Inafurahisha sana kuona watu wanamcheka na kumkebehi Dr. Ulimboka. Ya Mungu mengi, naamini wale aliokuwa anawapigania dhamira zao zitawahukumu milele. Tusishabikie fujo na mabavu, mbona Kenya madaktari wamegoma miezi mitatu sasa na hakuna aliyekatwa korodani? Hatuoni aibu kwamba wenzetu wanasuluhisha mambo yao kistaarabu? Kumtesa mtu kwa kudai haki yake ni ujima wa hali ya juu.
Kamwe sitashabikia mateso kwa watu wanaodai haki zao. Watu waliozoea kutesa hawachagui. Juzi ilikuwa kwa daktari, leo kwa mwanamziki, kesho mwanasiasa, kesho kutwa mshabiki wa siasa, wiki ijayo zamu ya wafanyabiashara, mwezi ujao zamu ya wakulima. Tukemee vyombo vya dola vinavyofanya kazi kihuni(e.g. sodomy), hakuna kiumbe-hata mbuzi, anayestahili kufanyiwa hivyo.