wanajipitia tu bila ushuru bila kuomba kifupi nchi ilikuwa uchi kabisa

😎
 
Kwa ufupi tu kinachotokea pale ni kwamba,kama umewahi kuishi sehemu zenye baridi kama iringa au mbeya kuna muda ukiamka asubuhi ukiongea una toa moshi/mvuke mdomoni sasa basi hewa inayotoka mdomoni inakua ni ya moto kuliko inayokuzunguka nje kwa hiyo inakua inalazimishwa kupoa itokapo mdomoni hapo ndipo unaona ule moshi ukipumua kupitia mdomo na ndivyo hivyo hivyo kwenye ndege zinazopita kwenye anga za kimataifa pale kunakua na baridi kali kwa hiyo hewa ya joto kali inayotoka kwenye jet engine ikikutana na baridi kali inalazimishwa kupoozwa hapo ndipo unapo ona ule moshi/mvuke

Nadhani utakua umeelewa kwa ufupi mleta uzi
Umemaliza mkuu...
 
Ndege huwa zinamwaga mafuta pindi zinapotaka kutua.
Kweli ndege inapotoka point A to point B rubani ana calculate umbali ,speed per miles kiasi cha mafuta na uzito wa ndege hivyo kama amatembea vzuri na amefika destination alafu hali ya upepo ikawa na mgandamizo mdogo yaani upepo wa kubeba uzito wa denge wakati inatua isitue kama mzigo kupunguza mshindo inabidi apunguze mafuta ili kupunguza uzito wa ndege na kumbuka mafuta yana kaa kwenye mabawa na huwa ya funguka wakati wa kupaa ili kasi yandege kwenye run way inasaidia kuinyanyua ndege juu kwa kukata upepo na mabawa hufunga kuinama chini wakati wakutua ili upepo upite kwa kiasi hivyo ndege huwa nzito hivyo akiona ndege ni kubwa na hakuna hali nzuri ya kutua hupunguza mafuta kama yapo mengi lakini ni mara chache maana ndege hutembea kwa vipimo ili kumaintain uzito angani hakiona halimbaya ya hewa au hatari ya kuanguka hufungua mafuta yatoke ili ikianguka isilipuke nimekujibu kwa njia ya jadi lkn utakuwa umenielewa
 
Ngoja ngoja twende taratibu jibu na hili inakuwaje hapa duniani tunapata joto kali na huko juu kuwe na baridi kali wakati joto tunalolipata huku ndo linatoka huko..??????
Iko hv kadir unavyopanda juu ndo barid linaongezeka,mfano ukpanda mlima mrefu,
 
Ngoja ngoja twende taratibu jibu na hili inakuwaje hapa duniani tunapata joto kali na huko juu kuwe na baridi kali wakati joto tunalolipata huku ndo linatoka huko..??????
Kwa uelewa wangu, miale ya jua inavyokua inatoka kwenye source (jua) kuja ardhini huwa haichomi inakua na (long wave) bali kinachosababisha tuhisi tunaungua ni pale inapo hit ground ikiwa inarudi juu inakua na short wave hivo tuliopo ardhini tunahisi kuungua maana miale inapokua inarudi kwenye source (jua) inaanza kukutana na sisi tuliopo ardhini, na kadiri inavyozidi kurudi juu ndivo inapoteza nguvu inakua (long wave) hiyo ndiyo sababu huko anga la mbali inakua baridi na huku chini tunahisi joto, kwa anaeelewa zaidi atanikosoa , Asantee
 
Acheni stori nyingi, hizi ni ndege za kawaida ila zikimwaga mafuta ndo utaona hivo. Kwa siku hizi sio common ndege kumwaga mafuta ndo maana hizo picha hazionekani sana, ila zaman kidogo ilikuwa ni kawaida saana ndege kuwa na mafuta mengi na kutua viwanja visivo salama ilikuwa lazima ndege zimwage mafuta ndo maana tulikuwa tunaona hizo ndege kila mara, ila mara baada ya kuongezeka kwa usalama wa airports na teknolojia za safari then hiyo kumwaga mafuta ni kama imeisha except kwenye emegency landing tu utaona ndege ikiwa hivo
 
Back
Top Bottom