Jamani, Dr. Ulimboka yuko wapi siku hizi?

Jamani, Dr. Ulimboka yuko wapi siku hizi?

Sijui kwa nini, lakini nimejikuta nimemkumbuka Dr Ulimboka! Sijui anaendeleaje, afya yake anaendeleaje, na huduma yake ya udaktari anaendeleaje! Namtakia afya njema na maisha marefu!
 
aaah yupo lakiini kama hayupo sipati picha akipatwa raibu saanane itakuwaje
 
Atakuwa muhimbili a naendelea na kazi ya udaktari
Hakuwa daktari wa Muhimbili. Sikumbuki vizuri lakini ilikuwa international organisation. Alikuwa na solidarity tu na wenzie kwa sababu alikuwa kiongozi wao.
 
Dr.Ulimboka alitekwa katika awamo ya nne akapelekwa kuteswa mabwepande na baadaye kuokotwa, sababu kubwa ya kutekwa kwake inaelezwa kuwa ni kuwatetea madaktari kitu ambacho watawala hawakukitaka.

Yale aliyoyatetea Ulimboka yalipuuzwa na awamu iliyopita lakini ilipoingia awamu mpya Cha KwanZa ilitaka kuweka mazingira ya huduma za afya kuwa mazuri japo baadaye kasi ya utoaji huduma bora imeshukwa kwa kukosekana motisha kwa watoa huduma, kukosekana kwa madawa na vifaa vya kutolea huduma.

Yamkini waliomtesa wanatibiwa au ndugu zao wanatibiwa na madaktari walewale aliokuwa anawatetea Ulimboka, yamkini waliohusika Leo hii damu ya Ulimboka inawatesa huko walipo na hakuna anayewasikiliza. Yamkini walioandaa hizo njama leo hawathaminiwi na wanateseka kwa ufukara ila mteswa amebaki Shujaa kwenye jamii.

Natamani kusikia alipo Shujaa huyu na ningetamani kujua wale waliotuhumiwa kumteka walifanywa Nini?
 
Huyu Daktari alipata madhara makubwa kule Mabwepande na baada ya kunusurika kifo, aliaahidi kuwa atasema kila kitu kuhusu watesi wake.

Kutokana na mateso aliyoyapata daktari huyu, gazeti moja maarufu lilifungiwa kwa kutoa habari za mhuka mkuu wa kadhia hii ambaye lilidai yuko Magogoni.

Sasa huyu daktari amepotea wala haongei tena. Je yuko wapi na je anaendelea na kazi yake ya udaktari au bado anajipanga kutoa taarifa kamili?

Kuna daktari mwenzake mmoja naye alipata madhara makubwa ya kupukutika ngozi na kunyonyoka nywele ambapo alikwenda kuponea India.

Rafiki yake mkubwa aitwae Six akapita sehemu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kanisani na kutangaza kuwa rafiki yake amepewa sumu. Dr mwenyewe aliporudi baada ya kunusurika kifo aliaahidi kuwa ataweka mambo hadharani. Wakati anaendelea kutangaza kuwa ataweka mambo hadharani, tukasikia ghafla kapewa uwaziri.

Kuanzia hapo akasitisha matangazo ya kuwa ataeleza kilicho mpata na hivyo kumfanya rafiki yake Six kuonekana ni mnafiki na mwongo mkubwa. Sasa hicho kimya chake kinaeleweka kwani keshapewa fidia.

Sasa rafiki yangu "Dr. Mabwepande" kapewa nini hadi awe kimya namna hii na kusahau ahadi zake?!
Nipo mkuu..una shida gani na mimi?
 
Back
Top Bottom