Jamani, Dr. Ulimboka yuko wapi siku hizi?

Jamani, Dr. Ulimboka yuko wapi siku hizi?

Kwa hiyo wewe uliyepoteza ndugu yako kutokana na mgomo unasemaje ni vema yale aliyofanyiwa Dr. Ulimboka?

Hata angeuawa kwa Makombora ya kutungulia Ndege bado ilikuwa ni adhabu ndogo! Mungu amlaani na amdhalilishe zaid ya alivyofanyiwa Mwanaharamu Mkubwa yule
 
Wana jamvi,

Naomba kuuliza alipo Dr. Ulimboka. Mara ya mwisho nilimsikia alivorudi toka matibabu. Tukasubiri press conference lakini hadi leo sijasikia allishia wapi.

Mtu yeyote mwenye kujua huyu bwana yuko wapi na anafanya nini sasa hivi anisaidie.
Labda wengine mtaniuliza kwanini nauliza au ananihusu nini.

Kiukweli nimemkumbuka tu kama binadam mwenzangu na kwa vile habari zake zilivuma enzi hizo sio vibaya kujua anaendeleaje huko alipo.
Mnaanza hapo...
 
la

lakini wao nao si walikuwa na madai yao?

Ni Haki Askari Magereza kugoma Kulinda Wafungwa kwa kuacha wazi Mageti ili Wauaji, Wabakaji na Majambazi kutoroka na kuja kusumbua Mitaani kwa kuwa tu wana madai Yao Serikalini?
 
sio haki mkuu

Basi huo Mfano ndio sawa na alichofanya Yule Mtoto wa Kinyakyusa, Ana Roho ngumu sana sana sana.

Aliamuru Wasakamwe hata wale waliokuwa walau roho za huruma zinawashika kwa kutoa japo Msaada kidogo halafu yeye hakuwa Mtumishi wa Umma
 
Ni Haki Askari Magereza kugoma Kulinda Wafungwa kwa kuacha wazi Mageti ili Wauaji, Wabakaji na Majambazi kutoroka na kuja kusumbua Mitaani kwa kuwa tu wana madai Yao Serikalini?
sio haki mkuu,lakini kama RC ana haki ya kumweka ndani daktari ww huoni hiyo ni hatari na udhalilishaji mkuu ?
 
Nakuombea kwa Mungu Siku ukiwa na Mgonjwa wako wa karibu sana ndipo na Madaktari nao wagome ndio ujue hasa Madhara ya Yule Muuaji Ulimboka ambae hakupaswa kuwa anaishi mpaka sasa!

Kuna Mama/Dada/ wake wa Watu wamefia kwny Ward za uzazi kwa kukosa tu daktari wa kuwafanyia Operation ndogo sana ya Uzazi!

Dhulma na hujuma aliyowafanyia Wanyonge wa Nchi hii hakika atasimama kujieleza Mbele ya Mwenyezimungu
Unatambua kuwa madaktari kama wafanyakazi wana haki ya kugoma? Unaniombea niwe na mgonjwa halafu madaktari wagome, mimi nakuombea ukafanye kazi yenye malipo kiduchu ili ujifunze kuwa kuna wakati inabidi udai haki yako kwa namna ambayo itawaumiza waajiri wako na wateja. Mimi sipo ktk sekta ya afya wala sina maslahi ya moja kwa moja zaidi ya kuwa mgonjwa mtarajiwa, sipendi niende hospitali nikose huduma, lakini sipendi zaid dhuluma zinazofanywa na dola dhidi ya mtu mwenye haki na jambo fulani. Dhuluma za namna hiyo zikiendekezwa, sisi watoto wa maskini tusio na connection za chama tutapata shida sana.

Mwisho nisisitize kuwa, tukitaka maendeleo ya kweli ktk sekta yoyote, tuache kutumia mabavu, tutumie akili, busara na ustaarabu.
 
Nikisoma dhihaka kama zilizojaa katika uzi huu huwa nahitimisha kwa kukubaliana na falsafa ya Wafaransa Joseph de Maistre na Alexis de Tocqueville kwamba huwa tunapata serikali tunayostahili. Inashangaza sana lakini ndio hali halisi ya Watanzania wengi.

Kwa kifupi, ni jamii yenye hulka ya kutii na kuabudu mamlaka iliyopo kwa yote watakayotwishwa. Iwe ufisadi kama wa awamu zilizopita (hasa 3 na 4) au udikteta kwa gia ya kusafisha "uozo wa kutisha" wa hizo awamu zilizopita pamoja na zenyewe kuabudiwa sana nyakati zake. Bila shaka kabisa, kesho akiingia Ikulu mwenye kuuza nchi kabisa ataimbiwa mapambio ya sifa kiasi cha kutuacha wengine tukichanganyikiwa kabisa.

Hiyo ndiyo Tanzania halisi. Mara nchi ya uchumi wa gesi; mara ya viwanda, mara ya uchumi wa kati, n.k. Mara misaada ni muhimu kutuwezesha kula; huko nje hela ni nyingi sana - ni kiasi cha kuomba tu. Mara hatuitaki misaada yao; sisi ndio tutakuwa watoaji wa misaada. Waimba mapambio ya sifa wa awamu zote hizo ni walewale! Kama vile ni nchi ambayo raia wake wengi ni aina ya yale "ma-jokeri" ya kwenye karata.
 
yupo south Africa anandelea na kazi take ya udaktari. jk alimfanya kitu mbaya Hana hamu na tz
 
Nakuombea kwa Mungu Siku ukiwa na Mgonjwa wako wa karibu sana ndipo na Madaktari nao wagome ndio ujue hasa Madhara ya Yule Muuaji Ulimboka ambae hakupaswa kuwa anaishi mpaka sasa!

Kuna Mama/Dada/ wake wa Watu wamefia kwny Ward za uzazi kwa kukosa tu daktari wa kuwafanyia Operation ndogo sana ya Uzazi!

Dhulma na hujuma aliyowafanyia Wanyonge wa Nchi hii hakika atasimama kujieleza Mbele ya Mwenyezimungu
Kwani yy alifanya kosa gani Kama ngomo ule ulifuata taratibu zote za mono... Unatakiwa kuilaumu serikali kwakushindwa kutimiza wajibu wake... Nasi kufuaraia mtu kuteswa vile
 
Back
Top Bottom